Thursday, April 17, 2014

Boko Haram Kidnaps Nearly 200 School Girls in Nigeria; Parents Facing 'Nightmare'


Islamic terrorist organization Boko Haram reportedly kidnapped nearly 200 girls from a boarding school in northeastern Nigeria.

"They took away my daughter," said one woman from Chibok, who asked for anonymity due to the uncertain fate of the children, according to AFP.

"I don't know what to do," the mother added. "They should not allow our daughters' dreams to be shattered by these murderers."

CNN reported that as many as 200 girls were taken from Government Girls Secondary School in Chibok Monday night after heavily armed Boko Haram Islamists stormed the boarding school in trucks, vans and buses.

"The Boko Haram attackers came to town around 9 p.m. and made straight for the school where they had a gun battle with soldiers stationed at the school and killed two soldiers," said Chibok resident Maina Babagana.

A father, whose daughter was also taken in the raid, described the ordeal as a "nightmare," and said that the whole town of Chibok is in mourning.

Tuesday, April 15, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Jifunze kuchukuliana na Mwenzi wako



Hata Mungu anafurahi ndoa inapokuwa na furaha na raha
 
Karibu katika masomo haya ya Uchumba hadi ndoa ,yanayoletwa kwenu na Mshauri wako wa Mahusiano na Ndoa.

Kwanza nikuombe sana radhi kutorusha masomo haya kwa muda mrefu lakini sasa kwa uwezo wa Mungu tutakuwa tunaendelea na masomo yetu kila wiki.

Kwahiyo uweke katika kalenda na kumbukumbu zako kila siku ya Jumanne tutakuwa na masomo haya….Karibu tuendelee..

Leo naomba nizungumzie kitu ambacho ni muhimu sana kwa mahusiano na ndoa pia. Unapojiandaa kuingia katika ndoa unapaswa kujiandaa jinsi utakavyokwenda kuishi na mwenzi wako. Maana uhusiano unaouendea sio kama ule uliokuwa nao na Baba, Mama, kaka, dada au bibi yako ni Zaidi sana mpendwa, unaingia katika uhusiano wa karibu wa ndani mtu ambaye utalala naye kitanda kimoja kila siku na wakati.
Mwenzi wako wa ndoa ni mtu wa karibu hata kama hujisikii kumuona

Mtu ambaye iwe jua iwe mvua utakuwa unamuona.

Mtu ambaye hata kama hujisikii kuongea na mtu siku hiyo atakuongelesha

Mtu ambaye hata kama hujisikiaa kumuona atakuwepo hapo na utamuona

Ni mtu ambaye lazima uwe naye karibu hata kama siku hiyo amekukwaza sanaa

Ndio maana nikaona kuna umuhimu wa kuwa na masomo haya maana mengi yametokea kama tunavyoona katika jamii sasa, talaka sasa inatolewa tu kirahisi rahisi tu, zamani nilipokuwa mdogo kiukweli kabisa nilikuwa sijui kama kuna talaka huo ndio ukweli wangu. Mungu alinipa neema ya kuwa katika mazingira hayo, sasa nilipokuwa na nikawa mjini ndipo nikasikia hiyo sentensi lakini bado niliona kama ni ya kundi fulani tu lakini nakuambia sasa inaogopesha maana imeingia kanisani. Katika kutafakari haya Mungu akanipa mzigo huu niseme na nyie watu wake kwamba NDOA BILA TALAKA INAWEZEKANA,Amen..

Haya tuendelee na Somo letu sasa, kuhusu kuchukuliana ni hali ya kumuelewa mwenzako pale anapofanya kitu ambacho hakikufurahishi au usichokipenda. Lakini kuchukuliana sio kupuuzia au kudharau naomba nitofautishe maana wengi wanapuuza au kudharau mambo wenzao wanayoyafanya hiyo nayo yaweza kuleta shida.

Monday, April 14, 2014

Mambo ya Msingi Kanisa linayoweza kupata kwa kujua/ kufahamu asili yake Sehemu ya II na Mwalimu Samwel Mkumbo

Mwalimu Samwel Mkumbo
Wiki iliyopita tulitazama kwa sehemu kama Utangulizi tu unaotupeleka kwenye Kujua kulingana na Somo hili juu ya MAMBO YA MSINGI KANISA LINAYOWEZA KUPATA KWA KUJUA/KUFAHAMU ASILI YAKE. Karibu tuendelee mtu wa Mungu,

 
Upo umuhimu sana wa kufahamu Asili ya Kanisa, na kama nilivyosema hapo mwanzoni ni kwamba si kwamba ninazungumzia Asili ya Kanisa kwa mtazamo wa Historia yake au mpangilio wa matukio yaliyotokea kwenye Kanisa tangu lilivyozaliwa, la hasha! Lakini nazungumzia Asili ya Kanisa kwa kutazama Uzao na Nafasi yake.

