Wednesday, August 21, 2013

Uchumba hadi Ndoa: Jifunze kutokana na Makosa ya Nyuma


Watarajiwa
 
Leo katika mwendelezo wa Somo la Uchumba hadi Ndoa na Vitu muhimu vya kuangalia unapotafuta  au kujiandaa kuwa na mwenzi wa maisha yako ,nawaletea kwenu hili swala muhimu sana la kujifunza kutokana na makosa ya huko nyuma.

Kama ulishakuwa katika mahusiano mengine huko nyuma na hayakwenda vizuri yakavunjika basi unalo jukumu la kujiuliza maswali hivi ni kwanini yale mahusiano yalivunjika. Je mimi ndie nilishababisha na kwanini? Je kama ni huyo mtu mwingine alivunja je ni kwanini aliyavunja? Au ni watu wengine walivunja kama vile ndugu za mwenzako au marafiki ni kwanini waone kwamba labda hatustahili kuwa pamoja?

Ukishatathimini hayo utaweza kujua kwamba labda mara nyingine sio kwamba unatakiwa umwachie tu Mungu ila na wewe unayo kazi ya kufanya ili yasitokee tena. Watu wengine wanapoona mahusiano yamevunjika wanajisahau kwamba na wao ni wanadamu kwahiyo wanakuwa tu na mtazamo kwamba mimi nilikuwa perfect na wala hataangalia kama kuna vitabia ambavyo vilichangia mahusiano yake ya nyuma yavunjike.

Ni kweli kabisa kuna wakati mahusiano yanavunjika mpaka kila kitu kinamwinua Mungu kwa hilo maana mtu alikuwa ananyanyasika na huo uhusiano haukuwa mpango wa Mungu kabisa. Lakini sio wakati wote kwamba huyo anayelalamika ndio aliyekosewa ila makosa yalikuwa yake ila mwenzake alimalizia tu kwa kuvunja.

Mtu anaweza kuwa kwenye uhusiano akawa na majivuno sana kiasi kwamba hata huyo mwenzake anamdharau anamuona kama vile amebahatika sana kukutana nay eye. Anamdharau hata mbele za watu,mwenzako anajaribu kukurekebisha lakini hurekebishi sasa anaanza kukukimbia taratibuuu halafu baadae unakuja kulalamika yaani alianza kutokueleweka kumbe wewe ndio ulisababisha.

Kama umejichunguza ukagundua kabisa kwamba kuna tabia fulani unayo ambayo mwenzako aliyeingia mitini alikuwa anailalamikia kwamba haipendi ni vizuri ukachukua hatua kubadilika maana utaingia kwenye mahusiano mwengine na usipokuwa makini atakimbia na huyo kumbe tatizo ni wewe.

Kuna mtu alinishuhudia alikuwa ameingia kwenye mahusiano na kijana ambaye ni wa maisha tu ya kawaida nay eye huyo dada alitoka katika familia yenye uwezo mkubwa lakini pia alikuwa na tabia ya kujiinua sana na kudharau watu ambao ni wa hali ya chini. Sasa hizo tabia akazipeleka kwa huyo mtarajiwa akawa anamdharau sana na kumringia mwenzake alijitahidi kumweleza lakini alishupaza shingo hakubadilika, alishangaa tu analetewa kadi yule kaka anaoa kwakweli alijifunza somo kubwa japo kwa maumivu makubwa. Akaniambia kutoka hapo aliweza kujifunza kutokana na makosa aliyoyafanya akajifunza kujishusha maana pia haikuwa rahisi,Ila alimuomba sana Mungu amuondolee kiburi na majivuno na amfundishe kujishusha, Mungu ni mwaminifu maana alimshughulikia akamfanya kiumbe kipya kwelikweli,

 na baadae Mungu alikuja kumpa mwenzi wake wa Maisha na kwasababu alishashughulikia ule udhaifu wake Mungu alifanya njia wakafunda ndoa nzuri tu.

Nimekupa huu ushuhuda ili ujue kwamba pamoja na kwamba unaomba, unafunga au unafanyiwa ukombozi ujue unalo Jukumu la kubadili tabia kwa kujifunza kutoka makosa ya nyuma usicheleweshe muujiza wako mpendwa.

Amua leo kubadilika, amua leo chukua hatua inawezekana hata ofisini, au marafiki kuna mrejesho nyuma wamekupa ili ubadilike hivyohivyo ndivyo vinawafanya wale wadada au wakaka wakimbie hebu badilika kama hatutakula Pilau siku za Usoni.

 

Pamoja na hili soma masomo mengine ya Vitu vya kuangalia unapojiandaa kuwa na mwenzi wa Maisha yaliyoandikwa katika blog hii.

 

Ubarikiwe sana

2 comments:

  1. nashukuru kwa somo lako,mungu akubariki sana

    ReplyDelete
  2. KWANZA NAMSHUKURU MUNGU KWAKUNIWEKA HAI MPAKA SASA,PIA NIKUSHURU KWAKUTUPA ELIM YA KIMUNGU.BINAFSI NIMEJIFUNZA MENGI.MUNGU AWAPE AFYA YA MWILI NA ROHO ILI MUWEZE KUENELEA KUTUPA ELIMU ZAIDI.MUNGU AWABARIKI SANA

    ReplyDelete