Saturday, November 22, 2014

George (bonge) wa Kwaya ya Lulu Mtoni afariki dunia

Mwimbaji wa nyimbo za Injili George au bonge wa Kwaya ya Lulu Mtoni amefariki dunia Jana katika hospital ya Muhimbili

Mipango ya mazishi inafayikia nyumbani kwake Tabata Bima

Kesho mwili wa marehemu utasafirishwa kesho kwenda nyumbani kwao Tukuyu, Mbeya

Wakati wa uhai wake alitumia maisha yake kumtukuza na kumuhubiri Yesu kwa njia ya uimbaji

Mojawapo ya nyimbo alizoimba ni "around the corner" na "lulu"

George aliwashangaza wengi pamoja na kuwa na mwili mkubwa alikuwa mwepesi kumwimbia Yesu akiruka ruka kwa Furaha

Kwa maelezo zaidi jinsi ya kufika nyumbani kwa marehemu piga namba ya mwenyekiti 0754 464102

Rejoice and Rejoice imawapa pole wote waliofikwa na msiba huh

Tutengeneze na Mungu maana hatujui siku wala Saa, Amen

Tuesday, November 18, 2014

Myles Munroe's Children Weep as Thousands Show Up for First Sunday Service Since Crash; Church Recalls Last Sermon


Myles Munroe and his wife, Ruth, (inset), and Myles Munroe Jr. and his sister, Charissa, (R).
Although prominent evangelical pastor Myles Munroe told the world that he had prepared his children to live without him should he die, his daughter, Charissa, and son, Myles Munroe Jr., couldn't hold back their tears as they faced his former congregation for the first Sunday since his untimely death with their mother, Ruth, and seven others in a fiery jet crash two Sundays ago.

Kevin Harris, spokesperson for the Bahamas Faith Ministries, which the renowned evangelical pastor and motivational speaker led before his death, told The Christian Post in an interview Monday that attendance at the church exploded Sunday with supporters who had been rocked by the tragedy.

"We had an overflow. We had to bring in [a] tremendous amount of seating. Thousands of people turned up," said Harris.

One 20-year member of Munroe's church, who asked not to be identified, told CP that the mood inside the church Sunday was "somber."

"It was a sad mood," explained the member. "Everybody was saddened by what happened. There was tears and everything."

A video posted to Facebook from the service shows a few minutes of Munroe's son addressing the church during that service before blacking out to a voice-only recording.

"I was gonna prepare a speech, but as I was getting ready this morning I just knew that I was coming to talk to family," Myles said, struggling with tears. "I figured I would just speak to family. It's been the hardest week for my sister and I and my family, and everyone else that has been affected; and it's because of family why we are able to stand here today," he continued.

"My dad always spoke about his belief in people, nothing else mattered but the people, regardless of how long he spoke or he travelled, he always made time for people. That's just the kind of person that he was. And we sometimes take that for granted just because people are here every day and you just don't think certain people won't be here tomorrow," he added, while urging the congregants not to take each other for granted.

Wednesday, November 12, 2014

JIANDAE KURUDI NYUMBANI Sehemu ya Kwanza na Mwalimu Samwel Mkumbo


Karibu katika mafundisho haya yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo

Mwalimu Samwel Mkumbo
Utangulizi:
 
Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao. (Waebrania 13:14)

Mtu huweza kutoka asubuhi kwenda katika shughuli mbalimbali wengine huenda mashambani wengine maofisini na wengine kwenye shughuli za aina nyingine, biashara lakini ifikapo jioni au usiku HURUDI NYUMBANI, inawezekana kama ni watoto au ni wazazi waliachana asubuhi wengine wakienda kazini wengine shuleni lakini jioni WATARUDI NYUMBANI.

Mtu anapotoka mji mmoja na kwenda mji mwingine kwa ajili ya kuishi huko aidha kwa sababu za kikazi au hata biashara, akafanikiwa na akaanzisha maisha huko akawa na familia huko na akajenga na makazi yake huko, lakini siku akifariki mara nyingi wengi HURUDISHWA kuzikwa NYUMBANI.

Katika kitabu hiki ambacho kitakusaidia kukueleza mambo kadhaa juu ya wokovu ulioupokea katika maisha yako, utajifunza mambo mengi na ni maombi yetu ya kwamba kitabu hiki kiwe msaada mkubwa sana kwako.

Mambo utakayojifunza:

Sura ya Kwanza: katika sura ya kwanza utajifunza namna ambavyo dunia hii si mahali pa kupategemea na ya kwamba si mahali pa kudumu, na pia utajua kama dunia si mahali pa kupategemea je hatma yako ni nini, na ni nini mwisho wa maisha yako.

Sura ya Pili: itakusaidia kujua ni nini unachotakiwa kufanya kama dunia si mahali pa kudumu ili uweze kufika unakotakiwa kwenda, utajifunza kuwa unahitaji sana maandalizi ya kuelekea mahali unapotakiwa kwenda.

Sura ya Tatu: mambo ya msingi ikiwa ni mwendelezo wa sura ya pili ni kujua ya kwamba unakokwenda hutakiwi kwenda mikono mitupu, kuna mambo unayotakiwa kuyabeba, hivyo kwanza utajikuta kuna maswali unatakiwa kuyajibu ya ulichobeba kwanza na kisha utajua ni nini unatakiwa kubeba.

