Monday, May 19, 2014

Kongomano la Mwanamke wa Thamani lawa Baraka kwa Wanawake wa Moshi


Kongomano la Mwanamke wa Thamani lililofanyika Moshi mjini, lilimalizika wiki iliyopita likiwaacha wanawake wengi wakiwa wamepata maarifa ya Neno la Mungu na kufunguliwa.


Pastor Neema Shoo mwandaaji wa Kongomano la Mwanamke wa Thamani akifungua rasmi Kongomano hilo
Upendo Kilahiro alikuwepo akimsifu na kumwabudu Bwana Yesu

Watu wakisifu na Kuabudu
 
 
Kongomano hilo liliandaliwa na Pastor Neema Shoo ambaye alifungua na utangulizi kutoka  Mithali 31:1 alisema mwanamke au mke mwema nani awezaye kumuona nikaonyesha kipo kitu ndani ya mwanamke ambacho ni cha thamani 

Mambo manne yaliyofichika ndani ya Mwanamke             

1. Hekima Ayubu 28:18b naam Kima cha Hekima chapita marijani, Kama hekima inapita marijani basi na Mithali 31:1 inasema mwanamke mwema uthamani wake unapita marijani basi hicho cha thamani ndani ya mwanamke ni Hekima       Mithali 14:1 inaonyesha ukiwa na hekima unajenga nyumba yako bali mpumbavu anaibomoa                                                                   

2. Ufahamu kilichofichika ndani ya mwanamke ni ufahamu Ufahamu ni uwezo wa kupambanua jema/baya.  Ufahamu ni Akili Mwanamke mpumbavu asiye na akili hubomoa nyumba kwa mikono yake ukiwa na Akili utajenga utajua nini nifanye wapi na saa ngapi kwalugha nyepesi Utajitambua.                                         



Pastor Neema akitambulisha Mchungaji wake na Baba na Mama wa kiroho Pastor Dickson Mtalitinya na Mke wake pia alifundish​a

Wednesday, May 14, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Usioe au Kuolewa kwa msukumo wa Sababu hizi kumi zisizofaa


 
Habari mpendwa wangu, Karibu tena wiki hii nyingine nzuri Mungu ametupa tuzungumze na kushauriana

Leo tunaendelea na somo letu zuri tuliloanza wiki iliyopita la Usioe au Usiolewe kwa Msukumo wa Sababu hizi Kumi zisizofaa

Halleluya nasikia furaha sana kupata kibali cha kuzungumza na wewe siku ya leo.

 

Haya tuendelee na zile sababu tano zingine;

 

6.      Hofu ya kujitegemea

Kuna watu wengine ni tegemezi sana kwa wazazi wao,utegemezi huu unaweza ukawa umesababishwa na malezi wazazi waliwalea au yeye mwenyewe tu ni mvivu.

Utakuta mzazi anamfanyia mtoto kila kitu, atamtafutia chuo, atampeleka chuo, atamtafutia kazi, atamtafutia kiwanja,kupikiwa, kufuliwa etc,yaani mtoto anafanyiwa kila kitu kiasi kwamba yeye mwenyewe hana nafasi ya kuwaza na kufanya vitu peke yake. Sasa hapo pia inategemea na mtoto mwenyewe kama anapenda hiyo hali ndio atabweteka hivyohivyo.

Sasa basi akiona amekaa kwao na umri unaenda sana na wazazi labda wanamshauri apange nyumba na kujitegemea yeye anapata woga kwasababu alizoea kufanyiwa kila kitu ili kukwepa hayo anaamua aolewe au aoe na yeyote anayejitokeza ili tu apate pa kutegemea.

Sasa ndugu yangu kama umemuoa mtu au umeolewa na mtu kwasababu ya huo woga unafikiri kweli utaiweza ndoa, na je huyo uliyemtegemea akashindwa kufikia hayo matarajio yako ya utegemezi si utakimbia, nakuomba leo badili mtazamo usichukua uamuzi wa kuingia kwenye ndoa kama sehemu ya kumtegemea mwenzio akufanyie fanyie, badilika leo ndugu yangu, kuolewa ni kuzuri pale tu panapofanyika vile Mungu anataka na kama nilivyosema mwanzo kuna sababu nzuri tu za kuoa au kuolewa lakini sio hofu ya kujitegemea.

