Friday, February 24, 2017

Mambo matatu Yanayokwamisha Malengo Yako - Joel Nanauka

Joel Nanauka
Kuna watu wengi sana wanaokufa na vipaji vyao,wanakufa na uwezo wao ambao kama wangeutumia basi ungeweza kuwasaidia sana kubadilisha maisha yao.Hata leo unaposoma makala hii,ndani yako kuna vipaji na uwezo wa kukufanya ufanikiwe kama utaanza kufanya mambo ambayo yamewasaidia wengine kufanikiwa pia.Katika saikolojia ya mafanikio imegundulika kuwa watu wengi wanapokuwa wazee sana huwa wanajilaumu kuwa hawakuishi maisha waliyotakiwa kuishi na walipoteza muda kutofanya yale ambayo yangeweza kubadilisha maisha yao.

Wengi waliohojiwa wakiwa wazee sana huwa wanasema wanatamani kupata fursa ya kurudia umri mdogo tena,na kama wakiipata hiyo fursa basi wataishi maisha yao kwa namna ya tofauti sana na vile ambavyo waliishi miaka yao yote iliyopita.Hii inaonyesha kuwa kama na wewe pia hautajua mambo ya kuyafanya kwa sasa unaweza kuingia katika kundi la watu ambao watakuwa wanajilaumu mara watakapokuwa wazee.

Nawe najua unasoma makala hii kwa sababu unatamani kufanikiwa kufikia kilele cha ndoto yako,lakini ukweli ni kuwa kama hautakuwa tayari kuchukua hatua madhubuti basi itakuwa ngumu sana kwako kufanikiwa.Uamuzi wa kufanikiwa hakuna mtu anayeweza kukufanyia isipokuwa wewe mwenyewe.

Mara nyingi uamuzi wa namna hii unaweza kutokana na kutaka kuepuka shida fulani au kutamani kupata raha fulani.Wengi waliofanikiwa walihusisha kitu kimojawapo kati ya hivi viwili.Kuna ambao walipitia hali ngumu sana katika maisha yao na kwa sababu hiyo walijikuta wamefika sehemu wamechukia maisha ya umaskini na wakakata shauri ndani ya mioyo yao kuanza safari mpya ya mafanikio,hawataki kabisa aidha wao au ndugu ama watoto wao wapitie hali ya mateso ambayo wao wamepitia.Wengine ni wale ambao waliishi maisha ya kawaida tu lakini wameona jinsi watu wengine ambavyo wamefanikiwa katika maisha yao na wao wametamani kuishi kama hao wengine.Katika maisha hakuna mtu anayefanikiwa kwa bahati mbaya,hata wewe kama unataka kufanikiwa ni lazima uamue kuanzia leo.

Swali la msingi ambalo ni muhimu kujiuliza ni kuwa;hivi kwa nini watu wanayajua haya ila hawachukui hatua?Leo nataka tuziangalie sababu kubwa 3 ambazo zimekwamisha malengo ya watu wengi:

Hofu ya kufanya jambo jipya

Ni ukweli ulio wazi kuwa kila mtu huwa hapendi kuondolewa kutoka mahali alipopazoea.Hii ndio maana kuna watu wakienda kanisani kila jumapili watakaa upande huohuo na wengine kiti kilekile na wakikuta kuna mtu amekaa huwa wanaona kama vile wamekalia kiti chao.Hata nyumbani,ukichunguza vizuri kuna watu huwa wanakaa kochi hilohilo ama kiti hichohicho wakati wa kula hata kama hajawahi kupangiwa kuwa akae hapo.Ndivyo ilivyo katika maisha ya kawaida watu wengi huwa hawapendi kubadilika.Kuna watu kila wakienda na kurudi kazini wanapita njia ileile kwa miaka nenda rudi,hata kama kuna njia nyingine hawajawahi kujaribu kabisa