Sura ya Nne: sura hii itakuelekeza mambo ambayo ni muhimu uyafahamu katika safari hii, mambo yatakayotokea njiani, mambo ambayo yanapotokea usishangae, lakini pia utapata tumaini kwa kujua ya kwamba hauko peke yako.

Nimalizie utangulizi huu kwa kusema JIANDAE KURUDI NYUMBANI.

Sura ya kwanza.

DUNIANI SIO KWETU

Nataka niweke wazo hili kwanza kwako wakati unaendelea kusoma sehemu hii, ni kwamba DUNIANI SIYO KWETU, ndio! Namaanisha hata wewe hapo ulipo, Duniani siyo Kwako, haijalishi umeweka nini duniani, au unaipendaje dunia, au dunia inakupendaje. Si kitu unawapendaje watu wa dunia na vitu vya dunia lakini nataka ujue, na siyo utani kabisa kwamba hapa DUNIANI SIYO KWETU.

Waebrania 13:13-14 imeandikwa hivi;

13 Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutumu lake. 14 Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

Monday, November 10, 2014

Dr. Myles Munroe, wife Ruth, among 9 killed in Bahamas plane crash


Dr Myles Munroe
This morning I received a sad message from a friend that our Life Coach and Role Model, Dr. Myles Munroe, the leader of Bahamas Faith Ministries, was killed Sunday when the plane he was in hit a construction crane, exploded and crashed in the Bahamas.

Munroe's wife, Ruth, was also among the 9 victims of the crash in Grand Bahama, according to the Bahamas Tribune.

Group picture takes before departure
The small plane  crashed after hitting the crane in a shipyard on approach to the Grand Bahama International Airport, according to officials there.
In addition to founding BFMI, the internationally known Munroe was also president of Myles Munroe International (MMI).  The BFMI website describes Munroe was a "lecturer, teacher, life coach, government consultant, and leadership mentor."



Dr Myles Munroe and his Wife Ruth
The plane crashed as people were gathering in Grand Bahama for the Global Leadership Forum -- an event organized by Munroe.
Last month Dr Myles Munroe visited Tanzania, where he spoke to Student Leaders, Business Leaders, Religious Leaders, politicians and Government Officials.
Rejoice and Rejoice blog, were are so touched with his death but as it is in written in Romans 8:28 "And we know that all things work together for good to those who love God, to those who are the called according to His purpose."

Friday, November 7, 2014

Exciting Business Opportunity from America now in Tanzania

Its is my pleasure to Welcome you all to an exciting Business Opportunity from America to our country Tanzania.

Trevo opens its next international location in Dar es Salaam, Tanzania ,Trevo President & CEO Mark Steven with Country Directors Mike Ajao and David Kagoro will be there to celebrate the upcoming opening date for new center.

Through this business people will get  financial and time freedom

If you have any question please dont hesitate to call the below Numbers

Wednesday, October 15, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Do you want your Spouse to change



Wengi wanataka kuona madadiliko kwa wenzi wao lakini hawako tayari kubadilika kwanza, hebu mpendwa wangu chukua hatua ya kubadilika leo.
Utakapobadilika na mwenzi wako utashangaa anabadilika

Muombe Mungu akuonyeshe ni eneo gani unatakiwa kubadilika na ukabadilike leo
Hata kama unaona hiyo tabia ni ngumu, mkabidhi Mungu yeye anaweza yote hakuna jambo gumu asiloliweza.


Mungu atusaidie na akakusaidie pia, Amen

Thursday, October 9, 2014

City Harvest welcomes you to Couples Seminar

You are all invited to Couples Seminar which will be held at City Harvest






Venue: Victoria Service Station Building, 2nd Floor along Mandela Road

Time: 9:30 to 5pm

Contribution:  5,000/= per person for bites and logistics

 

 

Successful Couples will make a Successful Family which will make Successful Society hence having Successful Nation

 

You are Warmly Welcome

Thursday, October 2, 2014

Welcome to End of Month Fellowship with Dar es Salaam Workers Christian Fellowships (DWCFs)





Here comes another colourful Thursday, once in a month, where all Dar es Salaam Workers Christian Fellowships (DWCFs) gether together under one roof in the wings of the Al-mighty.

 

It is JB Belmonte Hotel again with Pastor Mastai again, and praise and worship team from FPCT at 17:00 hours onwards!

 

The ivitation is free to anyone, and there is no entry fee or qualification. Come meet Jesus!

 

For more info see attached flyer.

 

You are warmly welcome J

Friday, September 5, 2014

Semina ya Siku tatu (3) ya Kufunguliwa kwa Mwanamke mjini Moshi na Pastor Neema Shoo


The Woman of Value iliyo chini ya Mchungaji Neema Shoo ( MTBC Moshi) inakuletea Semina ya Siku tatu ya Wanawake, Mabinti na Wamama kwa siku 3.




