Showing posts with label Maombi. Show all posts
Showing posts with label Maombi. Show all posts

Monday, December 26, 2016

MAOMBI YA FUNGUA MALANGO NA MILANGO - SEHEMU YA 7

Na Mchungaji Florian Katunzi -EAGT City Center

SILAHA NANE ZA KUFUNGUA MILANGO NA MALANGO YALIYOFUNGWA MBELE YAKO

Bwana apewe sifa. Bado naendela na mfululizo wa somo hili ambapo katika makala zilizopita nilikufundisha aina TANO za funguo za kufungua malango na milango. Nilizitaja funguo hizo ambazo ni Neno la Mungu, Toba, Imani, maombi na Nguvu za Roho za roho Mtakatifu. Kimsingi kama utazisoma na kuzielewa basi ni imani yangu ya kuwa utafika mbali kiimani sanjari na kujua ni kwa jinsi gani unatakiwa kupambana na adui shetani.

Leo nitahamia katika kipengele kingine cha silaha nane za kufungua milango na malango, Endelea….

Maombi yetu ya Kufungua Milango na Malango yaliyofungwa inahitaji Uhodari na Uthabiti katika Imani, hivyo lazima silaha hizi zitumike ndipo Milango na Malango yaliyofungwa yatafunguliwa. Kufungua kilichofungwa si kazi rahisi. Maandiko matakatifu yanasema; “Hatimaye mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani; kwa maana kushindana kwetu si juu ya damu na nyama bali ni juu ya falme na mamlaka juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa Roho, kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.” Waefeso  6:10-14
Maisha yetu ya Kristo yapo katika mgongano wa kiroho na shetani na huu mgongano unaitwa VITA VYA IMANI. Ambavyo vinaendelea hadi atakapokuja mara ya pili Yesu Kristo kuvikomesha. Lakini ushindi wa mtu wa Mungu umehakikishwa na Kristo mwenyewe kwa njia ya kifo chake pale msalabani. Alipokufa na kufufuka ametangaza ushindi kwa kila amwaminiye tangu wakati ule hata sasa tunashinda na zaidi ya kushinda. Palipo na neno “KUSHINDA” maana yake pana neno “KUSHINDANA”.
Maisha yetu ya imani ni ya kushindana na kushinda. Wengine kwa kutokujua, adui alipokuja kushindana nao wakaogopa, wakaona Mungu amewaacha na kujiuliza maswali mengi KWANINI BWANA AMEYARUHUSU HAYA? Kumbe maisha ya ukristo halisi ni vita sio lelemama ndiyo maana BWANA anasema tuwe hodari na moyo wa ushujaa. “Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakaye warithisha watu hawa… uwe hodari tuu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote… usiache kwenda mkono wa kuume au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako.” Yoshua 1:6-7
BWANA umtumia mtu hodari na mwenye moyo wa ujasiri sio mtu legelege na dhaifu. Ndiyo maana alimtumia Daudi kumpiga Goliati kwa sababu alikuwa na moyo wa uhodari na ujasiri mwingi. Daudi hakwenda vitani kubahatisha bali alikwenda ksuhindana na kushinda ndivyo ilivyotokea. Maandiko yanasema; “Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang’anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea na kuyagawanya mateka yake.” Luka 11:21-22

Yesu Kristo anahimiza kujifunga silaha zetu na kuyalinda Malango na Milango yetu. Pasipo kujifunga silaha hatuwezi kumshinda yule adui shetani. Lazima uzivae hizi silaha ndipo zitakazofanya Ushinde Falme za giza, Wakuu wa giza hili na kuyashinda Majeshi ya pepo wabaya. Maandiko yanasema; “Maana ingawa tunaenenda katika mwili hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili, maana silaha za vita vyetu si za mwili bali zinauwezo katika Mungu hata kuangusha ngome.” 2Wakorinto 10:3-4

Vita vyetu vya kiroho sharti vipiganwe kwa silaha za rohoni – pasipo kuvaa hizi silaha za kiroho hatuwezi kuziangusha ngome zilizojengwa kinyume na zenye kuhakikisha Malango hayafunguliwi.

SILAHA YA KWANZA
Zipo silaha nane za kiimani zenye nguvu za kufungua malango na milango iliyofungwa katika maisha yetu ya kiroho na kimwili. Silaha hizo ni:-

(i) KATAA
    Imani ni kuwa na hakika katika Mungu na mwenye haki ataishi kwa imani. Maandiko matakatifu yanaonyesha waziwazi ya kuwa msingi wa wokovu ni imani. Yatupasa kuyakataa yale tusiyoyaamini katika imani yetu, mfano wa Musa alivyokataa kuitwa mtoto wa binti Farao, japo kuitwa mtoto wa binti Farao kulikuwa na faida nyingi za kimwili lakini akachagua ufalme wa Mungu na haki yake kuliko ufalme wa Farao ambao mwisho wake ni kutupwa jehanamu ya moto. Hivyo Musa akatumia silaha hii ya kwanza ya KUKATAA matokeo yake BWANA akamtumia kama shujaa na mkombozi wa wana wa Israeli toka utumwani Misri. Maandiko matakatifu yanathibitisha; “Kwa Imani Musa alipozaliwa alifichwa miezi mitatu na wazazi wake kwa sababu waliona kwamba ni mtoto mzuri wala hawakuogopa amri ya mfalme KWA IMANI MUSA ALIPOKUWA MTU MZIMA ALIKATAA KUITWA MWANA WA BINTI FARAO. Akaona afadhali kupata mateso kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo akihesabu kushutumiwa kwake Kristo ni UTAJIRI MKUU kuliko hazina za Misri kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo. Kwa Imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme, maana alistahimili kama amuonaye yeye asiyeonekana kwa Imani alifanya Pasaka, na kule kunyunyiza damu ili yule mwenye kuangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wao” Waebrania 11:23-28

Musa alikataa kuitwa mtoto wa binti Farao, ukawa ndio mlango wa ukombozi wa wana wa Israel kutoka katika milango ya kuzimu ya Farao. Hii ni silaha kubwa sana ambayo lazima tuivae kabla ya mambo yote. Ni lazima kwa Moyo wako wote na Roho yako yote na kwa Akili zako zote Kataa hali uliyonayo katika ulimwengu wa Roho ama katika Mwili. Maandiko matakatifu yanasema; “Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” Mithali 18:20-21
Ukiri katika ulimi una nguvu ya kuangusha malango na milango ya kuzimu hivyo ulimi wa imani ni mti wa uzima. Ni vema kutumia ndimi zetu kujitamkia mema sisi wenyewe, kutamka mema kwa watoto wetu na juu ya mali zetu maana BWANA Mungu alitamka iwe na ikawa. “Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule; Moyo wa mtu mbaya haufai kitu” Mithali 10:20

Dada mmoja pale Morogoro eneo la Forest aliokoka akiwa na miaka kumi na mitano (Miaka 15), siku moja akiwa anatoka shule pale Morogoro mjini, alikutana na mvulana mmoja kumbe ni mjumbe wa shetani (mtu jini) lakini yeye aliona ni mvulana, wakasalimiana, lakini kumbe huyu binti amevamiwa na nguvu za yule jinni kwa sababu alimwambia dada nimekupenda naye akasema asante kama utani lakini ndo ukiri wa kinywa. Baada ya hapo huyu binti alianza kuota ndoto mbaya, anafanya mapenzi; hiyo hali iliendelea kwa muda mrefu akiwa ndani ya wokovu. Huyu binti alipokuwa anakuja kwangu kuniona alikuwa na umri wa miaka thelathini na sita (Miaka 36) akiwa bado hajaolewa, hiyo ilikuwa mwaka 2012, akisema;“Mchungaji nimefunga na kuomba na nimetoa sadaka sana lakini sipati mpenyo, ee Mtu wa Mungu niombee.”

Wakati naanza kumpa ushauri ili nipate kumwombea, nikaitiisha ile nguvu iliyo mfunga kwa jina lenye nguvu la Yesu Kristo. Ndipo nguvu ya pepo jinni dume likapiga kelele likidai huyu binti ni mke wake, limemuoa akiwa na umri wa miaka kumi na mitano kule Morogoro. Nikaipinga ile nguvu ya pepo, nikasema huyu ameokoka, ninyi mnawezaje kukaa ndani yake? Nikahoji tena ni mlango  gani mliotumia kumfunga huyu binti; yule jini akasema waziwazi huyu binti ni mvumilivu na mwaminifu sana kwa huyo Mungu wenu, lakini mimi ninammiliki kwa sababu yeye mwenyewe hajawahi kunikataa na kuitengua ndoa yetu, kwani hujui imeandikwaje katika Warumi? “Kwasababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, Utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.” Warumi 10:9-10

Yule kijana (Jini) alimwambia binti nakupenda naye akakubali lakini hawakuonana tena na ni miaka zaidi ya kumi na sita ndoa ipo katika ulimwengu wa roho. Ukiri una nguvu ya Uzima ama Mauti. Ni lazima ukatae  na utengue kila mkataba na maagano yote ya giza sawasawa na kuamini kwako. Ndiyo maana Musa alikataa kwanza kabla ya wito wake. Tendo la kukataa kuitwa binti Farao ndilo likamfanya Mungu amuite kwa kazi yake.

Wakristo wengi wanataka kufunguliwa Milango na Malango lakini bado hawajakataa kabisa Mizimu ya ukoo, Mizimu ya mababu na mabibi zao, maagano mbalimbali walioungamanishwa kwayo kabla ya wokovu. Usikiri Udhaifu juu yako, juu ya watoto wako, juu ya mume wako, juu ya mke wako, juu ya kazi yako, juu ya ndoa yako wala juu ya maisha yako.
         