Hebu jichunguze kitu ambacho unakifanya kwa sasa hivi umekuwa ukikifanya kwa muda gani na kwa nini haujabadilisha hadi leo.Leo fikiria kuna kitu gani kipya ambacho unaweza kuanza kukifanya kwenye maisha yako?Usikubali mwaka huu uiishe kabla haujaanza kufanya kitu kipya tofauti na unachofanya sasa hivi.Tajiri mkubwa wa marekani aliyekuwa anamiliki viwanda vya magari Henry Ford aliwahi kusema “Kama ukiendelea kufanya mambo yaleyale ambayo umekuwa ukifanya sikuzote basi utapata matokeo yaleyale ambayo umekuwa ukiyapata”.Je,unataka kuanza kuishi maisha ya tofauti?basi anza kufanya mambo ya tofauti kuanzia leo.

Hofu ya Kufeli/Kushindwa

Sababu nyingine inayowafanya watu washindwe kufanikiwa ni ile hofu ya kushindwa.Kuna watu wengi sana ambao wameogopa kufanya jambo fulani kwenye maisha kwa sababu ya hofu ya kuwa watashindwa.Mara nyingi,wazo la kwanza ambalo watu huwajia katika akili yao inapofika kufanya jambo fulani huwa ni “itakuwaje nisipofanikiwa?”.Kuna watu wanaogopa kufanya biashara kwa sababu ya kuwa na hofu ya kupata hasara,kuna watu wanaogopa kuomba kazi mahali kwa sababu ya hofu ya kukataliwa,kuna watu wanaogopa kuanza kulima kwa sababu ya hofu ya kupata hasara. Mtu mmoja mwenye hekima aliwahi kusema “Kila kitu ambacho kwa sasa hauna na unakitaka,kipo upande wa pili ukishaivuka hofu”.Mafanikio yako yamejificha nyuma ya hofu inayokukabili.

Kama kweli unataka kufanikiwa katika maisha yako ni lazima uanze kuishi katika namna ambayo hofu ya kufeli haina nafasi.hebu jiulize leo,kuna mambo mangapi ambayo unatamani kuyafanya lakini kinachokuzuia ni hofu ya kushindwa?Leo anza kuishinda hofu hiyo na anza kuchukua hatua mara moja.Kuanzia leo ningekushauri kutumia kanuni hii aliyowahi kuisema mwandishi maarufu sana wa marekani Jack Carnfield aliposema –‘Usiogope kufeli bali ogopa mafanikio ambayo unaweza kuyakosa unapoogopa kujaribu”

Kutumia visingizio vya kutokuwezekana

Jambo la tatu linalosababisha watu wafeli katika maisha yao ni ile hali ya kutumia visingizio walivyonavyo katika maisha yao.Wengine watatumia visingizio vya kutokusoma/kutokuwa na elimu ya kutosha,wengine watatoa visingizio vya hali mbaya ya uchumi,wengine watatoa visingizio vya familia walizotoka,wegine watatoa visingizio vya kukosa mitaji n.k.UKweli ni kuwa wakati wowote ule ukitaka kupata visingizio vya kutofanya jambo fulani basi utavipata vingi sana,ila kama kweli unataka kufanikiwa ni lazima uamue kutokuwa mtu wa visingizio kabisa katika maisha yako.Mkufunzi wa mafanikio wa Marekani Jim Rohn aliwahi kusema “Kama kweli unataka kitu utatafuta namna ya kupata,ila kama hautaki basi utatafuta visingizio”.Ukiona unatoa visingizio vingi ni kwa sababu bado haujadhamiria kupata unachotaka.

Kuna mambo mengi leo ukiulizwa kwa nini huyafanyi ututaanza kutoa visingizio,kumbuka kuwa kila unapotoa visingizio unapoteza uwezo wako wa kutatua changamoto inayokukabili.Kuanzia leo amua kuwa mtu ambaye hautoi visingizio na badala yake uwe mtu wa kuchukua hatua.Kuna Watu wanatoa visingizio kila siku;watamlaumu mzazi,ndugu ama rafiki.Kama uantaka kufanikiwa basi wewe usiwe mmoja wao.Amua kuachana na visingizio kuanzia leo na anza mar amoja leo kufanya hiyo biashara, kilimo n.k Chukua hatua.