Semina itafanyika kuanzia Ijumaa tarehe 10 saa 9 Mchana hadi 12 Jioni
                                           Jumamosi tarehe 11 saa 4 asubuhi hadi saa 10 Jioni
                                           Jumapili tarehe 12 saa 10 jioni hadi 12 jioni

Semina Itafanyika Katika Ukumbi wa Hindu Mandal Moshi Stand

Katika Semina hiyo watumishi mbalimbali watahudumu Pastor Neema Shoo, Bishop Mary Lutumba-DSM, Prophet Essien Godwin SImon-Ghana na Pastor Dickson Mtalitinya- Moshi.

Upendo Kilahiro and MTBC Moshi watatuongoza katika sifa na kuabudu

Wagonjwa na wenye shida mbalimbali wataombewa

Wanawake wa Kilimanjaro , Arusha na kote Tanzania hii Semina siyo ya kukosa mwambie na mwingine

Tuesday, August 26, 2014

Kuna Uhusiano Mkubwa kati ya Usalama na Ubora wa Nafsi yako na Uhai wa Kanisa -III na Mwalimu Samwel Mkumbo

 

 Mwalimu Samuel Mkumbo pichani
Karibu atika mifululizo yote ya somo hili kutoka mwanzo mpaka sasa imekuwa ni suala la kuangalia ni kwa jinsi gani nafsi zetu zinahusika sana katika Uhai wa Kanisa. Sehemu ya mwisho nitasema nawe kwa kifupi sana kuhusu Uhusiano wa nafsi ya Kanisa.

Karibu tujifunze pamoja…..

Luka 12:15 inasema hivi;

Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.

Ni heri kila mmoja akahakikisha ya kwamba Nafsi yake iko na furaha kila wakati, kwa ajili ya uhai wa kanisa lako, lakini pia kwa ajili ya uhai wa nyumba yako kama msingi wa kanisa, kwa ajili ya ofisi yako, kwa ajili ya ukoo wako.

Lakini pia ni vema kila mmoja akahakikisha anafanya bidii kumfurahisha mwingine na kuifanya nafsi ya mwingine isiwe na jeraha hata moja, kuifanya nafsi ya mwingine isitende dhambi, kila mmoja acheze karibu na mwenzake, kama kucheza basi tucheze peke yetu, hakikisha unamlinda mwenzake asipate shida wala asipotee.

1 Wakorintho 8:12 tunasoma hivi;

Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo

Kuna Uhusiano Mkubwa kati ya Usalama na

Ubora wa Nafsi yako na Uhai wa Kanisa

Sasa labda tutazame kwa nafasi nyingine uhusiano wa Nafsi yako ikiwa na Usalama na ubora wa nafsi yako na Uhai wa Kanisa ikiwa ni la nyumbani au ni mahali unapoabudu au ofisini kwako au hata shuleni kwako unakosoma.

Labda niweke jambo hili la msingi, tunapozungumzia kanisa ni lazima tukajua ya kwamba si suala la dhehebu moja tu au suala la watu wanaosali kwa pamoja lakini suala la Kanisa ni jambo linalohusu watu wote waliookoka na wanaomkubali BWANA YESU kuwa ni mwokozi wa maisha yao na Mfalme wa Ulimwengu wote.

Sasa kuna shida ambayo ni muhimu tukaishughulikia vizuri kidogo ili tusipate shida tunapoangalia utekelezaji wa Somo hili, na jambo lenyewe ni lazima akili zetu na fahamu zetu zifunguke tukajua mambo kadhaa ili tuone Umuhimu wa kuona Nafsi ya kila mmoja inakuwa salama na bora ili Kanisa liweze kuwa Hai.

1 Wakorintho 3:16-17 tunasoma hivi;

Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.

Sasa kuna jambo la msingi hapo natamani tulitazame kwa makini sana sana, maana kama tusipolitazama kwa makini tunaweza tusielewe vizuri, na hilo jambo linatuonesha Uhusiano uliopo kati ya Usalama na Ubora wa Nafsi yako inavyohusiana na Uhai wa Kanisa la Tanzania, Kanisa la Ulimwengu mzima lakini pia kuanzia na Kanisa la Nyumbani kwako na mahali unapoabudu.

Basi tuutazame huo mstari kwa makini sana sana, kuna maneno kadhaa ya huo mstari natamani tuyatazame kwa makini …..Hamjui ya kuwa NINYI mmekuwa hekalu la Mungu….. na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani YENU?....... Kama MTU akiliharibu hekalu la Mungu,… Mungu atamharibu MTU huyo….. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo NINYI.

Maneno niliyoyaweka kwa herufi kubwa yana maana kubwa sana, Paulo kwa uwezo wa Roho Mtakatifu anawaandikia Wakorintho akitaka kuwaonesha ni jinsi gani Uhusiano wa Kanisa unavyotengenezwa na unavyotegemea mtu mmoja mmoja. Anapozungumzia Hekalu la Mungu anasema ni NINYI au ndilo SISI kama tukijiweka kwenye nafasi ya Wakorintho na ambayo ni nafasi muhimu lazima tujiweke hapo ili hiyo nafasi tuichukue kwa Umuhimu mkubwa sana.