 “Neno BWANA lilinijia, kusema, kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; Nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Ndipo niliposema, Aa, Bwana Mungu! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto. LAKINI BWANA akaniambia, USISEME, Mimi ni mtoto maana utakwenda kwa kila nitakayekutuma kwake, nawe UTASEMA KILA NENO NITAKALOKUAMURU. Usiogope kwasababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana” Yeremia 1:4-8

Usiseme kinyume na Neno la Mungu juu yako maana BWANA anakuwazia mema naye ulituma Neno kwako lipate kukuponya na kukufungulia milango na malango ya Baraka na Ustawi.
Angalia Musa pamoja na BWANA kumtumia katika kutenda maajabu na miujiza mingi, lakini Musa alikufa akiwa na  utasi (kigugumizi) kwa sababu hakuukataa udhaifu huo bali aliukubali kuwa sehemu ya maisha yake. Maandiko yanathibitisha;
“Musa akamwambia BWANA, Ee Bwana, mimi si msemaji tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito. Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, BWANA? Basi sasa, enenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha utakalolinena. Akasema, Ee Bwana nakuomba, tuma kwa mkono wake huyo utakayemtuma. HASIRA YA BWANA ikawaka juu ya Musa, akasema, je! Hayuko Haruni, ndugu yako, Mlawi? Najua ya kuwa yeye aweza kusema vizuri. Pamoja na hayo, tazama, anakuja kukulaki, naye atakapokuona, atafurahi moyoni mwake. Nawe utasema naye, na kuyatia maneno kinywani mwake; nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na pamoja na kinywa chake, na kuwafundisheni mtakayofanya. Naye atakuwa msemaji wako kwa watu, hata yeye atakuwa mfano wa kinywa kwako, nawe utakuwa mfano wa Mungu kwake. Nawe utatwaa fimbo hii mkononi mwako, na kwa hiyo utazifanya zile ishara.” Kutoka 4:10-17

Mungu alimkasirikia Musa kwa kitendo cha kukataa Uponyaji wa kinywa chake. Matokeo yake mtumishi wa Mungu Musa mpaka anakufa, alikufa akiwa na utasi (kigugumizi).

Pia tunajifunza kwa YABESI; alikataa maisha ya huzuni, Bwana akageuza huzuni zake kuwa heshima. Kabla ya kupokea hicho unachotaka lazima uvae Silaha hii ya kukataa utaona mlango unafunguka mbele yako.“Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze, na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akasema, Ni kwasababu nalimzaa kwa huzuni. Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akasema, Lau kwamba ungenibarikia kwelikweli, na kunizidishia hozi yangu na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.” 1Nyakati 4:9-11

Pamoja na jina lake kuitwa huzuni, Yabesi alipomjua Mungu alikataa kuitwa huzuni, akakataa maisha ya huzuni. Ndani mwa Maombi haya ya Kufungua Milango na Malango ni lazima tukatae malango yote yaliyotupwa juu yetu au tumezaliwa nayo, maana katika ukiri wa Imani mna nguvu ya kufungua Milango na Malango.

Tunajifunza kwa AYUBU; Pamoja na mateso ya zaidi ya miaka kumi na saba (miaka 17), Kuugua, Kufilisika na Misiba, lakini bado mtumishi huyu wa Mungu alikataa kutamka kinyume cha Imani yake katika Mungu. Katika mambo yote Ayubu hakufanya dhambi wala kumuwazia Mungu kwa upumbavu. “Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na yakuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada  ya ngozi yangu kuharibiwa hivi. Lakini, pasipokua na mwili wangu nitamuona Mungu; Nami nitamuona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine, Mtima wangu unazimia ndani yangu.” Ayubu 19:25-27

Haya maneno yalifungua Mlango na Milango ya Ayubu tena akainuliwa toka kwenye shimo la uharibifu.  Baada ya hayo yote, BWANA aligeuza uteka wa Ayubu.

 “Basi huyo BWANA akaubarikia mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake, naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia efu sita, na jozi za ng’ombe elfu, na punda wake elfu. Tena alikuwa na wana waume saba, binti watatu. Akamwita huyo wa kwanza jina lake Yemima; na wa pili akamwita jina lake Kesia; na wa tatu akamwita jina lake Keren-hapuhu. Katika nchi hiyo yote hawakuwapo wanawake waliokuwa wazuri kama hao wa Ayubu; na baba yao akawapa urithi kati ya ndugu zao wana waume. Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arobaini, nae akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne. Basi Ayubu akafa, mzee sana mwenye kujawa na siku.” Ayubu 42:12-16

Ayubu alikataa  Kukiri udhaifu, Kukiri misiba, Kukiri mateso japo alikua kwenye mateso. Alisema, nalitoka tumboni kwa mama yangu ni uchi nitarudi nikiwa uchi. Maandiko matakatifu yanasema; “Maana mwenye kuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna. Kama vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mja mzito; kadharika huijui kazi ya Mungu, afanyaye mambo yote.” Muhubiri 11:4-5

Kwa imani katika Kristo Yesu yatupasa kukataa yaliyokinyume na imani na tukiri yakuwa anaweza kufanya mambo yote;  Aweza Kufungua Milango na Malango yaliyofungwa. Bwana Yesu Kristo anamtumia mtu aliye tayari kutumika na si vinginevyo. Acha kujiua kwa maneno ya kinywa chako. Maana yeye Kristo Yesu ni mwaminifu. Vaa na ujifunge SILAHA yako itakusaidia. “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.” Waebrania 3:20

Monday, December 19, 2016

MAOMBI YA KUFUNGUA MALANGO NA MILANGO - SEHEMU YA 6

AINA TANO ZA FUNGUO ZA KUFUNGUA MALANGO NA MILANGO

Na Mchungaji Florian Katunzi - EAGT City Center

UFUNGUO WA TANO

NGUVU ZA ROHO MTAKATIFU

Neno “Nguvu” kwa lugha ya Kigiriki ni (dunamis) ina maana ya zaidi ya Nguvu au Uwezo wa kawaida. “Inaashiria hasa nguvu iliyo katika utendaji wa ki-Mungu, hii ni nguvu zaidi ya nguvu.
(Dunamis is not just any power; it is miraculous power or marvelous works. Dunamis can also refer to “Moral power and excellence of soul according to the Greek lexicon). Nguvu ya Roho mtakatifu inajumuisha mamlaka ya kutoa pepo wachafu na upako wa kuponya magonjwa. Roho mtakatifu ndiye ufunguo wa kumshinda adui shetani na kazi zake. Roho mtakatifu ni zaidi ya nguvu ama uweza. Katika maandiko matakatifu, Yesu kristo alionyesha unafsi wa Roho mtakatifu kwa kumwongelea kama nafsi ambapo alisema; “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho  wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.” Yohana 16:13

Kimsimgi tunajifunza kwa Yesu Kristo kabla ya kuanza huduma yake hapa ulimwenguni, alipokwisha kubatizwa na Yohana mbatizaji, wakati anaomba mbingu zilifunguka Roho mtakatifu akashuka juu yake kwa Nguvu tangia hapo maandiko matakatifu yanathibitisha “Ikawa watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua, sauti ikatoka mbinguni wewe ndiye mwanangu mpendwa wangu ninyependezwa nawe.” Luka 3:21-22

Tunajifunza katika maandiko haya yakuwa Nguvu ya Roho mtakatifu haishuki kwa mtu hivihivi mpaka awe anaomba. Lakini wako wakristo wengi wanaotaka kujazwa Roho mtakatifu wakati hawana maombi katika maisha yao. Maombi ufungua mbingu zimfungukie mwombaji. Baada ya Yesu kristo kujazwa Roho mtakatifu, maandiko matakatifu yanashuhudia wazi yakuwa aliongozwa na Roho muda wa siku arobaini katika maombi. “Naye Yesu, hali amejaa Roho mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani.”  Luka 4:1

Pia yunajifunza ili milango na malago ya ukombozi wa mwanadamu yapate kufunguliwa ilibidi Roho mtakatifu ashuke kwa nguvu na uweza mkuu ili kumfunika mwanamwali bikra apate uwezo wa kubeba mimba pasipo kukutana na mwanamume kwa jinsi ya kibinadamu.
“Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, ROHO MTAKATIFU ATAKUJILIA JUU YAKO, na nguvu zake aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu ya hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, mwana wa Mungu.”

Roho mtakatifu akishuka kwetu huja na nguvu zake aliye juu katika Uwezo na nguvu za Roho Mtakatifu, tunavishwa uwezo wa kuangusha ngome zote zilizofunga Malango na Milango yetu ya Baraka za kiroho na kimwili, ndiyo maana Bwana Yesu kristo alisema, Mtapokea nguvu akisha kuwajilia Roho Mtakatifu. Mkristo nguvu yako haimo katika vitu vya upako kama vile; mafuta ya upako, maji ya upako, sabuni za upako, chumvi ya upako, kitambaa cha upako, udongo wa upako, kiganja cha nabii wa upako nambo yafananayo na hayo yanayoibuliwa kila kukicha katika ibada zilizotungwa kwa akili za binadamu. Ndugu mpendwa katika kristo yachunguzeni maandiko vema; mpate kuijua kweli inayoweza kuwawekeni huru mbali na mateso. Tukiwa na msimamo thabiti wa kiimani yatupasa kuliamini Neno la Mungu sio maneno ya watu, watawaijieni kwa mfano wa wanakondoo lakini ndani ni mbwa mwitu wakali. Maagizo ya Yesu Kristo aliye mwanzilishi wa huduma hii iliyokubwa na bora anasema;  Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.” Matendo 1:8
Yesu kristo aliwaambia wanafunzi wake msitoke Yerusalemu bali mwingojee nguvu ya Roho mtakatifu, ambayo kwa hiyo watatenda kazi ya kufungua waliofungwa. Maana pasipo huyo Roho mtakatifu hakuna atakayeweza. Tunaona akina Petro na Yohana baada ya kupokea Nguvu ya Roho mtakatifu waliweza kunena habari za Kristo Yesu na ufalme wake kwa ujasiri na nguvu. Hata wengi walistaajabu walipoona ujasiri wao. “Ndipo Petro akijaa Roho mtakatifu, akawaambia, enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli … wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine katika mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa wakastaajabu wakatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.” Mdo 4:8-13

