GET YOUR COPY NOW
Philipian 4:4
Philipian 4:4 "Rejoice in the Lord always. I will say it again: Rejoice!"
Showing posts with label Women. Show all posts
Showing posts with label Women. Show all posts
Saturday, June 10, 2017
Monday, May 19, 2014
Kongomano la Mwanamke wa Thamani lawa Baraka kwa Wanawake wa Moshi
Kongomano la Mwanamke wa Thamani lililofanyika Moshi
mjini, lilimalizika wiki iliyopita likiwaacha wanawake wengi wakiwa wamepata
maarifa ya Neno la Mungu na kufunguliwa.
![]() |
Pastor Neema Shoo mwandaaji wa Kongomano la Mwanamke wa Thamani akifungua rasmi Kongomano hilo
|
Upendo Kilahiro alikuwepo akimsifu na kumwabudu Bwana Yesu
Watu wakisifu na Kuabudu
Kongomano hilo liliandaliwa na Pastor Neema Shoo ambaye
alifungua na utangulizi kutoka Mithali
31:1 alisema mwanamke au mke mwema nani awezaye kumuona nikaonyesha kipo kitu
ndani ya mwanamke ambacho ni cha thamani
Mambo
manne yaliyofichika ndani ya Mwanamke
1. Hekima Ayubu 28:18b naam Kima cha Hekima chapita
marijani, Kama hekima inapita marijani basi na Mithali 31:1 inasema mwanamke
mwema uthamani wake unapita marijani basi hicho cha thamani ndani ya mwanamke
ni Hekima Mithali 14:1 inaonyesha
ukiwa na hekima unajenga nyumba yako bali mpumbavu anaibomoa
2. Ufahamu kilichofichika ndani ya mwanamke ni ufahamu
Ufahamu ni uwezo wa kupambanua jema/baya.
Ufahamu ni Akili Mwanamke mpumbavu asiye na akili hubomoa nyumba kwa
mikono yake ukiwa na Akili utajenga utajua nini nifanye wapi na saa ngapi
kwalugha nyepesi Utajitambua.
![]() |
Pastor Neema akitambulisha Mchungaji wake na Baba na Mama wa kiroho Pastor Dickson Mtalitinya na Mke wake pia alifundisha |
Thursday, May 8, 2014
Kongomano Kubwa la Mwanamke wa Thamani kufanyika mjini Moshi
Wote Mnakaribishwa Katika Kongomano Kubwa La Mwanamke wa Thamani litakalofanyika Moshi mjini.
Mada: Uthamani wa Mwanamke
Uhusiano wa Mungu na Mwanamke
Wahubiri: Pastor Neema Shoo -Host
Pastor Lilian Ndegi
Pastor Dickson Mtalitinya- MTBC Moshi
Lini: Tarehe 10/ 05/2014 siku ya Jumamosi kuanzia saa 4 Asubuhi hadi saa 9 Mchana
Wapi: Ukumbi wa Lutheran Bookshop Stand ya Moshi Mjini
Waimbaji: Upendo Kilahiro
MTBC Praise Team
Nikiongea na mwandaaji wa Kongomano hilo Pastor Neema Shoo, amesema kwamba wanawake watakaohudhuria Kongomano hilo wategee Kufunguliwa na Kupata Maarifa ya Neno la Mungu, hawataondoka kama walivyokuja, Amen!
Kwakweli mwanamke mwenzangu usikose maana vitu Mungu ameweka ndani ya hawa watumishi vitakupeleka kiwango kingine kabisa.
Kwa ninavyomjua Pastor Lilian Ndegi lazima wanawake wa Moshi wapate urejesho.... Haleluyaaaaaa
Thursday, March 13, 2014
Moyo wa Mwanamke 2014: Wanawake wajifunza Umuhimu wa Nguvu ya Maarifa katika maisha yao
Kongomano hilo la siku tano lililofanyika katika kanisa la Living Water Kawe (Makuti) ambako ndio Kanisa la mbeba maono hayo ya Moyo wa Mwanamke Mama Mchungaji Lilian Ndegi liliwafanya wanawake waingie katika viwango vingine vya juu baada ya kujifunza Umuhimu wa Maarifa katika maisha ya Mwanamke.
Mchungaji Lilian Ndegi pamoja na watumishi wengine kutoka sehemu mbalimbali za Afrika walikuwa wanenani katika Kongomano hilo. Baadhi ya Wanenani hao ni mbeba maono mwenyewe Pastor Lilian Ndegi, Esimy Kabeya (Afrika ya Kusini) ,Prophetes Jeanne Kiratu (Mombasa Kenya), Pastor Jael (Nairobi Kenya),Pastor Florence (Gloryland Arusha) na Mchungaji Naomi Mhamba ( Living Water Kawe)
Mungu aliwatumia sana hawa watumishi wake kuleta ujumbe wa Nguvu ya maarifa katika wanawake.
Wanawake walipata nafasi ya kujifunza jinsi ambavyo Mwanamke asipokuwa na maarifa nyumba na maisha yake yataharibika kama ilivyoandikwa katika Hosea 4: 6 "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako"
Mtumishi Esimy Kabeya kutoka Afrika Kusini na yeye alifundisha juu ya Nguvu ya Uelewa katika maisha ya mwanamke.
|
| Picha ya Watumishi/ Wananaji wa Kongomonano hilo la Moyo wa Mwanamke |
| Wanawake wakiwa chini ya Uvuvio wa Roho Mtakatifu |
| Caaaaaake... |
Kata Cake tuleeee..
|
Pastor Lilian Ndegi akilisha wengine Cake
Pia mama Mchungaji Lilian Ndegi alizindua Kitabu chake cha Thamani Maneno ya Kinywa Changu, nakushauri Mwanamke mwenzangu utafute hicho kitabu maana kinachotuponza wanawake ni Maneno :) . Haleluyaaaaaaaaaaaaaaa
Subscribe to:
Posts (Atom)