See You At The Top

©Joel Nanauka



Thursday, February 23, 2017

THE SERVANT GIRL OVERCOMING

Last Sunday's message at #CityHarvest.

THE SERVANT GIRL OVERCOMING

2Kings 5:1-18:

Naaman was a great man with great disease that needed a great cure. His transformation happened because of the servant girl. She had to overcome the following:

1. Prejudice: Preconceived opinions not based on reason.

2. Indifference: Lack of interest - the non of my business mindset.

3. The barrier of non- involvement: Let someone else do it.

4. Inadequacy: Am too young, too old, etc

5. Timidity: Being too afraid to share the message with different people.

Just like the servant girl, Christians have to overcome these obstacles in order to spread the gospel of Jesus Christ.

Saturday, February 18, 2017

WE ARE CREATED TO WORSHIP GOD by Pastor Rogers Namwenje

Everyone that has breath must Praise God

1 Corinthians 10: 31

Isiah 43:7

"Whom I created for my glory"

We are created to glorify God

We are created to worship God

God created man in his own image ,and command a man to multiply

One of the feature that we see in the image of God is GLORY

Whenever man multiplies the world is filled and because they have with them the Glory of God, meaning the World will be filled with Glory of God

We are created to make God Happy

We are created to excite God

We are at our best when we Glorify God

Bringing Glory to God is our business

In whatever we are doing let it be for the Glory of God

Our purpose is to glorify God

Let people knows we are serving the Mighty God

The art of worshiping is giving Glory to God

Where Do we Worship God?

Do We only worship God in the praise and worship session in our church?

Worshiping God is not in church only

Worshiping God is something we should do every single day

Worshiping God must be our lifestyle

Two things happen when we worship God


1.We worship God Collectively

2. We translate our service by our words

Worshipping God is not by singing only but by our WORDS

Words like GOD YOU ARE GREAT for something that has happened in your life

Maybe God has rescue you from fatal accident

When worshiping God you are not saying the words from the Song but Words from your HEART

WORSHIPING GOD MUST BE OUR LIFESTYLE

We ought to live life that glorify God

Sometimes we find the worshipping environment very hard this is because of what people have

brought from their homes

If brethren will come in the service with worshipping heart the presence of God will be evident

If you have the Spirit of worship even though you are in environment where nobody can see you

You will continue to live in the fear of God

When you are close to source of power you will do great things

"If you don't service the source You will run out of resource "

You cannot go wrong by worshipping God

If worshipping is bringing honor to God so anything that does not give honor to God we are

dishonoring God


THREE STEPS OF WORSHIP


1. It begins in our Mind


When you admire human being because of his Intellect is half of story but the complete part is

there is somebody who gave them the capability, so we ought to Praise the Creator God

"God you are intelligent than anything

"God you are such a wonderful creator

"God you are clever


2. Heart


Heart get signals that God is GREAT

3. BODY

My body will respond

My mouth will sing

My hands will be lifted


This is what happened for people who knows that they are created to Worship God

The Psalmist says "Everyone that has breath must Praise God "

When you know he is worth you cannot stop to Praise God

Job was rich but one day every riches that he has was taken away

" The Lord has given The Lord has taken. ...

This is kind of worship teaches us to worship God in every situation

True worship begin with Knowledge through Your Mind

You need to know God

John 17 ..This is eternal life that they should know you

God is not desperate of our worship he has angels worshipping him day and night

When we are worship God we are not doing him a favor we are doing ourselves a favour

It's in our best interest

Tuesday, February 7, 2017

UNACHOKITAKA USIOGOPE KUKIPANDA, USICHOKIPANDA USITEGEMEE KUKIVUNA

Baada ya sadaka ya Nuhu, MUNGU aliweka order…………

Mwanzo 8:22 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma.