Kwa hiyo Roho mtakatifu akiwa kwa mtu hujidhihirisha kwa madhihiriho ya ishara, miujiza na maajabu ambayo huwastaajabisha wengi wayaonapo. Roho mtakatifu uhuisha nafsi zetu na miili yetu toka kwenye mafungo ya giza kwa kutufungulia malango na milango. Tunajifunza kwa Lazaro alipougua, akafa, akazikwa kwa muda wa siku nne alikuwamo kaburini lakini kwa nguvu za Roho mtakatifu Yesu alipaza sauti yake akamwita Lazaro toka kwa wafu akawa hai tena. Hata sasa Roho mtakatifu bado anatenda kazi kwa wote waaminio maana tukimwita katika Kristo Yesu ushuka kuokoa na kuponya wengi. Hata kama lipo kaburi limefunga maisha yako ya kiroho na kimwili kwa uweza na nguvu za Roho mtakatifu sharti ufunguliwe. (Through Power of Holy Ghost we Force out evil spirit). Maandiko yanasema katika injili ya Yohana;Basi mtu mmoja alikuwa hawezi, Lazaro wa Bethania, mwenyeji wa mji wa Mariamu na Martha, dada yake. Ndie Mariamu yule aliyempaka Bwana marhamu, akamfuta miguu kwa nywele zake, ambaye Lazaro nduguye alikuwa hawezi. Basi wale waumbu wakatuma ujumbe kwake wakisema, Bwana, yeye umpendaye hawezi. Naye Yesu aliposikia, alisema, Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo. Naye Yesu alim,penda Martha na umbu lake na Lazaro. Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo. Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena. Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzi juzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena? Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu. Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake. Aliyasema hayo; kisha baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yrtu, Lazaro amelala, lakini ninakwenda nipate kumwamsha. Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona. Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi. Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa. Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. Basi Tomaso, aitwaye pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye. Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne. Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadri ya maili mbili hivi, na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao. Basi Martha aliposikia kwamba yesu anakuja, alikwenda kumlaki, na mariamu alikuwa akikaa nyumbani. Basi Martha akamwambia Yesu, bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa. Yesu akamwambia, ndugu yako atafufuka. Martha akamwambia, najua yakuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho. Yesu akamwambia, mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi, naye kila aishie na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo? Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimmwenguni. Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake, akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akasema, Mwalimu yupo anakuita. Naye aliposikia aliondoka upesi, akamwendea. Na Yesu alikuwa hajafika ndani ya kijiji, lakini alikuwa akalipo palepale alipomlaki Martha. Basi wale Wayahudi waliokuwapo na Mariamu nyumbani, wamfariji, walipomwona jinsi alivyoondoka upesi na kutoka, walimfuata, huku wakidhani ya kuwa wanakwenda kaburini ili alie huko. Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake, akasema, Mmemweka wapi? Wakamwambia, Bwana, njoo utazame. Yesu akalia machozi. Basi Wayahudi wakasema, angalieni jinsi alivyompenda. Bali wengine wao wakasema, je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife? Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake. Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, baba, nakushukuru kwakuwa umenisikia. Name nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kukusadiki kwamba ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.” Yohana 11:1-44
Roho mtakatifu huleta uzima badala ya mauti; akatoka nje maana yake, akahuwishwa Lazaro toka kwa wafu japo alikuwa amekufa na ameoza. Ijapokuwa alikuwa ananuka, nguvu ya Roho Mtakatifu iliposhuka juu yake aliyekuwa katika hali ya kufa ikamwinua Lazaro toka kwa wafu akawa hai tena. Ni vema kila mmoja aliyeamini kutambua kuwa Roho mtakatifu ni Ufunguo unaotoa nafsi nyingi katika mafungo ya giza. Kwa nguvu za Roho mtakatifu hata kazi zetu za kimwili zaweza kuhuishwa inaweza kuwa Biashara, Kazi, Elimu vyote vilivyozikwa na kufishwa kuwa hai tena. Kama BWANA alivyonena kwa kinywa cha nabii Ezekieli na kusema; “Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu. Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, BWANA, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema BWANA.” Ezekieli 37:13-14

Kwa nguvu za Roho mtakatifu sharti malango na milango vifunguliwe ndani mwa maombi sio nje ya maombi kwa kuwa tunapomlilia Mungu na kumwita, yeye hushuka na kutufungua mafungo yetu yote. “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini, nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka, makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala, nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.” Mathayo  27:50-57

Nchi ilitetemeka
Wakuu wa anga lazima watetemeke maana Roho Mtakatifu ni nguvu iliyo juu ya yote lazima Wakuu wa nchi washushwe, Wakuu wa giza washushwe, Wakuu wa majini washushwe katika viti vyao kwani Kila goti lazima lipigwe mbele ya Kristo Yesu Mwokozi. 

Miamba ilipasuka
Wako watu wamefungwa nafsi zao katika miamba na majabali mazito, lazima ipasuke ili wote waachiliwe waliofungwa vifungo kwenye miamba kupitia nguvu ya Roho mtakatifu.

Makaburi yakafunuliwa
Kaburi ni kifuniko kibaya sana kinachotesa wengi. Wengi wanafunikwa makaburini kupitia makafara ya tambiko. Kwa nguvu za Roho Mtakatifu miili mingi ya watakatifu waliofungwa na nguvu ya kaburi watainuka.

Kama pazia la hekalu lilivyopasuka, ndivyo kila kizuizi kilichowekwa katika maisha yako ya kiroho na kimwili kitapasuka toka juu mpaka chini. Huu ndio ulikuwa mwisho wa Agano la kale na kuwa mwanzo wa Agano jipya. Katika Kristo Yesu yakale sasa yamepita tazama yamekuwa mapya. Katika ulimwengu wa Roho watu wengi wamefungwa na mapazia ya mabibi na mababu zao, mapazia ya kiganga na kichawi, mapazia ya mizimu na matambiko, lazima tuwafungue watu wa Mungu mapazia hayo ndani mwa maombi haya ya kufungua milango na malango. Yesu akasema mfungueni sanda mwache aende zake. Ikiwa na maana Lazaro alipofufuka alitoka kaburini akiwa amevaa sanda (vazi la wafu) ndiyo maana Kristo Yesu aliagiza avuliwe hilo vazi yaani sanda ndipo aachwe huru aende zake. Hapa tunapata siri nzito ya kiroho ya kuwa wako wakristo wengi waliookolewa toka katika mafungo ya giza lakini hawajahamishwa na kuingizwa katika ufalme wa mwana wa pendo lake. Ni jukumu letu watumishi wa Mungu kufanya maombi na maombezi ya kuwafungua watu baada ya kuamini. Maana KWELI ya Mungu kupitia Neno ndiyo inayomuweka mtu huru mbali na mateso. Ni muhimu sana tukafundisha na kuombea sawasawa na Neno la Mungu. Maana wako wanaodhania ya kuwa baada ya kuokoka vita vyao vimeisha kumbe wokovu ndio mwanzo wa vita vya kiroho na kimwili. Kwa mantiki hiyo ndiyo maana Bwana Yesu akawaambia wanafunzi wake; “Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.”  Marko 14:38

Hata wana wa Israaeli walipokwisha kuokolewa toka utumwani Misri kwa nguvu na uweza mkuu, tunajifunza kwao jinsi walivyokutana na vipingamizi ambavyo viliwafanya wamlilie Mungu na kupigana vita. Walipigana kiroho, wakapigana kimwili. Mfano halisi ni vita vyao na Waamaleki “Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, tuchagulie watu, ukatoke upigane upigane na Waamaleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima. Ikawa, Musa alipoinua mkono wake, Israeli waliposhinda; na aliposhusha mkono wake, Amaleki walishinda. Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa. Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga. BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu. Musa akajenga madhabahu, akaiita jina lake Yehova-nisi; akasema, BWANA ameapa; BWANA atakuwa na vita na Amaleki kizazi baada ya kizazi.”  Kutoka 17:8-16

Wanadamu kwa jinsi ya ubinadamu wao wanaweza kufanya jitihada zao za kiganga na kichawi au za kawaida katika mwili wakakuwekea vipingamizi ili wewe mtu wa Mungu usiinuke. Lakini katika nguvu za Roho mtakatifu tutashinda na zaidi ya kushinda. Angalia mfano, Yesu Kristo walijaribu kumzuia asifufuke toka kaburini kwa kulilinda kaburi kwa kutumia askari wenye silaha na kuweka jiwe kubwa juu ya kaburi. “Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato, wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka. Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamiba, na kuwaambia watu, amefufuka katika wafu, na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza. Pilato akaawaambia, mna askari, nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo. Wakaenda, wakalilinnda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.” Mathayo 27:62-66
Lakini ilipofika saa ya Roho mtakatifu kudhihirisha nguvu zake, walinzi pamoja na silaha zao walikuwa kama wafu. Maandiko yanathibitisha; “Hata sabato ilipokwisha, ikapambazuka siku ya kwanza ya juma, mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi. Na tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la nchi, kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaja akaliviringisha lile jiwe akalikalia. Na sura yake ilikuwa kama umeme na mavazi yake meupe kama theluji. Na kwa kumwogopa, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu. Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi, kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. Hayupo hapa, kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa. Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya nimekwisha waambia.” Mathayo  28:1-7

Roho Mtakatifu ni Nguvu ya Mungu na ni Pumzi ya Mungu yenye kuleta uhai tena. Kama Kristo alihamishwa toka kwa wafu nasi tutahamishwa kiroho na kimwili kwa nguvu za Roho Mtakatifu.