Jambo amabalo ni la kulitazama kwa makini kwenye mistari hiyo ni kwamba inapozungumziwa kanisa basi tunatazama kama Muunganiko wa watu,. Maana HEKALU LA MUNGU (moja) linajengwa na NINYI (wengi), lakini pia inawezekana hilo Hekalu la Mungu ambalo ni watu wengi likaharibiwa na MTU yaani mmoja. Sasa basi kuna jambo la kulitazama tena hapo kwa makini Zaidi, kwamba kama Hekalu la Mungu linalojengwa na SISI linaweza kuharibu na YULE au WEWE basi pia linaweza kujengwa na WEWE- Nitalielezea hilo baadae kwa undani.

Wednesday, August 6, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Usifikiri utaweza kubadilisha tabia ya mwenzi wako baada ya kuolewa naye au Kumuoa

 

Bwana Asifiwe watu wazuri wa Mungu, namshukuru Mungu kwa siku hii nzuri aliyonipa maana kwakweli muda nao umekuwa mali.

Natamani sana kila wiki niendeleze Makala haya lakini mara nyingine tunabanwa na muda lakini pia Mungu ana makusudi kwa kila jambo.

Leo naomba tuzungumze jambo hili muhimu sana katika mahusiano, linalohusu pale mtu anapokuwa na matarajio kwamba mwenzi wake atakuja kubadilika tabia yake mbaya au isiyombariki baada ya kuingia kwenye Ndoa

Hii inakuwa hivi inawezekana watu wamekaa katika uchumba wanavyoendelea kuna tabia unaziona kwa mwenzi wako ambazo unaona kwamba ni ngumu yaani hazibebeki, lakini unaamua kwamba utaendelea maana unajua kwamba ukimuoa au akikuoa utakuwa na Mamlaka ya Kuweza Kumbadilisha au Kukomesha hiyo tabia.

Sisemi kwamba watu wenye udhaifu fulani hawawezi kubadilika,HAPANA mtu yoyote yule anaweza kubadilika ila Mabadiliko yatatokea tu pale mtu ANAAMUA kubadilika na sio kung`ang`anizwa kubadilishwa.

Hakuna aina ya ubabe ambao wewe mke au mume unaweza kutumiakwenye Ndoa ili kubadilisha tabia yake, sio pesa, sio chochote kitakachoweza kubadilisha mtu

Unaweza kuwa na mchumba ambaye ana mahusiano mengi mengi, leo umemkuta na meseji za Joyce, Kesho za Jane,mara umesikia jana alikuwa na mwingine sijui KFC au Steers pale, wengine tena wanakutumia labda meseji za kejeli au wengine wanakupigia simu kwamba huyo ni cha Wote, lakini wewe unang`ang`na kwamba eti huyu mtu wangu atabadilika pale tu Nitakapomuoa….

Kuna kisa nilikisikia hivi karibuni kaka alikuwa mchumba, kumbe huyo dada alikuwa anaendeleza mahusiano ya zamani kisirisiri, sasa kibaya sana siku mbili kabla ya harusi kuna mtu alimuona huyu mwanadada akiwa ametoka kwa yule mtu wake wa zamani, huyu kaka aliambiwa lakini akasema huyo mimi nikimuoa nitamkomesha hataweza kutoka hata ndani nitamfungia, NITAMBADILISHA.

Je Ndugu yangu unafikiri kweli kwa tabia hii huyo dada yetu ataacha mahusiano hayo, kama kweli anashindwa kuheshimu ndoa yake kabla hajaingia maana hapo hata huyo mume hajamjua vizuri je akishaishi naye kweli ndio ataiheshimu hiyo Ndoa. Hebu tafakari hili mpendwa wangu....

Neno katika Mathayo 6: 24“Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.”

Ukisoma Maneno ya Mungu hapo juu neno liko wazi Kabisa kwamba mtu huwezi kutumikia mabwana wawili yaani huwezi kushika mambo mawili lazima kuna moja utalidharau na kuzingatia lingine.

Tuesday, August 5, 2014

USALAMA NA UBORA WA NAFSI YAKO UNAVYOHUSIANA NA UHAI WA KANISA na Mwl Samwel Mkumbo -Sehemu ya Kwanza

Karibuni katika makala haya yanayoletwa kwani na Mwalimu Samwel Mkumbo
 
Mwalimu Samwel Mkumbo

Uhai wa kitu chochote kile unategemea namna au jinsi mwenye huo uhai au aliyekabidhiwa dhamana yuko katika hali gani, unaweza kulaumu juu ya uharibifu wa jambo au mambo Fulani lakini kabla ya kulaumu angalia kwanza yeye aliyeharibu au aliyekabidhiwa mikononi mwake yuko katika hali gani.

MATENDO 20:28 inasema hivi;

Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.

Sasa kabla sijaendelea Zaidi nataka niseme jambo la msingi sana hapa, kichwa cha Somo letu kinatuhitaji tuwe na ufahamu wa kuhakikisha kwamba kila tunachokiongea katika somo hili ni mambo makubwa mawili, NAFSI YAKO NA KANISA LAKO. Wewe ni nafsi moja katika kanisa, Je unayo kazi gani wewe kama Nafsi?