Hii ni kanuni rahisi lakini wengi hawajui kwamba impact yake ni kubwa… tena maandiko yanasema juu ya AINA YA MAVUNO INATEGEMEA AINA YA MBEGU MUNGU WALA USIJITAHIDI KUMDHIHAKI MUNGU MAANA IMEANDIKWA, Wagalatia 6:7 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

Maandiko yanaonyesha kuwa ukipanda mema, tegemea kuvuna mema.. Wagalatia 6:9-10

Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

JE, UNATAKA NINI NA UNAPANDA KITU GANI? Tena maandiko yanaongeza Mathayo 7:12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii. Hii ndiyo wengine wanaita kizungu WHAT GOES AROUND COMES AROUND

2 Wakorintho 9:10-11 Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu; mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.

UZURI NI KWAMBA KILA MARA MUNGU ANAKUPA MBEGU PAMOJA NA MKATE… Kama wewe ni mkulima utaelewa ukivuna mwaka huu, halafu zote ugeuze msosi… cha kupanda wewe umekula… wakati wa mavuno utapiga miayo au kuomba kwa jirani…

Ukisoma 2 Wakorintho 9:10-11 usifikiri hiyo mbegu ni mahindi ila ni sadaka.. ndiyo maana mbeleni utajiri umetajwa pamoja na ukarimu… lakini pia 2 Wakorintho 9:12 Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu

Hizi shukrani Mungu anazipokea kwa sababu kuna watu wanamshukuru kwa sababu wamekirimiwa au wamefanyiwa ukarimu.

Mwaka 2004, nilinunua shati langu la kwanza dukani (kabla ya hapo nilikuwa nachagua mitumba sokoni), nilipofikisha chumbani kwangu nikasikia sauti ndani yangu (Iliyoambatana na amani isiyo ya kawaida) Hili shati ulilolipenda sana ulitoe kwa mtumishi wangu….. kwa kweli sikujua maana ya limbuko wala chochote kinachofanana nacho. Nakumbuka nilikuwa nimeanza kunyofoa pini.. nikarudisha nikampelekea aliyekuwa mwenyekiti wangu wa Fellowship enzi hizo


Tangu 2004 kama nakumbuka sawa sawa sijawahi kununua mashati Zaidi ya 10. MENGI NINALETEWA NA KUPEWA NA WATU

Wakati nimetulia nikajiuliza, hivi kwa nini watu hawaniletei suruali? JIBU NI KWAMBA, SIKUWAHI KUTOA SURUALI KAMA LIMBUKO… Apandacho mtu ndicho atakachovuna

Niko kwenye DIVINE SUPPLY YA MASHATI ….Yule mtumishi alinibariki kwa moyo mkuu…

Nikakumbuka, Paulo aliwaambia Wafilipi 4:19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.

Haya hayakuwa maombi kwa kila mtu…. (Ijapokuwa wakristo wengi wanapenda kuyakiri lakini bado wamepungukiwa) SOMA Wafilipi 4:18 PAULO anasema Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

ALIWABARIKI Wafilipi 4:19 SAWA SAWA NA KILICHOPANDWA KWAKE Wafilipi 4:18

Je, unataka nini? Pesa? Nguo? n.k.... Jifunze kupanda unachokitaka kukivuna…. Mungu akusaidie ufanye kwa Imani na upendo….

PROPER GIVING ENDS STRUGGLES
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

Thursday, February 2, 2017

SIRI 39 ZA KUWA MILIONEA

Na Life Coach Luphurise



1. Tafuta fursa kila kona.

2. Tumia kipaji chako.

3. Kuwa na nidhamu katika fedha - matumizi mazuri ya pesa, nidhamu kwa watu wanaokuzunguka, usijikweze, usibague jamii, heshimu wote waliokaribu yako nk.

4. Kuwa na nidhamu katika afya yako: Afya ndio mtaji sahihi katika biashara yoyote - kuwa na mazoea ya kuangalia afya yako mara kwa mara nk.