ROHO MTAKATIFU UFUNGUA VIFUNGO VYA UTASA;
Kwa nguvu za Roho Mtakatifu na uweza wake Sara alipokea uwezo wa kuwa na mimba alipokuwa amepita wakati wake. Milango na malango ya utasa yaliyomfunga Sara muda wa miaka wa ishirini na mitano, kwa imani ilifunguliwa.
Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba; alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu.Waebrania 11:11
Hata sasa  kwa uwezo wa nguvu za Roho Mtakatifu, wako wakristo wengi watafunguliwa ndani mwa maombi ya kufungua milango na malango ya UTASA yasiwafunge tena maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu na kusema, hatakuwepo mwenye kuharibu mimba wala aliye tasa katikati yetu.

Roho Mtakatifu akufunike kama kivuli wewe uliyekuwa umefunikwa na roho chafu za mashetani. Roho Mtakatifu na nguvu zake zikufunike kama kivuli, ili Vuli la uchawi na uganga litoke kwako. Kwa nguvu za Roho mtakatifu tumevishwa uweza na Kristo Yesu wa kufungua na kufunga na tutakachokifungua kitafunguliwa katika Mungu aliye hai. Na tutakachokifunga kitafungwa katika Mungu aliye hai. Maana maandiko yanasema;
 “Na ufungua wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.” Isaya 22:22

Nguvu zake Roho mtakatifu zitakapokufunika, Utatenda makuu kwa uwezo wake. Katika yeye Roho Mtakatifu, Wagonjwa wanapokea uponyaji, wanaosumbuliwa na nguvu za mapepo wanawekwa huru mbali na mateso, walioshushwa chini na kudharauliwa wanainuliwa tena. “Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi.” Luka  9:1

Ni lazima tuhamishwe kwa Maombi yenye Imani. Usikubali kuteswa na kugandamizwa, Mtwike Yesu fadhaha zako, mizigo yako, taabu zako, vilio vyako  naye atakuhamisha tu.  Bwana atazitangua ishara zao wachawi na waganga, Maana kwa nguvu za Roho Mtakatifu hakuna uchawi wala uganga kusimama mbele yako tena. BWANA wa majeshi anasema; “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli.” Hesabu 23:23

Ushuhuda wa dada mmoja
Dada mmoja toka pale Kilimanjaro; alinijia akiwa na mateso ya magonjwa yaliyomkumba alipopigwa na upepo njia panda akiwa anakwenda dukani pale kijijini kwao. Baada ya kupigwa na upepo alianguka na kuzimia, alipozinduka alijikuta yuko hospitali akiwa amelazwa. Baada ya miaka miwili kupita tangu apigwe na upepo wa ajabu, ndipo alipokuja kwenye Ibada ya Maombezi ya kufungua Milango na Malango. Ndipo nilipomwombea kwa kuziita nguvu za Roho mtakatifu zenye kung’oa kila aina ya  mapando yaliyopandikizwa kwa watu wa Mungu. Hapa tunaona wachawi wanatumia upepo kumloga na kumwingia dada huyu. BWANA anatuma nguvu ya Roho mtakatifu katika kanisa la kwanza kama uvumi wa upepo. Maandiko yanathibitisha kwamba; “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.” Matendo ya Mitume 2:1-4

Upepo wa kichawi na kiganga uliokuwa unamtesa huyu dada ulimalizwa nguvu zake na kubatilishwa kwa Nguvu za Upepo wa Roho Mtakatifu, nikatengua kila aina ya upepo mchafu ulio mpitia kwa jina la Yesu Kristo.








Monday, December 12, 2016

MAOMBI YA KUFUNGUA MALANGO NA MILANGO - SEHEMU YA 5

Na Mchungaji Florian Katunzi - EAGT City Center

Bwana asifiwe mtu wa Mungu. Bado tunaendelea na mfululizo wa somo hili ambapo katika matoleo yaliyopita nilikufundisha juu ya funguo tatu na nikakwambia faida na namna ya kuzitumia. Na leo tunaendela na ufunguo wa  nne …

Endelea….

UFUNGUO WA NNE

MAOMBI
Maombi:  maana yake ni kusemezana na MUNGU au kutafuta uso wa BWANA; katika hali ya unyenyekevu na kicho “Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu, AONE KAMA YUKO MTU mwenye akili, Amtafutaye Mungu.” Zaburi 13:2
Katika kipengele hiki tunakwenda kujifunza maombi kama ufunguo wa kufungua milango na malango yaliyofungwa.
 “BWANA akamtokea Sulemani usiku, akamwambia, Nimesikia uliyoyaomba, na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu. Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikamuru nzige kula nchi, na nikiwapelekea watu wangu tauni; ilkiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa. Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa ili kwamba jina langu lipate kuwako huko milele; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima. 2Mambo ya Nyakati 7:12-16

Tunajifunza kwa mfalme Sulemani jinsi alivyo jinyenyekeza na kusimama madhabahuni pa BWANA ikiwa ni ishara iliyowazi ya kuwa BWANA ndiye mfalme wa wafalme astahiliye kuabudiwa na kutukuzwa. Hivyo tunajifunza mambo manne yafuatayo:-
(1) “Ikiwa watu wangu watajinyenyekesha” watu wa Mungu lazima watambue ushindi wao dhidi ya malango ya giza unapatikana ndani mwa maombi sio nje ya maombi. Mtu akijinyenyekesha sawasawa na Neno la Mungu hakika atashinda na zaidi ya kushinda. “… Ikawa, Musa alipoinua mkono wake, Israeli walishinda; na aliposhusha mkono wake Amaleki walishinda. Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa Yoshua akaangamiza amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga…” Kutoka 17:8-16
Kwa kuinua mikono yake kwa BWANA Musa anaonyesha wazi jinsi anavyomtumaini na kumwamini Mungu. Waamaleki walipotokea kupigana na Israeli lengo lao ni kuwazuia wasipite walifunga malango na milango kwa njia ya kuanzisha vita. Nguvu ya ushindi ya Israeli ilitegemea kudumu katika Maombi, Imani na utii kwa Mungu. Wakati maombi ya Musa yalipokoma (aliposhusha mikono) mtililiko wa nguvu za Mungu ulikoma kwa watu wa Mungu. Hii ikiwa dhahiri kwamba tunapoomba nguvu ya Mungu hushuka na kinyume chake tusipoomba hakuna nguvu ya Mungu inayoshuka. 

Pia tunajifunza ya kwamba Baraka za Mungu na Ulinzi wa Mungu havishuki hivhivi kwetu mpaka tuvishushe kwa njia ya Maombi. “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea naye atafutaye huona naye abishaye atafunguliwa.” Mathayo 7:7-8

(2) “Na Kuomba” maana yake, watu wa Mungu lazima waombe kwake bila kukoma kwa ajili ya kupata rehema na neema zitokazo kwa Mungu na lazima wamtegemee moja kwa moja na kumwamini yeye aingilie kati. Bwana Yesu Kristo anasema; “…imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa.”
Luka 18:1-
Katika maisha ya imani yako mapito mbalimbali yenye magumu, vita, dhiki, njaa, magonjwa na adha mbalimbali ambazo mtu wa Mungu anakabiliana nazo (changamoto za maisha). Pamoja na changamoto zote hizi hatukati tamaa bali tunatiwa nguvu katika yeye Kristo Yesu. Maandiko matakatifu yanasema “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa n je unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Maana dhiki yetu nyepesi iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.” 2Wakorintho 4:16-18

(3) “Kutafuta uso wa Mungu” Watu wa Mungu ni lazima wamrudie Mungu kwa bidii na kwa moyo wote na kutamani uwepo wake na sio tu kujaribu kukimbia shida ndipo milango yao na malango yao yatakapofunguliwa siku zote za maisha yao. Katika maisha ya huduma ya Yesu Kristo hapa duniani aliutumia ufunguo huu wa kuutafuta uso wa Mungu aliye hai na maombi yake yalisikiwa na uweza wa Mungu ulikuwa ukimtoka na kuponya watu. Alianza kwa maombi (Luka 4:1-14), akadumu katika maombi (Luka 6:12-19)  na kumalizia katika maombi (Luka 22:39-46).  Tofauti sana na maisha ya wakristo walio wengi ambao huomba wakati wa shida na majaribu.  “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu; na ingawa ni mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu ya milele kwa watu wote  wanao mtii; kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki” Waebrania 5:7-10

(4) “Kuziacha njia zao mbaya” Watu wa Mungu ni lazima watubu kwa kweli ya Mungu na kuziacha njia zao mbaya ndipo maombi yao na dua zao zitasikiwa. Bwana Yesu Kristo alisema “… amin, amin, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. Wala mtumwa hakai nyumbani siku zote; mwana hukaa siku zote. Basi mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kwelikweli.” Yohana 8:34-36

Hivyo BWANA anataka kabla ya mambo yote katika maisha yetu tufanye maombi kwa sababu ndiyo ufunguo unaofungua njia. Pasipo kufungua milango na malango kwanza hatuwezi kupenya kiroho na kimwili. Tukisoma maandiko matakatifu yanaonyesha dhahiri hakuna mtu wa Mungu aliye shinda pasipo maombi tangu baba zetu wa imani mpaka manabii walishika sana ufunguo huu wa maombi. “Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukurani, zifanyike kwa ajili yua watu wote; kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na imani, katika utauwa wote na ustahivu. Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu; ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli. Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.” 1Timotheo 2:1-6

Haya ni Maombi yenye kujengwa katika Msingi wa Neno la Mungu,
Imani itokanayo na Neno la Mungu. Mwombaji ni lazima Aombe sawa sawa na Neno la Mungu.