Unaweza usijue wala usiliangalie kwa uzito, lakini inapasa kuelewa tafsiri hii;

KANISA ni Nafsi za watu zilizounganishwa kwa kunia mamoja katika Imani yao na hiyo Imani wameijenga katika msingi wa YESU KRISTO, hivyo kanisa bila ya nafsi zilizokubaliana za watu wengi wa aina mbalimbali si kanisa maana ili wawe kanisa lazima nafsi zao ziungane kwa kunia mamoja na kuwa na Imani moja ambayo hiyo Imani ndiyo inatengeneza nia moja.

TAZAMA NAMI:

Ili kanisa liwe na Nguvu na likae katika mstari unaotakiwa ni lazima nafsi za watu ndani ya Kanisa ziwe ziko salama kabisa, yaani ziwe zimetunzwa katika hali ambayo uhakika wa kundi kuishi kwa Amani utakuwepo kwa uhakika.

Labda tuunganishe vipande viwili vya huo mstari wetu wa msingi ili uone jambo la msingi kidogo….. Jitunzeni nafsi zenu,,.,.. mpate kulilisha kanisa lake Mungu,.,.,..

Mfano wa Mtumwa Mwaminifu

Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye wakili mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo. Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote. Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa; bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini (LUKA 12:42-46)

Sasa hapo ninataka nikufundishe jambo ambalo kimsingi ambalo halipo kwenye Mistari hiyo hapo juu, na lenyewe ni juu ya adhabu aliyopewa huyo wakili. Ona mtari huu;,..,.. akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, AKILA NA KUNYWA NA KULEWA;,.,….

Maana suala sio kusema bwana wake anachelewa ila baada kuona bwana wake anachelewa alifanya nini? Na wala sio kuwapiga watumwa ila baada ya kuwapiga watumwa alifanya nini? Yeye alichokifanya ni KULA NA KUNYWA NA KULEWA,..,..

Biblia inaposema yeye ALIKULA NA KUNYWA NA KULEWA, maana yake aliacha kufanya alichotakiwa kufanya lakini pia aliiharibu nafsi yake kwa MVINYO yaani kwa Ulevi. Maana suala si kula na kunywa kwa sababu hayo ni mahitaji ya mwili wa kila mtu, lakini suala ni KULEWA na biblia inasema KILEO HUDHIHAKI,. Na pia HUPOTOA HUKUMU ZA HAKI.

Friday, July 25, 2014

JE UMEKATALIWA

                 
 

Mara Nyingi utasikia mtu akisema yule jamaa Ana Roho ya kukataliwa au mimi jamani kila ninachokifanya nakataliwa au kila ninapoenda nakataliwa.                         
 
Inawezekana umekataliwa mambo mengi katika maisha tena kibaya zaidi umekataliwa na watu wako wa karibu kama ndugu, jamaa na marafiki au pia waweza.kujikuta umekataliwa na wafanyakazi wenzako au wafanyabiashara wenzako au watumishi wenzako, wanafanya maamuzi makubwa lakini hawakihusishi labda wanakudharau wanaona kwamba hustahili kujua.     
Mara nyingi familia zimekuwa na tabia ya kuwakataa na kuwatenga wenye kipato kidogo katika familia, yamkini wewe ni mzaliwa wa kwanza lakini familia haikudhamini IMEKUKATAA kwasababu hawaoni mchango wako na.kwakweli hujafanya makusudi ni kwamba huna tu cha kutoa, wameuza uzaliwa wako wa kwanza kwa mdogo wako ambaye ndio Tajiri wa familia, wanaamua maamuzi makubwa ya familia hawakushirikishi kwasababu tu huna kitu.     Ndugu yangu watu wamekudharau ,wamekucheka, wamekung'ong'a kwasababu huna kitu au huna elimu au huna mtoto au huna mwenzi wa maisha, labda hali yako ya kukataliwa imesababisha huna hata pa kukaa wala huna wa kukupa chakula Ndugu yangu nimekuja kuongea na wewe siku ya Leo waliokukataa ni wanadamu tu ila Mungu hajakukataa wala hana mpango wa kukutaa unayo sababu ya kufurahi siku ya Leo kwasababu mfalme wa wafalme ,Mungu Mkuu,Jehova,Yahweh,HAJAKUTAKAA.                 
 
Ukisoma 1 Petro 2: 4-9, utaona jinsi hata Yesu alikataliwa lakini maandiko yanasema katika mstari wa 4 "Mmwendee yeye jiwe lililo hai lililokatakiwa na wanadamu lakini kwa Mungu ni TEULE LENYE HESHIMA".                         
 
Yesu alikataliwa na wanadamu, alipigwa, alidhihakiwa, alitemewa mate,alidharauliwa , ALIKATALIWA tena kwa watu wake wenyewe wakimkejeli huyu si mtoto wa fundi seremala tu iweje Leo a anatuletea wokovu kwasababu wao walikuwa na madaraja kwamba labda katika ukoo Fulani tu au watu wa aina Fulani ndio tu wanaweza kuwa wazuri wakasahau Yuko Mungu ambaye njia zake hazichunguziki,anayejua Mwanzo na Mwisho wake, Leo ndugu yangu ukumbuke Mungu ni yeye yuleyule hajabadilika anakuon tofauti na watesi wako wanavyokuona, hali ya sasa isikufanye ukakata tamaa ukakosa Baraka na Miujiza Mikubwa iliyo mbele yako, hivi unajua ndugu yangu wewe ni Uzao mteule,kuhani wa kifalme, taifa takatifu, mtu wa Milki ya Mungu? Usisikilize kelele zao Mungu anakuwazia mawazo Mema, hakuna mwanadamu mwenye usemi wa mwisho juu ya mustakabali wako aliyekuumba ndio anajua mustakabali wako yeye ndio anakujua, wao wakiona maskini, Mungu anakuona Tajiri, wakikuona huzai Mungu anaona hakuna tasa katika Israel, wakiona wewe wa mwisho Mungu anakuona kichwa wala si mkia, Wewe ni Mshindiiii.                          
 
