Tuesday, July 22, 2014

TAMBUA BARAKA ZINAZOKUJIA ZINATOKA WAPI Sehemu ya Pili (II) na Mwalimu Samwel Mkumbo

Bwana Yesu asifiwe mpendwa wangu, Karibu tena katika makala haya ya mafundisho ya Neno la Mungu yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo.
Kwa kifupi Mwalimu Samwel Mkumbo ni Mhitimu wa Chuo Kikuu mwenye wito na karama ya Kufundisha Neno la Mungu.

Karibu tuendelee na Sehemu ya Pili ya Somo hili lililoanza wiki iliyopita, kama hujasoma sehemu ya Kwanza nakushauri pitia katika blog hii usome sehemu ya kwanza ili kupata mtiririko mzuri wa Somo.

 
Mwalimu Samwel Mkumbo


Ø  Chanzo cha Mapato ya Anayetoa/ Chanzo cha Sadaka yenyewe.

Kuna wakati tunaweza kujua nini uamuzi wa kufanya au nini ni nia ya sadaka tunayopokea kwa kuangalia chanzo cha mapato ya anayetoa, au chanzo cha sadaka hiyo. Tazama mfano huu;

Huyo mfalme akawaagizia posho ya chakula cha mfalme,na ya  divai aliyokunywa, akaagiza walishwe hivyo muda wa miaka mitatu; ili kwamba hatimaye wasimame mbele ya mfalme……….. Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa…….. (Danieli 1: 5, 8).

Ninachotaka tuone hapo ni kwamba pamoja ya kwamba hawa vijana watatu, naam, huyo Danieli, Meshaki, Shedraki na Abednego walipata nafasi ya kupata chakula kizuri kutoka katika meza ya mfalme tena wakiwa katika nchi ya ugeni bila kusahau walikuwa na hadhi ya utumwa, lakini hawakukubali kupokea hiyo Baraka au zawadi kutoka Ikulu, tena Biblia imeweka kweupe sababu yao, ni kwamba hawakutaka kujitia unajisi.

Maana walijua ya kuwa kuna uwezekano ya kuwa kama  ni nyama basi zitakuwa zilizokuwa zimetolewa sadaka kwa miungu ya Wababeli, lakini pia hawakupenda kunywa mvinyo yao wala kitu chochote, lakini pia hawakutaka kujitia unajisi kwa chakula cha mfalme na ilikuwa ni mila na desturi ya wayahudi kutoshiriki chakula na watu wa mataifa.

Japokuwa biblia haijaweka kweupe ni lini hasa au wakati ambao hao wakina Danieli waliacha kula mtama au ni lini walianza kula vyakula vya kawaida lakini sabab kubwa ya kukataa ni kwamba walikataa chanzo cha chakula hicho.

Ø  Uhusiano wa mtoaji na watu wengine.

Kuna wakati mwingine watu hupenda kuwafadhili watumishi wa Mungu na kuonesha wema kwa watumishi wa Mungu, tena sana. Lakini unakuta mtu huyo huyo huwatendea watu wa nyumbani mwake mambo maovu, na hata kama si watu wa nyumbani mwake lakini hata watu wengine wa kawaida huwatendea mambo yasiyo mema wala hawafadhili, au kuwatendea wema nga kidogo. Jambo kama hilo si jema na ni vema mtu kama huyo uwe nae makini sana maana inaweza kuwa mtego sana kwako, lakini pia inaweza kuwa laumu kwa hao anawatendea mabaya maana wanaweza kuona kuwa unawafanyia fitina,. Tusome pamoja hapa; 

……..Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio….(Wagalatia 6:10).

Lakini kwa makini tena tazama maneno haya…………tuwatendee watu wote mema;….na hasa jamaa ya waaminio…..

 

Ushauri wa Ziada.

Katika kukaa katika nafasi nzuri ya utumishi na mahusiano mazuri na watu na namna ya kuangalia jinsi tunavyotumika tazama kitabu cha TIMOTHEO.

No comments:

Post a Comment