Yesu baada ya kubatizwa kabla ya Huduma alianza kwa Maombi, ambayo yalifanya mbingu zimfungukie. Kwa mantiki hiyo tunajifunza yakuwa Maombi ufungua malango na milango ya mbingu. Tunaona mfano wa Kristo Yesu kama kielelezo; 
“Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua, sauti ikitoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu, nimependezwa nawe.” Luka 3:21-22

Katika maisha yetu ya ukristo tukitaka kufungua milango na malango kwa ajili yetu wenyewe, kwa ajili ya watoto wetu, kwa ajili ya mali zetu sharti tutumie kwa bidii ufunguo huu wa Maombi, sawasawa na ushahidi wa Neno la Mungu lilivyonenwa kwa kinywa cha mtumishi wa Mungu Ezra alipokuwa anaongoza watu wa Mungu toka uahamishoni Babeli kwenda kujenga na kufungua milango na malango ya Yerusalemu. pamoja na kuwa na kilakitu cha kujengea kama vile dhahabu, fedha na vitu vingi vya thamani. Ezra hakuvitegemea hivyo bali aliutegemea mkono wa BWANA ulio hodari ndio maana aliitisha mbiu ya kufunga na kuomba ili kujitafutia njia iliyonyooka itokayo kwa Mungu kabla ya kuanza safari. Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za Mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote. Maana naliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani, kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni kinyume cha wote wamwachao. Basi tukafunga, tukamsihi Mungu wetu kwa ajili ya hayo; naye akatutakabali.” Ezra  8:21-23

Yako mema toka kwa Mungu aliye hai kwa Mwombaji. MBINGU ZIKIFUNGUKA ndani mwa Maombi, Magonjwa yataondoka katika miili ya watu, Maana Maombi hushusha Uweza wa Ki-Mungu wenye nguvu ya kufungua Mafungo yote. Yesu Kristo baada ya Kuomba, Mbingu zilifunguka, kilichotokea ni Udhihirisho wa nguvu za Ki-Mungu zenye kuponya watu.

“Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba. Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu, na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.” Luka  5:16-17

UWEZA WA BWANA ndio unaofungua Malango na Milango kwa Mwombaji. Pasipo Maombi hakuna kitakacho tendeka katika maisha ya mkristo anaye mtegemea Mungu. “Ikwa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake, akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita mitume, Simoni, aliyemwita jina pili, Petro na Andrea nduguye, na Yakobo na Yohana, na Filipo na Bartolomayo, na Mathayo na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Simon aitwaye Zelote, na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote, ndiye aliyekuwa msaliti. Akashuka pamoja nao, akasimama mahali tambarare, pamoja na wanafunzi wake wengi, na makutano makubwa ya watu waliotoka Uyahudi wote na Yerusalemuu, na Pwani ya Tiro na Sidoni, waliokuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao na wale waliosumbuliwa na pepo wachafu waliponywa. Na makutano yote walikuwa wakita kumgusa, kwa sababu uweza ulikuwa ukimtoka ukiwaponya wote.” Luka  6:12-19

Yesu Kristo, anafanya Maombi usiku kucha maana yake anakesha katika Maombi. Matokeo yake ni Udhihirisho wa nguvu na uweza wa ki-Mungu unashuka kwa watu na kuwaponya. Ndani mwa maombi ndimo tunamovishwa Uweza na Nguvu za ki-Mungu aliye hai zenye kuangusha malango na ngome za kuzimu.

Yesu Kristo alikuwa na uwezo katika Kutenda na Kunena, lile Neno alilolisema kwa watu liliambatana na Uwezo na Nguvu. Maana wako watumishi wengi wa Mungu ambao wananena tu lakini neno lao halina nguvu matokeo yake kondoo wa BWANA wanaingia na mizigo yao kwenye ibada na wanatoka na mizigo yao. Kukosa funguo za ufalme wa Mungu ni jambo la hatari kwa mtumishi wa Mungu.

Unapomwendea Mungu sharti ujue unasimamia Neno gani la Mungu, maana Mungu hulituma Neno na ndani yake ndimo ulimo Uzima. Katika maisha yetu ya wokovu tunaweza kukutana na watu wengi wenye wivu na nia ovu, kama hawa makuhani wa kisadukayo kwa wivu wao waliwakamata mitume wakawatupa gerezani lakini kwa mkono wa BWANA wenye nguvu alituma malaika wake akawafungua mafungo yao;  sawasawa na Neno la Mungu. Toka kitabu cha Matendo ya Mitume 5:18-20 Neno linasema; “Wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza, lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.”  

Hapa tunajifunza ya kuwa hatuko peke yetu katika mapito yetu yuko asiyeshindwa. Wajapofunga magereza yao, wajapofunga ndoa zetu, wajapofunga watoto wetu wasiolewe, wajapofunga uchumi wetu yatupasa tumwite Mungu aliye hai naye hakika atatufungua maana kwa msaada wa BWANA tutatenda makuu, na maadui zetu tutawakanyaga kwa nguvu zake. Japo gereza liliendelea kulindwa na walinzi na malango yake na milango yake kufungwa BWANA aliposhuka ndani ya gereza alifanyika mlango wa kutokea.  “Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari, wakisema, gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.” Matendo 5:22-23

Kila kilicho kamatwa kikawekwa ndani ya Gereza la Kiganga na Kichawi, gereza la magonjwa, gereza la nyumba ndogo, gereza la kuzaa kufa kufa na mapooza, gereza la kufeli katika masomo/ kutokufaulu katika mitihani, gereza la uchumi, Lazima VITAFUNGULIWA.

 “Basi watu wote wakulao wataliwa, na adui zako wote watakwenda kufungwa, kila mmoja wao, na hao walio kuteka nyara watatekwa, na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo. Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema BWANA” Yeremia  30:16-17

BWANA akufungulie Mlango na Milango sawa sawa na Kuomba kwako. Mungu analiangalia Neno lake apate kulitimiza, hivyo Omba sawa sawa na Neno utapata jawabu lako. Usiogope, Maana hutapatwa na aibu tena; Tunayo mamlaka ya kugeuza kila hali sawasaw na Neno la Mungu alilonena kwa kinywa cha nabii Isaya na kusema; “Nimeziona njia zake; nami nitamponya, nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia.” Isaya  57:18

Maombi yanafungua Malango na Milango ya Mbingu. Naye BWANA humwongoza daima mtu Mwombaji na Kuishibisha nafsi yake mahali pasipokuwa na maji na kumtia nguvu. Sawasawa na Neno la Mungu lililonenwa na kinywa cha nabii Isaya“Naye BWANA atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.” Isaya  58:11

AYUBU aliomba Ustawi kwa ajili yake, kwa ajili ya watoto wake na mali zake. Akatoa Sadaka za kuinuliwa mbele za Mungu aliye hai akiziambatanisha na Maombi yake. Naye BWANA akamwitikia na kumstawisha katika hayo aliyoyaomba na kuyatolea sadaka.

 “Basi ilikuwa, hapo hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu hutuma kwao akawatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kusongeza sadaka za kuteketezwa kama hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Yumkini kwamba hawa wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu sikuzote. Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Kisha BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure? Wewe hukumzingira kwa UKINGO pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.” Ayubu 1:5-10
Katika fungu hili la Neno la Mungu tunapata kielelezo cha mtu wa imani, mchaji wa Mungu, mwelekevu na aliyejiepusha na uovu. Tunapata taswira ya maisha yake ya kiimani jinsi alivyo yajenga katika msingi wa maombi, hata wakati wa mapito yake BWANA aliendelea kuwa Ukingo kwake. Ndiyo maana alisema “Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, nay a kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu; nami nitamwona mimi nafsi yangu, na macho yangu yatamtazama wala si mwingine…” Ayubu 19:25-27 

Ayubu alifanya maombi maalumu kwa ajili ya watoto wake hakuwaacha wajiendeendee bali alisimama kama kuhani wa familia yake, akawainua mbele za Mungu kwa maombi na sadaka. Nasi katika maisha yetu tumepewa ukuhani usioondoka katika Kristo Yesu. Yatupasa kusimama imara katika maombi kuyafungua malango na milango, kwa ajili yetu sisi, watoto wetu na mali zetu. Kwa kuwa Mungu anamtafuta mtu miongoni mwetu atakayesimama mbele zake mahali palipo bomoka na kujenga boma. “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.” Ezekieli 22:30

Monday, December 5, 2016

MAOMBI YA KUFUNGUA MALANGO NA MILANGO - SEHEMU YA 4

Na Mchungaji Florian Katunzi - EAGT City Center

Mpendwa msomaji bado naendelea na somo hili la maombi ya kufungua malango na milango, ambalo pia utaweza jipatia nakala ya kitabu chako hivi punde.

Wiki jana nilikugusia juu ya ufunguo wa pili wa kufungua milango na malango ambapo nilikufundusha juu ya imani. Bado tunaendelea na aina hizi tano za funguo na leo nitakufundisha juu ya ufunguo wa tatu…..Endelea.

UFUNGUO WA TATU;

TOBA
Toba ni tendo la kiimani la kuungama dhambi na maovu yote yaliyokwisha kufanyika kwa nia ya kujenga upya mahusiano na Mungu aliye hai sawasawa na Neno lake. Maana dhambi ni uasi hivyo atendaye dhambi hujitenga na rehema za Mungu. “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.” Mithali 28:13

Yako malango na milango iliyofungwa kwa watu wa Mungu kwa sababu ya dhambi. Maana wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu. Palipo dhambi na makosa panahitaji toba si vinginevyo. Watu wengi wameruka ufunguo huu matokeo yake wamefunga na kuomba hawakupata majibu kwa kuwa Mungu hadhihakiwi, apandacho mtu ndicho atakacho vuna. “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” Warumi 6:23

Tunajifunza kwa mtumishi wa Mungu Danieli baada ya kuvisoma vitabu vyenye maneno ya Mungu alipata ufahamu utokanao na Neno, akaamini sawasawa na Neno la Mungu jambo la tatu akachukua hatua ya kutubia maovu na dhambi zake na za Taifa lake. Ili kwa njia ya toba BWANA awafungulie milango na malango yaliyokuwa yamefungwa kwa nguvu za miungu ya Babeli. 