 Inuka Mungu HAJAKUKATAA.........Haleluyaa

Tuesday, July 22, 2014

TAMBUA BARAKA ZINAZOKUJIA ZINATOKA WAPI Sehemu ya Pili (II) na Mwalimu Samwel Mkumbo

Bwana Yesu asifiwe mpendwa wangu, Karibu tena katika makala haya ya mafundisho ya Neno la Mungu yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo.
Kwa kifupi Mwalimu Samwel Mkumbo ni Mhitimu wa Chuo Kikuu mwenye wito na karama ya Kufundisha Neno la Mungu.

Karibu tuendelee na Sehemu ya Pili ya Somo hili lililoanza wiki iliyopita, kama hujasoma sehemu ya Kwanza nakushauri pitia katika blog hii usome sehemu ya kwanza ili kupata mtiririko mzuri wa Somo.

 
Mwalimu Samwel Mkumbo


Ø  Chanzo cha Mapato ya Anayetoa/ Chanzo cha Sadaka yenyewe.

Kuna wakati tunaweza kujua nini uamuzi wa kufanya au nini ni nia ya sadaka tunayopokea kwa kuangalia chanzo cha mapato ya anayetoa, au chanzo cha sadaka hiyo. Tazama mfano huu;

Huyo mfalme akawaagizia posho ya chakula cha mfalme,na ya  divai aliyokunywa, akaagiza walishwe hivyo muda wa miaka mitatu; ili kwamba hatimaye wasimame mbele ya mfalme……….. Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa…….. (Danieli 1: 5, 8).

Ninachotaka tuone hapo ni kwamba pamoja ya kwamba hawa vijana watatu, naam, huyo Danieli, Meshaki, Shedraki na Abednego walipata nafasi ya kupata chakula kizuri kutoka katika meza ya mfalme tena wakiwa katika nchi ya ugeni bila kusahau walikuwa na hadhi ya utumwa, lakini hawakukubali kupokea hiyo Baraka au zawadi kutoka Ikulu, tena Biblia imeweka kweupe sababu yao, ni kwamba hawakutaka kujitia unajisi.

Maana walijua ya kuwa kuna uwezekano ya kuwa kama  ni nyama basi zitakuwa zilizokuwa zimetolewa sadaka kwa miungu ya Wababeli, lakini pia hawakupenda kunywa mvinyo yao wala kitu chochote, lakini pia hawakutaka kujitia unajisi kwa chakula cha mfalme na ilikuwa ni mila na desturi ya wayahudi kutoshiriki chakula na watu wa mataifa.

Japokuwa biblia haijaweka kweupe ni lini hasa au wakati ambao hao wakina Danieli waliacha kula mtama au ni lini walianza kula vyakula vya kawaida lakini sabab kubwa ya kukataa ni kwamba walikataa chanzo cha chakula hicho.

Ø  Uhusiano wa mtoaji na watu wengine.

Kuna wakati mwingine watu hupenda kuwafadhili watumishi wa Mungu na kuonesha wema kwa watumishi wa Mungu, tena sana. Lakini unakuta mtu huyo huyo huwatendea watu wa nyumbani mwake mambo maovu, na hata kama si watu wa nyumbani mwake lakini hata watu wengine wa kawaida huwatendea mambo yasiyo mema wala hawafadhili, au kuwatendea wema nga kidogo. Jambo kama hilo si jema na ni vema mtu kama huyo uwe nae makini sana maana inaweza kuwa mtego sana kwako, lakini pia inaweza kuwa laumu kwa hao anawatendea mabaya maana wanaweza kuona kuwa unawafanyia fitina,. Tusome pamoja hapa; 

……..Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio….(Wagalatia 6:10).

Lakini kwa makini tena tazama maneno haya…………tuwatendee watu wote mema;….na hasa jamaa ya waaminio…..

 

Ushauri wa Ziada.

Katika kukaa katika nafasi nzuri ya utumishi na mahusiano mazuri na watu na namna ya kuangalia jinsi tunavyotumika tazama kitabu cha TIMOTHEO.

Monday, July 21, 2014

The Assemblies of God to Celebrate 100th Anniversary in US





The Assemblies of God is the U.S.'s oldest Pentecostal denomination. (Assemblies of God)

Worldwide members of the Assemblies of God (AG), one of the fastest-growing international protestant denominations, will join together in the U.S. this fall to celebrate the AG's 100th anniversary year, the unity they have shared for the past century and the remarkable growth of the denomination globally.