 

7.      Hofu ya kumuumiza mwenzako

 

Inawezekana ulikuwa kwenye mahusiano ya uchumba, lakini muda ulivyoendelea ukaona kwamba huwezi tena kuendelea na huo uhusiano inawezekana kwa sababu nzuri tu

Sasa labda ukiangalia muda ambao mlikaa katika huo uhusiano, mambo mliyoahidiana na kufanya pamoja, labda jinsi jamii inavyowatambua, ukaingiwa na hofu kwamba kwakweli sitaweza kumwambia huyu kaka au dada kwamba siwezi kumuoa au kuolewa naye kwasababu nitamuumiza sana. Matokeo yake unamuoa au unaolewa na mtu ambaye kiukweli hukupenda ila ni kwasababu uliogopa kumuumiza.

Sasa vile vitu vilivyokusababisha utake kufanya uamuzi wa kuachana nae na wewe ukashindwa kwasababu uliogopa kumuumiza, ujue kwenye Ndoa ndio utaviona vizuri sana tena clear, sasa sijui utamlaumu nani unaanza kukosa raha na mwisho kama hutakuwa makini na Mungu kuingilia kati hiyo ndoa inaweza kuvunjika kabisaa.

Au mwingine anaamua kabisa kumwambia mwenzake kwamba kutokana na jinsi huu uhusiano unavyoenda naona tuvunje kabla hatujaenda kupata matatizo katika ndoa, sasa mwingine hasa wakina dada Analia hapo mawiki na mawiki, na mwingine anatishia kujiua, sasa mkaka akiona hivyo anaogopa kwamba mwenzake atapoteza maisha kwasababu yake kwahiyo analazimika kuendelea na mahusiano hadi ndoa.

Je unategemea akimuoa huyo aliyetishia kujiua na bado ulikuwa na sababu za msingi za kuvunja uhusiano unafikiri maisha ya ndoa yatakuwaje? Hebu tafakari

Nakumbuka kuna kijana aliniambiaga namuoa fulani kwasababu unajua nimekaa nae miaka mingi sasa nimempotezea muda japo simpendi lakini namuonea Huruma,hiyo si sawa bora uchumba uvunjike kwa machozi kuliko Ndoa jamani naomba kusisitiza, Haleluya bado unanipenda jamani maana kuna watu wanapenda kung`ang`ania wee kama kakukataa jamani sio mwisho wa Safari na wala hutakufa kwa kumkosa tena baadae ukijam kutafakari  kwanini nilikuwa napoteza muda kwa mtu kama huyu utajicheka sanaaaaa cause they don’t deserve you, Wewe ni mtoto wa Mfalme Bwana, Ambassador of Christ why worries enhee! Aminaaaa!

Tuesday, May 13, 2014

When the Little is Much by Pastor Yared Dondo


Pastor Yared Dondo
Lead Pastor,City Harvest Church
Opening Scripture 1 King 17 : 8-16

 “And the word of the Lord came unto him, saying,

 

9 Arise, get thee to Zarephath, which belongeth to Zidon, and dwell there: behold, I have commanded a widow woman there to sustain thee.

 

10 So he arose and went to Zarephath. And when he came to the gate of the city, behold, the widow woman was there gathering of sticks: and he called to her, and said, Fetch me, I pray thee, a little water in a vessel, that I may drink.

 

11 And as she was going to fetch it, he called to her, and said, Bring me, I pray thee, a morsel of bread in thine hand.

 

12 And she said, As the Lord thy God liveth, I have not a cake, but an handful of meal in a barrel, and a little oil in a cruse: and, behold, I am gathering two sticks, that I may go in and dress it for me and my son, that we may eat it, and die.

 

13 And Elijah said unto her, Fear not; go and do as thou hast said: but make me thereof a little cake first, and bring it unto me, and after make for thee and for thy son.

 

14 For thus saith the Lord God of Israel, The barrel of meal shall not waste, neither shall the cruse of oil fail, until the day that the Lord sendeth rain upon the earth.

 

15 And she went and did according to the saying of Elijah: and she, and he, and her house, did eat many days.

 

16 And the barrel of meal wasted not, neither did the cruse of oil fail, according to the word of the Lord, which he spake by Elijah.”

 

When Elijah request a help from a widow she replied that have nothing but a handful meal in a barrel and little oil in a cruse.

May be there is someone here who think he has little but I want to assure you God has different plan, the little you have can be much in the Kingdom of God

If God want to do something is doesn’t matter what you have, whether it is much or little, educated or not,rich or poor, ministry accepted or rejected, he will fulfill his word regardless of who is standing.

In the above story the country was devastated , there are several things that we can learn from this story;

1.      Poverty

The country was in Poverty.

Sometimes we complained that we are poor but we are not fair because our condition is better compared to others.