 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo; katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, yaani, miaka sabini. Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako; wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi. Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa. Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi. Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi, wala hatukuitii sauti ya BWANA, Mungu wetu, kwa kwenda katika sheria zake, alizoziweka mbele yetu kwa kinywa cha watumishi wake, manabii. Naam, Israeli wote wameihalifu sheria yako, kwa kugeuka upande, wasiisikilize sauti yako; basi kwa hiyo laana imemwagwa juu yetu, na uapo ule ulioandikwa katika sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu; kwa sababu tumemtenda dhambi. Na ye ameyathibitisha maneno yake, aliyoyanena juu yetu, na juu ya waamuziwetu waliotuamua, kwa kumletea mambo maovu makuu; maana chini ya mbingu zote halikutendeka jambo kama hili, lilivyotendeka juu ya Yerusalemu. Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Musa, mabaya haya yote yametupata lakini hata hivyo hatukumwomba BWANA, Mungu wetu, atupe fadhili zake, ili tugeuke na kuyaacha maovu yetu, na kuitambua kweli yake. Basi BWANA ameyavizia mabaya hayo, akatuletea; maana BWANA, Mungu wetu ni mwenye haki katika kazi zake zote azitendazo; na sisi hatukuitii sauti yake. Na sasa, Ee Bwana Mungu wetu, uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kamailivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu. Ee Bwana sawasawa na haki yako yote, nakusihi, hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka. Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana. Ee Mungu wangu, tega sikio lako, ukasikie; fumbua macho yako ukautazame ukiwa wetu, na mji ule ulioitwa kwa jina lako; maana hatukutolei maombi yetu kwa sababu ya haki yetu, lakini kwa sababu ya rehema zako nyingi. Ee Bwana, usikilize, ukatende, usikawie; kwa ajili yako wewe, Ee Mungu wangu; kwa sababu ya mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako. Basi hapo nilipokuwa nikisema, na kuomba, na kuiungama dhambi yangu, na dhambi ya watu wangu Israeli, na kuomba dua yangu mbele za BWANA, Mungu wangu, kwa ajili yam lima mtakatifu wa Mungu wangu; naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni. Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danieli, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu. Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya. Muda wa majuma sabini umuamuriwa juu ya watu wako, na juu ya mji wako mtakatifu, ili kukomesha makosa, na kuishiliza dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, na akuleta haki ya milele, na kutia muhuri maono na unabii, na kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu. Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba, na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu. Na baada ya yale majuma sitini na mawili, masihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika , na hata mmwisho ule vita vitakuwepo; ukiwa umekwisha kukusudiwa. Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.” Danieli  9:1-27

                                                                 
Danieli anaanza kwa Kuungama ili apate kufungua Malango na Milango iliyofungwa.

Unapotubu dhambi na kuziacha ni Mlango wa kuinuliwa, Hata kama umetupwa chini, Maandiko yanasema wazi Mtu mwaminifu atakuwa na Baraka tele na Malango yake yatafunguliwa daima.

“Haya njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theruji, zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa kama sufu. Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi, bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga maana kinywa cha BWANA kimenena haya.”  Isaya  1:18-19

Angalia pia watu wa Ninawi, walivyofungua Malango yao kwa nguvu ya TOBA, maana Walilisikia Neno, Wakaliamini na Kutubu, Naye Yehova akawafungua. Walibatilisha lango la mauti kwa njia ya toba. Hivyo toba ina nguvu katika Mungu hata kuangusha ngome za mauti na kuzimu. Mfalme wa Ninawi aligeuza hasira ya Mungu juu yake na watu wake pale alipoomba rehema za Mungu kwa njia ya toba. Nasi tukiomba rehema kwa ajili yetu na watoto wetu hakika BWANA ni mwingi wa rehema si mwepesi wa hasira, yeye husamehe wote wanao jinyenyekeza kwake.

 “Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu. Naye akapiga mbiu akatangaza habari katika mji wa Ninawi kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng’ombe, wala makundi ya kondoo, wasile wala wasinywe maji bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi na kuiacha hasira yake kali ili msiangamizwe? Mungu akaona matendo yao ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akaghairi neno lile baya ambalo alisema atawatenda, asilitende.” Yona  3:6-10

TOBA ilirejesha upya uhai kwa watu wa Ninawi.

Nasi Kanisa hatuwezi kufunguliwa Malango na Milango pasipo kufanya TOBA ya kweli.

 “Tazama mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.” Isaya 59:1-2

Lazima uiondoe dhambi katikati yako kwa Kutubu na Kuungama mbele za Mungu. Ufunguo huo wa TOBA ndio unaotupa Uwezo na Ujasiri wa kupaingia Patakatifu pake Mungu aliye hai kwa jinsi ya Imani. Ni lazima MKRISTO UZAE MATUNDA YAPASAYO TOBA.

 “Basi zaeni matunda yapasayo toba.” Mathayo 3:8”

Wokovu maana yake ni Kutengwa mbali na dhambi.
Hatuwezi kufunguliwa Milango ya Baraka na Ustawi kama hatutajitenga na maovu.
 “Ndipo Yona akamwomba BWANA Mungu wake, katika tumbo la yule samaki, akasema, Nalimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu, naye akaniitikia; katika tumbo la kuzimu naliomba. Nawe ukaisikia sauti yangu. Maana ulinitupa vilindini, ndani ya moyo wa bahari, gharika ya maji ikanizunguka pande zote, Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu. Nami nikasema nimetupwa mbali na macho yako, lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu. Maji yalinizunguka hata nafsini mwangu, Vilindi vilinizunguka, mwani ulikizinga  kichwa changu, Nalishuka hata pande za chini za milima, Huyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele. Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni, Ee BWANA, Mungu wangu, Roho yangu ilipozimia ndani yangu, nalimkumbuka BWANA; maombi yangu yakakuwasilia katika hekalu lako takatifu. Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo, Hujitenga na rehema zao wenyewe; lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukurani, nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA. BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.” Yona  2:1-10

Nabii Yona alipo Omba toba na Rehema akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, BWANA akamwinua tena, akamfungulia Milango na Malango ya Utumishi. Angalia pia Samsoni pamoja na kumkosea Mungu kwa kiwango kikubwa kwa uzinzi mpaka akatobolewa macho, Lakini alipo Omba TOBA, Jehova Elshadai, Mungu anayetenda zaidi ya tarajio akamwinua tena.

 “Samsoni akaenda Gaza, akaona huko mwanamke kahaba, akaingia kwake. Watu wa Gaza wakaambiwa yakwamba, huyo Samsoni amekuja huku, wakamzingira wakamvizia usiku kucha penye lango la mji, wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, na tungoje mpaka mapambazuko, ndipo tutamwua. Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji na miimo yake miwili, akaing’oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni. Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila. Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja. Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvy zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe. Samsoni akamwambia, wakinifunga kwa kamba mbichi saba ambazo hazija kauka bado, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamletea kamba mbichi saba zisizokauka, naye akamfunga nazo. Na yule mwanamke alikuwa na watu katika chumba cha ndani, wakimwotea. Basi akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakuja. Ndipo akazikata zile kamba kama vile uzi wa pamba ukatwavyo ukiguswa na moto. Basi hiyo asili ya nguvu zake haikujulikana. Delila akamwambia Samsoni, Tazama, umenidhihaki na kuniambia uongo; sasa tafadhali, niambie, wawezwa kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia wakinifunga tu kwa kamba mpya ambazo mtu hakufanya kazi nazo, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Basi Delila akatwaa kamba mpya akamfunga nazo, akamwambia, Wafilisti wanakuji, Samsoni, na wale wenye kuotea walikuwa katika chumba cha ndani. Naye akazikata, akazitupa kutoka mikononi mwake kama uzi. Delila akamwambia Samsoni, hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande.   Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi. Ikawa, kwa vile alivyomsumbua kwa maneno yake kila siku, na kumwudhi, roho yake ikadhikika hata kufa. Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, wembe haukupita juu ya kichwa change kamwe; maana mimi nimekuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. Delila alipoona ya kuwa amemwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akatuma mtu akawaita wakuu wa Wafilisti, akisema, Njoni huku nmara hii tu, maana ameniambia yote aliyo nayo moyoni mwake. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea wakachukua ile fedha mikononi mwao. Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka. Kisha akasema, Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika usingizi wake, akasema, nitakwenda nje kama siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya kuwa BWANA amemwacha. Wafilisti wakamkamata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza. Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake. Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu. Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu. Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili. Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea. Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza. Samsoni akamwita BWANA, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili. Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto. Samsoni akasema; na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu waliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale waliowaua wakati wa uhai wake. Ndipo ndugu zake, na watu wote wa nyumba ya baba yake wakatelemka, wakamtwaa wakamchukua, wakamzika kati ya Sora na Eshtaoli,  katika kiwanja cha kuzikia cha Manoa baba yake. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini.”  Waamuzi  16:1-31

TOBA ilimfanya Samsoni ahesabiwe kuwa miongoni mwa Mashujaa wa Imani maana wokovu aliouleta siku ya kufa kwake ulikomesha ufalme wa Wafilisti kwa kuwa aliwaangamiza kuanzia mdogo mpaka mfalme wao. “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingetosha kuleta habari za Gidioni na Baraka na Samsoni na Yefta na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya samba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga, walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.” Waebrania 11:32-34

Israeli wakafanya dhambi kwa kukosa uaminifu katika kitu kilichowekwa wakfu. Walipokwisha kuangusha mji wa Yeriko na kuta zake na wakauingia mji wa Ai. Akani mwana wa Zabdi mwana wa Zera wa kabila la Yuda, alitwaa baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu, hasira ya BWANA ikawaka juu ya wana wa Israeli kutokana na kutokuwa waaminifu katika maagizo ya Mungu aliye hai.