Established as an outgrowth of the 1906 Azusa Street Revival among Pentecostals in the U.S., the General Council of the Assemblies of God was formed in Hot Springs, Arkansas, in April 1914 as a broad coalition of ministers who desired to work together to fulfill common objectives, such as sending missionaries around the world and providing fellowship and accountability.

"This centennial event will be a moment of revival, a moment of celebration and a moment of focusing on our mission, to complete the great unfinished task of ensuring every person has a chance to hear of Jesus' love for them," said Dr. George O. Wood, General Superintendent of the Assemblies of God. "This 100th anniversary gives us the opportunity to focus on what God still has for us to do as we look with joy to our past history, give thanks for the present and look forward to what we still have to accomplish in the future."

Following its formation in 1914, the Assemblies of God quickly took root in other countries and formed indigenous national organizations. The Assemblies of God throughout the world now exceeds 67.5 million adherents, including more than 3.1 million members in the U.S. The denomination has experienced 24 years of consecutive growth, bucking the trend among most other U.S. denominations in recent years.

The Centennial Celebration will be a truly international event, with guest speakers from AG churches all over the world. In addition to Dr. Wood, keynote addresses will be delivered by Yong Mok Cho of South Korea, Juan Carlos Escobar of Spain, Edward A. Grabovenko of Russia, Lazarus Chakwera of Malawi, Barnabas Mtokambali of Tanzania, Ivan Satyavrata of India, José Wellington of Brazil and Max Schläpfer of Switzerland. Other U.S. speakers include Hal Donaldson, John Lindell, Wilfredo "Choco" De Jesús, Nam Soo Kim, Jason Frenn (who ministers in Latin America) and Raegan Glugosh, a U.S. missionary to Romania.

The Centennial Celebration is expected to be one of the largest international gatherings of AG members, with more than 5,000 individuals traveling from 112 different countries to attend.

In addition, many of the sessions will be carried live via direct simulcast and international television networks. Churches throughout the U.S. will serve as live simulcast hosts, while Unsión will broadcast live to Latin America, where the AG has over 30 million adherents, and LMTV will broadcast live to Africa, where the AG has over 17 million adherents.


Source: Charisma
 

Tuesday, July 15, 2014

TAMBUA BARAKA ZINAZOKUJIA ZINATOKA WAPI na Mwalimu Samwel Mkumbo

Bwana Yesu asifiwe mpendwa karibu sana katika makala haya yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo.

Mwalimu Samwel Mkumbo
Hakika Baraka ni jambo mojawapo la msingi sana kwa  watoto wa Mungu na ni jambo la Faraja tuonapo mwana wa Mungu akifanikiwa katika mambo yake yote. Kama inenwavyo;

..,….Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli. Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo…,… (3Yoh 1:1-2)

Sasa basi ni vema ukafahamu  ya kuwa kubarikiwa ni jambo la msingi sana na tena ni moja ya ushuhuda kwa watoto wa Mungu. Lakini pia Baraka ni kutukuka sana katika Ukuu wa Mungu na pia juu ya haya yote tunaweza kuona ni kwa jinsi gani uweza  wa Mungu unajidhihirisha katika mambo yetu ya mwilini naam katika kutuma mema katika Tumaini jipya la imani yetu.

Lakini pia Biblia inatupa maelezo kadhaa juu ya kupata Baraka au mafanikio maana si kila mafanikio (Baraka) zina mkono wa Mungu ndani yake, au ni utukufu wa Mungu mingine ni mitego ya shetani katika kutuangusha katika imani yetu katika KRISTO YESU, naam! Maandiko matakatifu yanatupa mifano kadhaa ya Baraka zitokazo kwa Mungu na zile zinazoletwa na mwovu kama mtego kwetu.

Vielelezo!!

-Habari za Elisha na Naamani.

2 Wafalme 5:1-14 tunaona kisa kizuri na cha kutufundisha juu ya Baraka.

Nabii Elisha alipata nafasi ya kufanya muujiza wa uponyaji kwa Naamani (Yule jemadari wa Shamu) juu ya ukoma wake, na baada ya muujiza huo, mtu huyo, huyo Naamani alitaka kumpa zawadi Elisha, lakini Elisha hakukubali,. 2 Wafalme 5: 15-16 inasema;

Akamrudia Yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa  tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako. Lakini akasema, Kama BWANA aishivyo ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutisha apokee, lakini akakataa.

Katika maandiko hayo utaona ya kuwa Elisha hakupokea Baraka kutoka kwa Yule Jemadari naam, huyo  Naamani, lakini ni vema tukafahamu ya kuwa si kwa sababu Elisha alikuwa na tabia ya kutopokea zawadi na Mbaraka kutoka kwa watu aliowahudumia, la hasha! Bali ipo sababu nyingine, maana  ni Elisha huyu huyu alipokea msaada kutoka kwa mama Mshunami! Tazama hapa;  2Wafalme 4:8

Kwa hiyo si kila tunuku unayopewa ni ya kukubali lakini pia si zote ni za kukataa maana kila jambo lina maana yake na matokeo yake ambayo kwa hayo twaweza kutambua kusudi na mapenzi ya Mungu kwetu lakini pia hila na mitego ya shetani.


-Mfano wa Yesu.

