Wednesday, November 20, 2013

Christina Shusho anakuletea Tamasha Kubwa la Nataka Nimjue


Christina Shusho muimbaji wa Nyimbo za Injili

Muimbaji mahiri wa Nyimbo za Injili nchini Tanzania Christina Shusho anategemea kufanya tamasha Kubwa la kusifu na kuabudu litakaloambatana na kurekodi Live Albamu ya Nataka Nimjue.

 

Uzinduzi huo unategemea kufanyika Jumapili tarehe 24/11/2013 katika ukumbi wa Kanisa la CCC Upanga mkabala na Mzumbe University Dar.

 


Siku hiyo Christina Shusho atasindikizwa na waimbaji wengine mahiri wa Nyimbo za Injili kama Bahati Bukuku, John Lisu, Upendo Kilahiro, Paul Clement, Joshua Mlelwa, Amani Kapama, The Voice and Kinondoni Revival Choir

 



 


Kiingilio ni 10,000/= Wakubwa, 20,000/= VIP na 3,000/= Watoto

 

Historia yake ya kuimba Christina Shusho ilianzia alipokuwa Sunday school kanisani, akaendelea kuimba Kwaya mbalimbali na mwaka 2004  ndipo alipoweza kutoa album yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la Ni Kitu Gani.

                                        Waweza kuangalia Nataka Nikujue hapa

Alipokuwa akizungumza na Blog ya Rejoice and Rejoice Christina Shusho alisema siku hiyo watu wategemee kukutana na Mungu wa leo na kuna kitu Mungu anakwenda kufanya maana atatembelea watu kwa kupitia ibada ya kusifu na kuabudu. Watu watakutana  na Nguvu ya Mungu.

 

 
CHRISTINA SHUSHO Rejoice and Rejoice Blog tunakutakia maandalizi mema na Mungu akakutumie siku hiyo, Amen

No comments:

Post a Comment