“Lakini wana wa Israeli walifanya dhambi katika kitu kilichowekwa wakfu; maana Akani, mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila ya Yuda, alitwaa baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu; hasira ya BWANA ikawaka juu ya wana wa Israeli. Kisha Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko mpaka mji wa Ai, ulio karibu na Bethaveni, upande wa mashariki wa Betheli, akawaambia, akisema, pandeni juu mkaipeleleze nchi, basi wakapanda juu wakaupeleleza Ai. Wakarejea kwa Yoshua wakamwambia, wasiende watu wote, ila waende watu kama elfu mbili, tatu, wakupige Ai; usiwataabishe watu wote kwa kuwaendesha huko; maana watu hao ni wachache tu. Basi watu wakaenda huko wapata elfu tatu tu; nao wakakimbia mbele ya watu Ai. Watu wa ai wakawapiga watu kama thelathini na sita; wakawafuatia kutoka mbele ya mlango mpaka Shebarimu, wakawapiga huko kwenye matelemko; mioyo ya watu ikayeyuka, ikawa kama maji. Yoshua akararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA hata jioni, yeye na wazee wa Israeli; wakatia mavumbi vichwani mwao. Yoshua akasema, Ee Bwana MUNGU, kwa nini umewavusha watu hawa mto wa Yordani, ili kututia katika mikono ya Waamori, na kutuangamiza? Laiti tungelikuwa radhi kukaa ng’ambo ya Yordani Ee Bwana, niseme nini baada ya Israeli kuwapa visogo adui zao? Maana Wanaani na wenyeji wote wan chi hii watasikia habari hii, naowatatuzingira, na kulifuta jina letu katika nchi. Nawe utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu? BWANA akamwambia Yoshua, Haya! Inuka, mbona umeanguka kifudifudi hivi? Israeli wamefanya dhambi, naam, wamelivunja agano langu nililowaagiza; naam, wametwaa baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu, tena wameiba, tena wameficha na kuvitia pamoja na vitu vyao wenyewe. Ndiposa wana wa Israeli hawawezi kusimama mbele ya adui zao; wakawapa visogo adui zao, kwa sababu wamelaaniwa; mimi sitakuwa pamoja nanyi tena, msipokiharibu kitu kile mlicho nacho kilichowekwa wakfu. Haya! Inuka, uwatakase watu, ukaseme, Jitakaseni, mwe tayari kesho; maana BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi; kitu kilichowekwa wakfu kiko katikati yako, Ee, Israeli; huwezi kusimama mbele ya adui zako, hata mtakapokiondoa kile mlicho nacho kilichowekwa wakfu. Basi asubuhi mtaletwa karibu nami kabila kwa kabila; kisha itakuwa ya kwamba kabila ile atakayoitwaa BWANA itakaribia jamaa kwa jamaa; na jamaa ile atakayoitwaa BWANA itakaribia nyumba kwa nyumba; na nyumba ile atakayoitwaa BWANA itakaribia mtu kwa mtu. tena itakuwa ya kwamba yeye atakayetwaliwa, naye anacho kitu kile kilichowekwa wakfu, akateketezwa kwa moto, yeye na vitu vyote alivyo navyo; kwa sababu amelivunja agano la BWANA, na kwa sababu ametenda upumbavu katika Israeli. Basi Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, akawasogeza Israeli kabila kwa kabila; kabila ya Yuda ikatwaliwa. Akazisogeza jamaa za Yuda, akitwaa jamaa ya Wazera; akaisogeza jamaa ya Wazera mtu kwa mtu; Zabdi akatwaliwa. Akawasogeza watu wa nyumba yake mmoja mmoja; na Akani, mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila ya Yuda akatwaliwa. Yoshua akamwambia Akani, mwanangu, nakusihi, umtukuze BWANA, Mungu wa Israeli, ukaungame kwake; uniambie sasa ulilolitenda; usinifiche. Akani akamjibu Yoshua, akasema, kweli nimefanya dhambi juu ya BWANA, Mungu wa Israeli, nami nimefanya mambo haya na haya. Nilipoona nyara katika joho nzuri ya Babeli, na shekel mia mbili za fedha, na kabari ya dhahabu, uzani wake shekel hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake. Basi Yoshua akatuma wajumbe wakapiga mbio mpaka hemani; na tazama, vile vitu vilikuwa vimefichwa hemani mwake, na ile fedha chini yake. Wakavitoa kutoka hapo katikati ya hema, wakavileta kwa Yoshua, na kwa wana wa Israeli wote, nao wakaviweka chini mbele za BWANA. Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na lile joho, na ile kabari ya dhahabu, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori. Yoshua akasema, mbona umetufadhaisha hivi? BWANA atakufadhaisha wewe leo. Ndipo Israeli wote wakampiga kwa mawe, kisha wakawateketeza kwa moto, na kuwapiga kwa mawe. Kisha wakakusanya juu yake chungu kubwa yam awe hata leo; naye BWANA akauacha ukali wa hasira yake. Kwa sababu hiyo jina la mahali pale likaitwa, Bonde la Akori hata hivi leo.” Yoshua 7:1-26

Kitu kilichowekwa wakfu maana yake ni cha Mungu.

Mfano:
ZAKA ni sehemu ya kumi ya mali, mazao, mifugo, fedha n.k
BWANA ametoa maagizo na sheria maalumu katika vitu vitakatifu, nayatupasa kupambanua kati ya vitu vitakatifu (wakfu) na vya siku zote. Maandiko matakatifu yanasema; 
“Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.” Kumbukumbu 14:22

Inasisitizwa kuwa makini na kuvitenga vitu vitakatifu kwa Mungu visiwe au kuliwa katika malango ya nyumba zetu maana kufanya kinyume na maagizo ya neno la Mungu ni kukaribisha laana na ukaufu katika kazi zetu za mikono. Maandiko matakatifu yanasema;
“Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka zako, wala divai yako, wala mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng’ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako;” Kumbukumbu 12:17
Jilinde nafsi yako usile zaka siku zote za maisha yako; maana ukila zaka umekula kitu kilichowekwa wakfu ni dhambi. “Kwa kuwa mimi, BWANA,  sina kigeugeu; ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo. Tokea siku za baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, name nitawarudia ninyi, asema BWANA wa majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi kwa namna gani? Je! Mwanadamu atamwambia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa nanmna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu. Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, nakuwamwagieni Baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. Nami kwa ajili yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi. Na mataifa yote watawiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema BWANA wa majeshi.” Malaki 3:6-12

Kutokutoa zaka ni kwenda kinyume na maagizo ya Mungu hivyo mtu uliyeokoka ukila zaka utapigwa mbele ya adui zako;
·        Biashara yako itapigwa.
·        Ndoa yako itapigwa.
·        Elimu ya watoto wako itapigwa.
·        Ustawi wako utapigwa.

“Je mwanadamu utamwibia Mungu? Lakini ninyi; mnaniibia mimi lakini ninyi mwasema tumekuibia kwa namna gani”

Kutokutoa zaka ni kumpora Mungu haki yake katika kazi zako za mikono (sehemu ya kumi ya mapato yako) ni sehemu takatifu kwa Mungu. BWANA anasema;
“Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, NI YA BWANA; NA KAMA MTU AKITAKA kukomboa cho chote cha zaka yake, ATAONGEZA SEHEMU YAKE YA TANO juu yake.” Mambo ya Walawi 27:30-31

Sehemu ya kumi ni takatifu kwa Mungu. Hivyo kutoa zaka sio swala la hiari bali ni lazima kama kulivyo kuokoka ni lazima, nje ya hapo utatupwa Jehanamu. Kumwacha Mungu siyo lazima unywe pombe au ufanye uzinzi lakini kwa tendo la kukosa uaminifu ni dhambi na Kristo anasema TUBUNI NA MREJEE, tafuteni ufalme wa Mungu na haki yake na mengine yote mtazidishiwa. BWANA Yesu Kristo akasema;

“Ole wenu waandishi na mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo IMEWAPASA KUYAFANYA, WALA YALE mengine msiyaache.” Mathayo 23:23
Yesu Kristo aliunga mkono utoaji wa fungu la kumi alipowakemea Mafalisayo waliotilia mkazo fungu la kumi tu huku wakiwa wamesahau mambo ya adili na sheria. Wengine hudhani alipinga utoaji wa fungu la kumi, lakini sivyo, yeye alikuwa anaweka uwiano.

Wako wanaodhani kuwa fungu la kumi sio lazima wakidai ni kwaajili ya waumini wa agano la kale. Wao hudhani fungu la kumi ni agizo la torati. Lakini sivyo. Fungu la kumi liliamriwa kabla ya torati unaweza kusoma “Abramu aliporudi kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni bonde la mfalme. Na Melkizedek mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu sana… Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.” Mwanzo 14:17-20

Kwa kuwa Imani tu pasipo matendo ya haki ya kiimani, ufalme wa Mungu hauwezi kuwa kwako. Ili malango na milango ifunguke sharti kuwa mwaminifu. Maana BWANA ameahidi kwa ajili yetu atamkemea yeye alaye:
·        Asile tena Kazi zetu.
·        Asile tena Ndoa zetu.
·        Asile tena Familia zetu.
Maana Kristo Yesu “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.”
Luka 16:10

Ukishindwa kutoa zaka ya hicho kidogo unachopata, huwezi kupewa kikubwa. BWANA anasema angamiza vyote lakini wewe kwa tamaa unaficha, matokeo yake unaleta mauti katika familia yako badala ya Baraka na ustawi.

