Thursday, March 13, 2014

Moyo wa Mwanamke 2014: Wanawake wajifunza Umuhimu wa Nguvu ya Maarifa katika maisha yao

 
Kongomano hilo la siku tano lililofanyika katika kanisa la Living Water Kawe (Makuti) ambako ndio Kanisa la mbeba maono hayo ya Moyo wa Mwanamke Mama Mchungaji Lilian Ndegi liliwafanya wanawake waingie katika viwango vingine vya juu baada ya kujifunza Umuhimu wa Maarifa katika maisha ya Mwanamke.
 
 

Mchungaji Lilian Ndegi akifungua kwa maombi, kwakweli Mungu alimtumia sana huyu mama katika njia ya tofauti. Hapo unaweza kuona karama za Roho Mtakatifu zinavyofanya kazi hasa pale unapoamua kumtafuta Mungu kwa bidii.

 
Mchungaji Lilian Ndegi pamoja na watumishi wengine kutoka sehemu mbalimbali za Afrika walikuwa wanenani katika Kongomano hilo. Baadhi ya Wanenani hao ni mbeba maono mwenyewe Pastor Lilian Ndegi, Esimy Kabeya (Afrika ya Kusini) ,Prophetes Jeanne Kiratu (Mombasa Kenya), Pastor Jael (Nairobi Kenya),Pastor Florence (Gloryland Arusha) na Mchungaji Naomi Mhamba ( Living Water Kawe)
Mungu aliwatumia sana hawa watumishi wake kuleta ujumbe wa Nguvu ya maarifa katika wanawake.
Wanawake walipata nafasi ya kujifunza jinsi ambavyo Mwanamke asipokuwa na maarifa nyumba na maisha yake yataharibika kama ilivyoandikwa katika Hosea 4: 6 "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako"

 
Mchungaji Naomi Mhamba(Prof.) alifundisha juu ya Uponyaji wa Uzao wa Mwanamke Vs Nguvu ya maarifa alifundisha vizuri sana akitoa mifano halisi ya kulea kizazi hiki na maarifa yamekuwa mengi ambapo Ibilisi analeta maarifa mengi katika jamii na yanavizia watoto na jinsi ya kukabiliana na hila hizo za Ibilisi kwa kumlea mtoto kama Mungu alivyokusudia


Wamama wakisikiliza kwa makini kwakweli ungeangalia nyuso zao kila mmoja aliweza kupokea kitu kipya cha kumsadia yeye, maisha na familia yake. Na kama tunavyojua ukimfundisha Mwanamke umefundisha jamii.



Mtumishi Esimy Kabeya kutoka Afrika Kusini na yeye alifundisha juu ya Nguvu ya Uelewa katika maisha ya mwanamke.


Picha ya Watumishi/ Wananaji wa Kongomonano hilo la Moyo wa Mwanamke



Wanawake wakiwa chini ya Uvuvio wa Roho Mtakatifu


 
Siyo kama mama alifungisha Harusi siku hiyo jamani ni style ya kufundisha ya mama huyu ambayo inamfanya mtu unaelewa kwa kiwango cha juu, hapa anaonyesha mfano wa wanawake wawili tofauti mwenye Hekima na asiye na Hekima. Kwa nje anaweza kuonekana mdada mrembo lakini kumbe ndani hana hekima na mwingine anaweza akaonekana kwa nje labda havutii sana lakini ndani akawa na hekima
 
 

 
Pastor Lilian Ndegi akifundisha kwa kutumia mfano wa wacheza Karata waliokuwa wanacheza kwa kutumia Almasi ,ikiwa na maana kwamba usipokuwa na maarifa utafanya kitu cha thamani kikose uthamani wake na ni rahisi kukupoteza
 
Prophetess Jeanne Kiratu kutoka Mombasa Kenya alifundisha juu ya Jinsi Mungu anavyokwenda kufanya Turn Around (Mageuzi) katika maisha ya mwanamke pale atakapotumia Maarifa yaliyoko katika Neno la Mungu katika maisha yake
 
Pastor Jael kutoka Nairobi na yeye alifundisha Nguvu ya Hekima katika maisha ya Mwanamke, alifundisha kwa njia ya shuhuda za wanawake mbalimbali ambao zamani hawakuwa na hekima katika maisha yao lakini walipopata maarifa wakaishika Hekima na maisha yao na familia yakabadilika hadi watu wakashangaa
 
 

 

Pastor Florence kutoka Gloryland Arusha alifundisha juu ya Nguvu saba za Maarifa, akafafanua kwamba wengi wanaomba tu bila kuwa na maarifa lakini mara nyingine maombi bila maarifa ni kama kelele mbele za Bwana. Mchunangaji huyu alifanya wanawake wacheke sana kwa style yake ya kufundisha kwa umaridadi. Alifundisha wanawake umuhimu wa kuishi kama Malkia na Wafalme.


Neema Baraka na yeye alikuwepo kumwimbia na kumtukuza Bwana, wanawake walipata nafasi ya kumsifu na kumtukuza Bwana Yesu.




Kusifu na Kuabudu



 

Upendo Nnkone alikuwepo katika huduma yake ya kumsifu na kumwabudu Bwana Yesu





Ritha Chuwalo akimchezea Bwana Yesu, twendeeeee


Chezea Bwana...



Wow Wow kulikuwa na mambo mengine mazuri pia katika Kongomano hilo ambapo siku ya Tarehe sita ilikuwa ni Birthday ya mama Pastor Lilian Ndegi ambapo wamama walikuwa wameandaa Cake na wanawake waliweza kushiriki kwa pamoja. Happy Belated Birthday Mchungaji..


Caaaaaake...




 
Kata Cake tuleeee..


Pastor Lilian Ndegi akilisha wengine Cake



Pia mama Mchungaji Lilian Ndegi alizindua Kitabu chake cha Thamani Maneno ya Kinywa Changu, nakushauri Mwanamke mwenzangu utafute hicho kitabu maana kinachotuponza wanawake ni Maneno :) . Haleluyaaaaaaaaaaaaaaa




 

1 comment:

  1. Ingekuwa vema kuweka hayo masomo na sio mkuweka tu picha. kwani tunajifunza mengi kupitia hii blog. barikiwa daima

    ReplyDelete