5. Usipoteze muda - jali muda kuliko kitu chochote kwani muda ndio kila kitu, muda ni mali.

6. Shiriki kwenye makongamano au semina mbalimbali za ujasiriamali.

7. Kuwa na vyanzo vingi vya kukuletea kipato.

8. Tafuta maarifa kwa mamilionea mbalimbali duniani - soma historia za mamilionea jinsi walivyofanikiwa.

9. Jenga urafiki na taasisi za kifedha - mamilionea wengi hukopa fedha kutoka katika taasisi za kifedha - tembelea taasisi za fedha watakupa ushauri mbalimbali na watakupa mkopo, usisikilize maneno ya watu kuwa taasisi za pesa ni za watu matajiri hiyo sio kweli.

10. Kuwa na shauku, kuwa na fikra za kuwa milionea na wewe utakuwa.

11. Kuwa na imani kwamba utakuwa milionea na itakuwa hivyo.

12. Wekeza ktk miradi au biashara mbalimbali.

13. Wekeza sehemu yenye mahitaji ya bidhaa inayotakiwa kuzalishwa - angalia fursa hapo ulipo na wekeza.

14. Kuwa na bajeti katika mapato na matumizi yako.

15. Chunguza jamii yako wanakosa bidhaa gani kisha dili na bidhaa hiyo nawe utakuwa milionea.

16. Kuwa na wazo (Business idea): mamilionea wengi hutumia mawazo kutoka kwa watu mbalimbali kutengeneza pesa. Wazo ndio cheti cha kuwa milionea anza sasa fanyia kazi wazo lako ili kukuletea fedha.

17. Fanya vitu wewe mwenyewe - acha kufanya vitu kama fulani, usiige mtu, buni vya kwako, mamilionea huwa hawaigi, ukiwa mkweli kwako utakuwa mkweli kwa watu.

18. Kuwa na malengo - kumbuka hakuna maendeleo pasipo na malengo, fahamu hilo.

19. Kuwa na moyo wa ujasiri - usiogope kushindwa jitahidi ktk kupambana na maisha usikubali kubezwa au kuvunjwa moyo. Ukianguka nyanyuka tena, usifikirie kutakuwa na mtu wa kukusaidia zaidi ya kujisaidia mwenyewe.

20. Kuwa karibu na matajiri -usiogope kwani hao ni binadamu kama wewe, jaribu kuwadadisi ili wakupe mbinu mbali za kuwa tajiri hadi milionea. Ukiwa karibu nao unaweza ukapata nafasi ya kazi au kukuunganishia biashara ukaanza kufanya na kufanikiwa.

21. Mtangulize Mungu -mwabudu, msifu, mtolee sadaka, saidia masikini, wajane, wagonjwa, jenga nyumba za ibada. Mungu ndio kila kitu mtegemee yeye.

22. Fanya vitu kitofauti; fanya vitu vigeni, muonekano tofauti ingawa biashara ni ile ile, tumia lugha tofauti, panga bei tofauti, nk. Mfano aina tofauti za simenti, chupa za soda na juisi nk.

23. Acha woga - jaribu biashara yoyote, woga wako ndio umasikini wako, usiogope kukosolewa unapokosolewa ndio unajifunza. Usiogope mikopo, mamilionea wengi hufanya mambo ambayo wewe unayaogopa.

24. Kuwa na mtazamo chanya - usikubali mawazo hasi, marafiki zako wawe na mawazo chanya, usikubali kuvunjika moyo na usikubali mawazo yako yaingiliwe na mtu.

25. Anza kufanyia kazi wazo lako usisubiri mtu.

26. Kuwa na mipaka katika mambo yako - usifanye mambo kwa mkumbo, usiige, buni mambo yako. Mamilionea wengi wanabuni bidhaa zao hawapangiwi na mtu.

27. Dili na watu wenye kipato kidogo na kati katika biashara zako; mamilionea wengi hulenga mahitaji ya watu wa hali ya chini ambao ndio wengi hapa duniani. Baadhi ya mahitaji ya watu wa hali ya chini ni;

(a) Vyakula na vinywaji.
(b) Vifaa vya ujenzi.
(c) Vifaa vya umeme.