BWANA Yesu Kristo anasema “Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu. Luka 16:15
Maana vyote vitapita lakini Neno la Mungu halitapita kamwe katika maisha yetu. Ufalme wa Mungu umo ndani yetu pale tunaposhika Neno lake kwa uaminifu.

AKANI kwa tamaa ya joho tu na shekeli mia mbili za fedha (Akani anasema NALITAMANI MKAVITWAA katika hema yangu na ile fedha. Akani na familia yake waliangamizwa “Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na lile joho, na ile kabari ya dhahabu, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori. Yoshua akasema, Mbona umetufadhaisha hivi? BWANA atakufadhaisha wewe leo. Ndipo Israeli wote wakampiga kwa mawe, kisha wakateketeza kwa moto, na kuwapiga kwa mawe. Kisha wakakusanya juu yake chungu kubwa yam awe hata leo; naye BWANA akauacha ukali wa hasira yake. Kwa sababu hiyo jina la mahali pale likaitwa, Bonde ka Akori, hata hivi leo.” Yoshua 7:24-26

Baada ya TOBA ya wana wa Israeli BWANA akasema “…Inukeni mwende Ai; angalia mimi nimeutia Ai na watu wake; mji wake na nchi yake mikononi mwenu na hawatasimama tena mbele yenu.”

Ushindi wetu wa ki-Mungu hutoka kwa Mungu hivyo afichaye dhambi zake HATAFANIKIWA bali yeye aziungamaye atapata rehema mbele za Mungu.

Ufunguo huu ni wa muhimu sana katika maisha yetu “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mithali 28:13
Kukosa uaminifu huleta kupigwa. Lazima tuchunguze mwenendo wetu na tuyatubie matendo yetu mafu.

“[Ikiwa siku zile Wafilisti walikusanyika ili kupigana na Israeli],  nao Waisraeli wakatoka juu ya Wafilisti kwenda vitani; wakatua karibu na Ebenezeri, nao Wafilisti wakajipanga juu ya Israeli wakapigwa mbele ya Wafilisti; wakauawa watu wa jeshi lao lililokuwa uwandani wapata watu elfu nne. Hata watu walipofika kambini, wazee wa Israeli wakasema, mbona BWANA ametupiga leo mbele ya Wafilisti? Twende tukalilete sanduku la agano la BWANA toka Shilo hata huku, lije kati yetu, na kutuokoa katika mikono ya adui zetu. Basi wakatuma watu kwenda Shilo, nao wakalileta toka huko sanduku la agano la BWANA wa majeshi, akaaye juu ya makerubi; na Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwako huko pamoja na sanduku la agano la Mungu. Na sanduku la agano la BWANA lilipoingia Kambini, Israeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu, hata nchi ikavuma. Nao Wafilisti waliposikia mshindo wa zile kelele, walisema, Maana yake nini mshindo wa kelele hizi kubwa katika kambi ya Waebrania? Wakatambua ya kuwa sanduku la BWANA limefika kambini. Wafilisti wakaogopa, maana walisema, Mungu ameingia kambini. Wakasema, Ole wetu! Kwani halijawa jambo kama hili tangu hapo. Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa na mkono wa miungu hawa walio hodari? Hawa ndio miungu waliowapiga Wamisri kwa mapigo ya kila namna jangwani. Iweni hodari, na kufanya kiume enyi Wafilisti, msije mkawa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa watumwa wenu; fanyeni kiume, mkapigane nao. Wafilisti wakapigana nao, Israeli wakapigwa, wakakimbia kila mtu hemani kwake; wakauawa watu wengi sana; maana katika Israeli walianguka watu thelathini elfu wenye kwenda vitani kwa miguu. Hilo sanduku la Mungu likatwaliwa; na Hofni na Finehasi, wale wana wawili wa Eli, wakauawa. Basi, mtu mmoja wa Benyamini akapiga mbio kutoka mle jeshini akafika Shilo siku ile ile, hali nguo zake zimeraruliwa, na mavumbi kichwani mwake. Alipofika, tazama, Eli alikuwa ameketi kitini pake kando ya njia, akingojea; maana moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Na yule mtu alipoingia mjini, akatoa habari, mji wote ukalia. Naye Eli aliposikia kelele za kile kilio, akasema, maana yake nini kelele za kishindo hiki? Yule mtu akafanya haraka, akaenda, akamwambia Eli. Basi Eli umri wake umepata miaka tisini na minane; na macho yake yamepofuka hata asiweze kuona. Yule mtu akamwambia Eli, Mimi ndimi niliyetoka jeshini, nami leo hivi nimekimbia toka jeshini. Naye akasema, Yalikwendaje, mwanangu? Yeye aliyeleta habari akajibu, akasema, Israeli wamekimbia mbele ya Wafilisti, tena watu wengi sana wameuawa, hata na wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa pia, na sanduku la Mungu limetwaliwa. Ikawa walipotaja sanduku la Mungu, Eli akaanguka kitini pake kwa nyuma, kando ya mlango, shingo yake ikavunjika, akafa; maana alikuwa mzee, tena mzito. Naye alikuwa amewaamua Israeli miaka arobaini. Tena mkwewe, mke wa huyo Finehasi, alikuwa mja-mzito, karibu na kuzaa; basi, aliposikia habari ya kutwaliwa sanduku la Mungu, nay a kwamba mkwewe na mumewe wamekufa, akijiinamisha, akazaa; maana utungu wake ulimfikilia. Hata alipokuwa katika kufa, wale wanawake waliohudhuria karibu naye wakamwambia, Usiogope; kwa maana umezaa mtoto mwanamume. Walakini hakujibu, wala hakumtazama. Akamwita mtoto, Ikabodi, akisema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; kwa sababu sanduku la Mungulilikuwa liketwaliwa, na kwa sababu ya mkwewe na mumewe.” 1Samweli 4:1-21

Israeli walipopigwa hawakuangalia kwa makini sababu ya kupigwa kwao matokeo yake badala ya kufanya toba wakaanza kusaka vitu vya upako viwasaidie katika vita vyao, matokeo yake wakapigwa navyo, wakafa watu wengi sana na sanduku la BWANA Mungu wa majeshi likatekwa.
Ndivyo walivyo wakristo wengi siku za leo, milango na malango yao yanapofungwa badala yakutengeneza njia zao mbele za Mungu, matokeo yake wanasaka vitu vya upako, kama vile maji, mafuta chumvi, vipande vya sabuni matokeo yake wamefarakana na Mungu kwa kufuata ibada ziliotungwa kwa namna ya wanadamu. Maana Mungu ni Roho na wale wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli, kwa mantiki hiyo mtu wa Mungu zingatia kweli ya Mungu ndani ya Neno lake si vinginevyo, mahali pa toba fanya toba. BWANA anasema; “Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu. Basi zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni bali sasa amewaagiza watu wote wa kila mahali watubu.” Matendo17:29-30 
Nasi yatupasa tutengeneze mienendo yetu maana pasipo kuwa na matendo ya haki tukakimbilia kulitaja jina la Kristo Yesu tu, malango na milango havitafunguka.
“Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako? Maana wewe umechukia maonyo, na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, ukashirikiana na wazinzi. Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, na ulimi wako watunga hila. Umekaa na kumsengenya ndugu yako, na mwana wa mama yako umemsingizia. Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. Walakini nitakukemea; nitayapanga hayo mbele ya macho yako.” Zaburi 50:16-21

Dhabihu ya Mungu ni Roho iliyopondeka na kutubu.

“Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.”  Zaburi 51:17

Anania na mkewe Safira walikufa kwa sababu ya kutokuwa waaminifu katika kitu kilichowekwa wakfu mbele za Mungu.

 “Lakini mtu mmoja jina lake Anania pamoja na Safira mkewe, aliuza mali, akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume. Petro akasema, Anania, kwanini shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa.ofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya. Vijana wakamchukua nje, wakamzika. Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia naye hana habari ya hayo yaliyotokea. Petro akamjibu, niambie mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? Akasema, Ndiyo, kwa thamani hiyo. Petro akamwambia imekuaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia miguu yao ya waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe. Mara akaanguka miguuni pake akafa. Wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mume wake.” Matendo  5:1-10

Usituppe neno la Mungu nyuma yako, maana mshahara wa Dhambi ni Mauti.

 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawata urithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi wala watukanaji, wala wanyang’anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii lakini MLIOSHWA, LAKINI MLITAKASWA, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.” 1 Wakorintho  6:9-11

Lazima kuoshwa kwa Damu ya Yesu Kristo kwa njia ya TOBA, hapo ndipo Malango na Milango yako itakapofunguliwa mbele yako.

Lazima Kristo amiliki na kutawala maisha yako, hivyo hatulegei bali tunapiga mbio katika Maombi; ijapokuwa Utu wetu wa nje unachakaa lakini Utu wetu wa ndani sharti ufanywe upya siku kwa siku.
Lazima tuyavue matendo yote maovu na Tumvae Kristo.

 “Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni.” 1Petro 1:17

Kwa hiyo tujifunge viuno vya nia zetu tukitumainia kwa utimilifu ile neema inayoletwa katika ufunuo wake Yesu Kristo. Kama watoto wa kutii tusijifananishe na tamaa zetu za kwanza za ujinga wetu, bali kama yeye aliyetuita alivyo mtakatifu, sisi nasi yatupasa tuwe watakatifu katika mienendo yetu wote. Kwa maana imeandikwa mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.



~~~~~ Usikose sehemy ya 5 wiki ijayo ~~~~~