Hebu tutazame mifano michache itakayonisaidia kukuelekeza mambo ambayo ninataka nikuoneshe mtu wa MUNGU, katika mifano hii utaona mambo kadhaa ambayo yatafungua ufahamu wako umuhimu wa kujua Asili ya Kanisa kwa kutazama Uzao na Nafasi yake.

Habari za Wana wa Skewa.

Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo. Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo. Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.  (Matendo 19:13-16)

Sasa lengo kubwa si kukuonesha hadithi hiyo nzima, lakini kuna kipengele ambacho hakipo hapo kwenye hiyo mistari na si kwamba kimesahaulika kwenye hiyo mistari lakini hakipo kabisa,  lakini nataka nikitumie hicho hicho kipengele ambacho ukiangalia kwa undani hakipo ndicho nataka nitumie kukufundisha hapo. Kipengele chenyewe ni MAJIBU YA WANA WA SKEWA.

Friday, April 11, 2014

COUPLES SEMINAR COUPLES SEMINAR It is here again......


You are all Welcome to  the Couples Seminar (Semina ya Ndoa) to be held in Dar es Salaam

 

When: 21st April 2014 -Easter Monday


Time: 9:30 a.m to 5.00 p.m
 
 
Where: Mirado Hall, Sinza Makaburini, Dar es Salaam, Tanzania

Theme: Successful Marriage, Successful Family, Successful Nation


Entrace Fee: 35,000/= Couples

                     20,000/= Singles

Speakers : Dr Elly
                   Eng. Lucas and Happiness Mgalula
                   George & Sayuni Mngodo

Event Host: Pastor Yared and Matilda Dondo
                      Mr and Mrs Harris Kapiga

What to expect: After having an interview with one of  the seminar hosts, he revealed that he expects a major transformation to all the couples who will attend.

Main Topic: The main topic for the day is scheduled to be Romance and Sex in Marriages which has been one of the key concerns in today's marriages.


Food and Soft Drinks will be served

Wednesday, April 9, 2014

Nilichojifunza kuelekea Maadhimisho ya Miaka 75 ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God(TAG)


Kanisa la Tanzania Assemblies of God liko katika maandalizi ya kusherekea miaka 75 tangia kuanzishwa kwake. Kanisa hilo lilianzishwa mwaka 1939 na Mmishenari aitwaye Paul Deer ambaye alitokea katika uamsho wa Kipentekoste wa Azusa uliotokea kule Los Angeles, California nchini Marekani miaka ya 1906 hadi 1915.


Askofu Emmanuel Lazaro, Askofu wa Kwanza wa Kanisa la TAG


Paul Deer alifikia mkoani Mbeya ndipo akaanzisha Kanisa la TAG akishiriakiana na watu wengine.

Maadhimisho hayo yamesaidia tukaweza kujua mambo muhimu sana ambayo Wakristo wenzetu waliyafanya ili kuhakikisha kanisa linakuwepo na kuenea duniani.

Jambo kumbwa sana lililonifanya nijifikirie mara mbilimbili juu ya maisha yangu ya Ukristo ni jinsi wamishenari hao walivyotembea miles 120 ili tu kuhakikisha sehemu mbalimbali za Afrika zinapata Injili ya Kweli ya Yesu Kristo.
 
Askofu Dr Barnabas Mtokambali, Askofu Mkuu wa sasa wa Kanisa la TAG

Sasa nikiangalia kizazi cha sasa tulivyozoea kupanda bajaji, pikipiki na tax katika umbali mfupi ilimradi tu tusitembee maana ni wavivu watoto wa dotcom, je kweli tunaweze kutembea mpaka Tandahimba kupeleka Injili ya Yesu Kristo? Kwani hao waliotutangulia walisukumwa na nini hasa? Na sisi tutafanyaje basi ndugu yangu ili tuweze kuacha historia ya Injili hapa duniani.

Tujue kwamba kule Mbinguni kutakuwa na taji je kwa unavyojiangalia utavikwa taji kwa jambo gani hasa ulilolifanya la KUJITOA HASWAA kwa ajili ya Injili………….Tujichunguze na kumuomba Mungu atusaidie ni wapi anataka tumtumikie ili na sisi tubaki katika Historia kwamba tulifanya a,b,c kwa ajili ya Injili.

Kwa kifupi Maadhimisho yatafikia Kilele mwezi wa saba kule Mbeya.