28.Kuwa mwaminifu - mamilionea wengi ni waaminifu ktk mali za watu. Wengi walikuwa wakipewa mali wakauze ndio walipe pesa, wanadhaminiwa malighafi za viwandani hadi wanamiliki viwanda vyao. Uaminifu ndio njia ya kukufanya uwe milionea.

29. Pokea ushauri kwa watu hasa kuhusiana na biashara yako - waulize watu kuhusu huduma yako ya biashara wanaionaje na fanyia kazi ushauri wao.

30. Kuwa na plani katika kazi zako kila siku.

31. Kuwa na maono ya jinsi unavyotaka maisha yako yawe.

32. Panua soko la bidhaa zako usitegemee soko la sehemu moja.

33. Ubunifu ni muhimu sana - fanya ubunifu ktk kuuza bidhaa zako ili mauzo yasishuke, kuwa mbunifu ktk wateja wako kwani itakusaidia kugundua wateja wako wanataka nini - kuwa karibu nao, wasikilize, waheshimu nk.

35. Nunua hisa katika mabenki, makampuni mbalimbali: Mamilionea wengi hununua hisa hivyo humiliki mabenki na makampuni mbalimbali.

36. Kuwa milionea kunaanzia kichwani mwako-ukiweka mawazo yako kichwani utakuwa milionea kweli utakuwa sio kusema tu mdomoni. Amini utakuwa milionea na utakuwa kweli.

37. Maneno ya walioshindwa yasikukwamishe safari yako ya kuwa milionea.

38. Ondoa neno haiwezekani wewe kuwa milionea - kila binadamu anaweza kuwa milionea.

39. Mshukuru Mungu kwa hicho alichokupa - kumbuka neema ya Mungu ndio imekufikisha hapo ulipo hivyo toa msaada kwa watu wasiojiweza, yatima, masikini, wajane, wagonjwa, toa sadaka, walemavu nk.

HITIMISHO;
Shujaa mwenzangu, kuwa milionea inawezekana kama mimi na wewe tukifuata njia hizi 39 zinazotumiwa na mamilionea wengi duniani..

Wednesday, February 1, 2017

HUKUUMBIWA MABAYA

Na Shemeji Melayeki

MWANA WA MUNGU, MABAYA HAYAKUTENGENEZWA KWA AJILI YAKO

Uwe makini na ukiri wako mambo yanapoonekana kusambaa na kuunga mkono matangazo ya hali mbaya…

IMEANZA HIVI… You shall also decree a thing, and it shall be established unto you: and the light shall shine upon your ways.

(Job 22:28)

KWA SABABU HIYO BASI…….

When men are cast down, then you shall say, There is lifting up; and he shall save the humble person.

(Job 22:29)

KUWA HUMBLE “MNYENYEKEVU” SIYO KUJITANGAZIA MABAYA NA KUJIONA KWAMBA UMESTAHILI MATESO….. SEMA…… KUNA KUINUKA TENA

OBSERVE WHAT YOU SAY… DO NOT DECLARE THE FALL WHEN PEOPLE ARE FALLING..

Zaburi 91:10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.

Zaburi 91:7-8

Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe. Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.

YESU ALIAMBIWA LAZARO AMEKUFA, LAKINI HAKUWAHI KUSEMA HIVYO HATA KIDOGO…. Yohana 11:11 Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

ILIBIDI WAMLAZIMISHE ASEME UHALISIA…. Yohana 11:14 Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

HATA KWA KIJANA ALIYEKUFA… Luka 8:52-54 Na watu wote walikuwa wakilia na kumwombolezea; akasema, Msilie, hakufa huyu, bali amelala usingizi tu. Wakamcheka sana, maana walijua ya kuwa amekwisha kufa. Akamshika mkono, akapaza sauti, akisema Kijana, inuka.

WHEN MEN ARE CAST DOWN, THEN I SHALL SAY, THERE IS LIFTING UP; AND HE (THE LORD) SHALL SAVE THE ME.
TUONANE JUMAMOSI HII MLIMANI DULUTI, WALETE WENYE MAHITAJI AU UKIWA NA HITAJI LAKO TUPATIE TUKUOMBEE

AMEN

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565