Some they don’t have place to live, the whole family( father, mother, grandmother, grandfather and kids) are working as servants to rich people

Elijah was poor even the brook that he depended for water dried. He has nothing.

As he was speaking to God, God told him to go to Zeraphat to meet a widow who will feed him.

In Verse  9 Arise, get thee to Zarephath, which belongeth to Zidon, and dwell there: behold, I have commanded a widow woman there to sustain thee.

In those days widows where poor than other people but still God commanded him to go widow.

The widow has nothing and she has given up with her life, she was waiting to die

She believes in God but has no hope to live again.

To believe in God is not sufficient we have to put into action what we Believe

 

2.      Promise

Thursday, May 8, 2014

Kongomano Kubwa la Mwanamke wa Thamani kufanyika mjini Moshi

 

 
Wote Mnakaribishwa Katika Kongomano Kubwa La Mwanamke wa Thamani litakalofanyika Moshi mjini.
 
Mada:  Uthamani wa Mwanamke
            Uhusiano wa Mungu na Mwanamke
 
Wahubiri: Pastor Neema Shoo -Host
                 Pastor Lilian Ndegi
                 Pastor Dickson Mtalitinya- MTBC Moshi
 
Lini: Tarehe 10/ 05/2014 siku ya Jumamosi kuanzia saa 4 Asubuhi hadi saa 9 Mchana
 
Wapi: Ukumbi wa Lutheran Bookshop Stand ya Moshi Mjini
 
Waimbaji: Upendo Kilahiro
                MTBC Praise Team
 
Nikiongea na mwandaaji wa Kongomano hilo Pastor Neema Shoo, amesema kwamba wanawake watakaohudhuria Kongomano hilo wategee Kufunguliwa na Kupata Maarifa ya Neno la Mungu, hawataondoka kama walivyokuja, Amen!
 
Kwakweli mwanamke mwenzangu usikose maana vitu Mungu ameweka ndani ya hawa watumishi vitakupeleka kiwango kingine kabisa.
Kwa ninavyomjua Pastor Lilian Ndegi lazima wanawake wa Moshi wapate urejesho.... Haleluyaaaaaa
 
 
 

Wednesday, May 7, 2014

Get to Know Dudu a Burundian Gospel Artist




Born on September 27th 1981 in Bujumbura, the main town of a very small country right in the heart of Africa called Burundi, Dudu T. NIYUKURI grew up loving music from his younger age.

He started to sing when he was 10 years old in a church where Daddy was the pastor; from whom he even got his first chords on guitar. Growing more passionate in music, he went, in 1995 to a music youth center to search for more. And that’s when he started to properly get involved into music.

In 1998 Dudu surrendered his life to Christ and started to walk closely with Him. From that relationship with God was born a compassionate heart for all the people who haven’t come to meet the Lord yet and a strong desire to be a witness of the life changing power of the Gospel.

In 2001, after his church leaders recognized the undeniable anointing upon his life, they entrusted him with the charge of the praise and worship department where he couldn’t help but be effective. The evidence came along that in the time when  the country was going through tough civil war, the praise and worship ministry which Dudu was exercising in his church became like an oasis for his desperate fellows and began to build up hope that would actually impact their relationship with God and change their destiny.

As the ministry grew bigger in impact, the need of a professional training in music became obvious because of the limitations he was facing as far as music production was concerned. So God opened a door and he packed his bags and headed for Johannesburg, S.A. in a 2-years period in  the « Academy of Sound engineering » College.

He came out with an operating sound engineering diploma and began to promote Gospel music in Burundi with different artist like Fabrice Nzeyimana, David Nduwimana, Peace-Nadine Ningabire, Fortrant Bigirimana, the GMP team, the Redemption Voice and so on since 2008.

Recently in 2011, he settled to work on his album Jubilee, a collection of Dudu’s hits which is now available.
 
 

Tuesday, May 6, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Usioe au Kuolewa kwa msukumo wa Sababu hizi kumi zisizofaa






Karibu tena katika Makala haya ya Mahusiano na Ndoa, leo Washauri wenu tuko Tayari kabisa kuwaletea somo zuri kabisa la kujiepusha kuingia katika ndoa kwasababu tu ya misukumo isiyofaa

Leo tutaanza kuongea juu ya kuolewa au kuoa kwa msukumo wa sababu tano zisizofaa, sababu tano zingine tutamalizia wiki ijayo, Karibu Sana

 

Tunaposema sababu zisizofaa ina maana kuna sababu Nzuri tu zinazofaa za kwa mtu kuamua kuoa au kuolewa sasa hizo tutaleta baada ya kumaliza hili