 

Endelea kutembelea Rejoice and Rejoice Blog mambo mazuri yanakuja

 

Ubarikiwe na Bwana Yesu Kristo, Amen

Thursday, April 3, 2014

One on One with Moji Olusoji Nigerian Gospel Artiste a Winner of Africa Gospel Music Awards (AGMA) 2013

Rejoice and Rejoice Blog is going Global....
 
We are privileged to have an Interview with Moji Olusoji a Winner of Africa Gospel Music Award (AGMA) 2013.


Moji Olusoji Nigerian Gospel Artiste

Blogger: Praise the Lord may I know who are you? Your names and Nick Names if any

 Moji: In summary I am a wife-mother-Geoscientist-Gospel Artiste and I love the Lord deeply. I am married to Kayode Olusoji (The Gidi Gan Master) and by the grace of God blessed with 3 lovely boys. I am from Ondo State in Nigeria. Well people call me Moji and my hubby calls me Moj and sometimes Mj.
Blogger: Wow Thanks, When did you receive Christ

Moji: I received Christ sometimes in the 80’s. Well for me it was a decision I took over a period of time. I kept confessing my sins over and over again but thank God I am saved by his grace.

Blogger: Amen, What motivated you to be involved in Gospel Music

Moji: My motivation to be involved in gospel music I will say is from the fact that I am convinced this is what God wants me to do. I remember vividly the dream I had back in the 80’s where I was in a big stadium sized auditorium, some Artists had ministered before me and when I came up, the presence of God was all over the place, things began to happen. That for me drives me because I am convinced beyond reasonable doubt that when I sing, I am a minister and people’s lives must not be the same again. There is no other platform to do this for me than gospel, spreading the good news through my music. My passion is raising worshippers to God.
 
Blogger: When did you start and How

Moji: Singing for me started in the 80’s. Over the years I have been consistently involved in several brands, church choirs, groups at different levels both in Nigeria and outside Nigeria. Specifically, in the UK.  But professionally, I started in 2007 as an independent Artiste.


The Poise

Tuesday, April 1, 2014

Mambo ya Msingi Kanisa linayoweza kupata kwa Kujua au Kufahamu Asili yake na Mwalimu Samwel Mkumbo


 Amani ya Kristo iwe pamoja nawe mtu wa Mungu, Karibu katika makala haya yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo ambaye ni Graduate wa Chuo Kikuu Dar es Salaam na alikuwa Coordinator wa Fellowship ya God Kingdom Business (GKB)
 
Mwalimu Samwel Mkumbo
UTANGULIZI...

Lengo kubwa la somo hili ni kutazama ni vitu gani ambavyo kanisa la Tanzania na Ulimwengu kwa ujumla linakosa kwa sababu tu Kanisa halijachukua maamuzi ya kujua Asili yake na namna ambavyo MUNGU analitazama Kanisa.

Na labda niweke wazi jambo hili ya kwamba si azimio kubwa katika Somo hili kusema ASILI ya Kanisa kwa namna ya Historia ya kuzaliwa kwake kwa kutaja miaka au labda matukio ya muhimu, la hasha! Japo tunaweza kuangalia Historia kwa sehemu kidogo tu ikibisi kufanya hivyo ili kujua mambo mengi zaidi.

Maana ninajua wapo wazee wetu wa Imani na wenye kuijua Historia ya Kanisa la Tanzania na Ulimwengu kwa ujumla na wanafundisha hayo hivyo basi Azimio kubwa ndani ya Somo hili ni kutaka Kanisa lijue Asili yake kwa namna ya Uzao na Nafasi yake! Ndio! ASILI YAKE kwa kuangalia UZAO na NAFASI yake.

SEHEMU YA KWANZA

Moja ya jambo ambalo MUNGU analitaka ni sisi watu tuliookoka Kujua Asili yetu ndani ya Asili tuliyokuwa nayo. Yaani inapasa tufahamu kuwa sisi ni kina nani tunatoka wapi na tunakwenda wapi, naam ni watu wa shina na chipukizi gani?

Na mara kadhaa kwenye Biblia Mungu anataka na watumishi wake wanafanya juhudi kutaka kutujulisha asili ya Kanisa, maana tunapoijua asili ya Kanisa kuna mambo ya msingi tunayapata ndani yake na ambayo tusipojua asili ya Kanisa hatuwezi kuyapata, na hayo mambo si kama ni ya ziada kwamba tukiyapata sawa na tukiyakosa sawa, HAPANA! Ni mambo ya MSINGI na ni Muhimu sana Kanisa likafahamu kwa upana wake hasa vijana ambao kesho na keshokutwa ndio watakaokuja kuliongoza na kulilea Kanisa, ndio! Ni muhimu sana sana.

1 Petro 1:18 inasema hivi;

Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;