Wednesday, July 2, 2014

Nigerian Gospel Singer Sinach weds Pastor Joseph

 
Nigeria Gospel Singer, Osinachi Kalu popularly known as Sinach last Saturday June 28th exchanged vows with Pastor Joseph at Christ Embassy Church, Ikeja, Lagos.
 
Sinach is Globally known for her  hit Song " I Stand Amazed"
 
 
Sinach and Husband Pastor Joseph
 
 
With this Ring....
 









 


Wow I am so happy for you Sinach

Monday, June 23, 2014

NAFSI ILIYONASWA na UZINZI na Frank Philip



Mtumishi Frank Philip
Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani …Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika” (Mithali 6:26 & 32,33).

Nimeona jambo hili, nami nikatafuta kujua kama kuna hekima ndani yake “men’s hearts can be shared, but women’s hearts replaces”. Maana yake: Moyo wa mwanaume ukipenda, waweza kupenda tena kwa wakati mmoja, ila moyo wa manamke ukipenda, humwondoa wa kwanza na kumpenda mwingine.

Ukitaka kuona kwa njia ya urahisi, jiulize ni kwanini mwanaume mmoja anaweza kuoa wake zaidi ya mmoja na maisha yakaenda? Na jiulize tena, je! Mwanamke anaweza kuwa na mpenzi wa nje ampendaye sana, na maisha yake ya ndoa/mahusiano yakawa sawa? Wote wawili: mwanamke na mwanaume, wana hatari ya kuingiliwa mioyoni mwao, japo kwa madhara tofauti.

Hii hali sio rahisi kuikubali katika mahusiano ya kawaida ambapo mtu anatoka nje ya ndoa/uhusiano kwa siri. Mara nyingi mtu afanyaye mambo hayo, hudhani yuko sawa, kumbe ameathirika kabisa. Ukitaka kujua ninachosema, angalia mambo ya kawaida kabisa ya kwenye ndoa/uhusiano kwa watu ambao mmoja au wote wamenaswa nafsi na kahaba. Mambo ya kawaida kabisa kwenye uhusiano/ndoa yanaanza kuwa kero, mzigo na ya kuchosha. Ukiona hii shida, usipambane na mtu kwa jinsi ya mwilini, shughulika na nafsi kwa sababu hapo ndipo penye shida.

Nitasema na wanawake sasa. Hii hali ya “replacement”, huwa haianzi mara moja. Huenda kwa awamu, na hatua mbali mbali, kuanzia hisia, matendo kisha ngono. Ndio maana mwanamke akitoka nje ya ndoa watu husema “amefika mbali”. Mara zote huanza na “nafsi kunaswa” na kahaba. Kama kuna mtego mbaya, ni kuacha nafsi yako inaswe. Kwenye nafsi ndiko kuliko na mawazo na maamuzi. Kama nafsi imenaswa, mara ZOTE mtu ataanza kuwaza tofauti, na kisha kufanya maamuzi mabaya. Ndio maana tunaonywa sana kwamba “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima” (Mithali 4:23). Ukitaka kuona uzima kwenye ndoa/uhusiano wako, linda sana moyo wako; ukitaka kuona mauti kwenye ndoa/uhusiano wako, achilia moyo wako uingiliwe.

Friday, June 20, 2014

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili na Mama Mchungaji Deborah Said amefariki Dunia

 
Deborah Said wakati wa uhai wake
 
Mama Mchungaji na mwimbaji wa Nyimbo za Injili Debora Said amefariki dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 20/06/ 2014 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Deborah Said ni mke wa Mchungaji John Said wa Kanisa la Victorious Living lililopo Mabibo External

Marehemu ameacha watoto wanne na Mgane Mchungaji John Said

Katika Uhai wake Deborah Said alikuwa ameimba nyimbo mbalimbali za Kumsifu na Kumwinua Mungu, utumishi wake uliwagusa wengi hata Tanzania, siku si nyingi alikuwa amezindua albamu yake ya Mti wenye Matuda

Deborah Said akizindua Albamu yake ya Mti wenye Matunda kabla hajatangulia kwa Baba
 
Blog imefanikiwa kuongea na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili wa Chama  cha Muziki wa Injili Tanzania  MC Joshua Makondeko ambaye amesikitishwa sana na msiba huu na Mara nyingi tuliona akituomba sana katika facebook wall yake tumuombee Deborah na hata Deborah aliporuhusiwa hospitali  aliendelea kumshukuru Mungu kwa Uponyaji wa mwimbaji huyo wa nyimbo za Injili, kwasasa MC Joshua Makondeko yuko safarini  Rukwa ameomba kila waimbaji wa Injili wote wafike kuifariji familia pia wafike na mchango wa elfu 10 wamuone Cosmas Chidumule

Msiba uko nyumbani kwao nyuma ya Mabibo Hostel karibu na Pepsi Bar uliza kwenye Msiba wa mama Mchungaji

Programu ya mazishi itakuwa kuanzia hawajaamua mpaka sasa ila itakuwa kuanzia wiki ijayo, Blog itaendelea kuwapata taharifa ya Ratiba ya Mazishi


POLENI WOTE KWA MSIBA HUU,Roho Mtakatifu Awafariji yeye ndiye Mfafiji wa Kweli