 

1.      Kuwa huru na ulinzi au kufuatiliwa na Wazazi

Vijana wengi wameamua kuoa au kuolewa kwasababu labda wazazi wao wamekuwa wanaingilia sana uhuru wao kwa mtazamo wao

Kama tunavyojua maana pia hata sisi tulikuwa vijana, kijana anakuwa anatamani sana kuwa huru kujipangia maisha yake labda afanye hivi na vile au arudi nyumbani usiku au saa ingine asirudi kabisa, sasa mzazi anakuwa mkali atamuuliza maswali kwanini unafanya hivi, kwanini umechelewa, kwanini unachelewa kazini, nakadhalika nakadhalika, au labda ana mahusiano mzazi anayatilia mashaka, sasa kijana mwingine anaona wazazi wanaingilia uhuru wake, Kwahiyo sasa anaamua ili kuondokana na hiyo adha hawa wazazi wananizingua sana ngoja niolewe tuone watanifuatilia huko kwa mume au nyumbani kwangu.

Sasa ni kweli utakuwa umeoa au kuolewa kama huo tu msukumo wa kuoa kwakweli ndugu yangu sio sahihi, kwasababu baada ya muda maswali na ufuatiliaji ule unaweza kuanza tena kwa mwezi wako atataka kujua ratiba zako sasa kwasababu wewe ndicho ulikimbia kwenu huoni kama hapa utakimbia tena, Hebu tafakari kabla hujaamua hiyo ni sababu kweli ya msingi ya wewe kuolewa…

 

2.      Kukimbia matatizo ya nyumbani kwenu

Kila familia ina changamoto zake, wengine uchumi unayumba, nyingine baba mlevi na mkorofi labda, au magomvi yasiyoisha, wengine kusakamwa, wengine ukaa uswahilini sana hupapendi kwakweli, sasa kwa kuona hivyo na labda wanakataa usipange unaamua kuoa au kuolewa ili uwe mbali na kero hizo za nyumbani.

Ina maana wewe huwezi kuvumilia mawimbi ndugu yangu, kama umeshindwa kuvumilia changamoto za wazazi wako hivi huyo unayemuona kwamba anakuambia anakupenda sasahivi je kweli akipata au changamoto utaweza kukaa kweli, maana leo anaweza kukosa kazi, hela ukajikuta uko katika maisha ambayo hata uliyokimbia kwa wazazi wako ni mazuri Zaidi, eenhe tuambie utakimbia tena au? Ndio maana leo tuko hapa kukusaidia na kukushauri lazima utafakari kabla hujaamua ili usije ukaamua kuingia katika ndoa kwasababu ambazo hata hazina tija, zipo sababu zenye tija tutakuja kuzifundisha.

Tafakari ndugu, mdogo na mwanangu, je kuna lingine linalokufanya uamue uchukue huo uamuzi.

 

3.      Unajiona mnyonge na hufai wala hustahili na huna sifa sasa akitokea mtu anasema anakupenda unaamua fasta

Kuna watu labda mazingira waliokulia au ufahamu walionao juu ya maisha umewafanya wawe wanyonge na kujiona hawafai, hawastahili, hawana sifa ya kuoa au kuolewa

Inaweza kuwa labda wazazi waliwalelea katika mazingira ya unyongee sana wakiwaambia kwamba hawafai, wamekuwa wakijidharau sana, wakijishusha sana

Na hii hata wanapokuwa na marafiki wanaendeleza hii tabia , kwahiyo hata mashuleni wanajulikana ni watu wasiofaa, wanyongee sanaa sana, hawana sifa na kibaya wao wenyewe wanajitambulisha hivyo

Labda mwingine anavyojiona na umbile lake anaweza kujidharau au kudharauliwa

Sasa mtu ambaye yuko katika mazingira hayo akatokea tu mtu akawambia anampenda anaweza kuamua haraka sana kwasababu labda hakuwahi kupata mtu anayemdhamini, lakini hiyo tu haitoshi kuwa sababu ya kuoa au kuolewa

Friday, May 2, 2014

City Harvest in Collaboration with Shofar Ministry (SA) Welcomes you to the Worship Revival Night

You are all Welcome to a Worship Revival Night
 

 
 
 
When: Today Friday, 2nd May 2014
 
 
Time: 9:00 p.m to 05:00 a.m
 
 
Location: City Harvest Church, Mabibo Garage,Victoria Filling 2nd Floor
 
 
Entrace: FREE ENTRACE
 
 
 
YOU ARE ALL WELCOME, LETS PRAISE AND WORSHIP OUR LORD!