Monday, January 28, 2013

Mambo yameiva uzinduzi wa Albam “Uko Hapa” ya John Lisu


 

Kama tunalivyokwisha kusikia yule muimbaji wa nyimbo za Injili ambaye nyimbo zake zinawabariki wengi maana kwakweli nyimbo hizo huwa zinashusha wingu la Bwana na kufanya muimbaji aingine triple p nikiwa na maana Patakatifu Pa Patakatifu ambaye si mwingine bali ni John Lisu amesema maandalizi ya kuizindua au kuiweka wakfu Albam yake mpya inayoitwa” Uko Hapa” yanakwenda vizuri sana maana kila kitu kama ukumbi,mapambo ,waimbaji na vinginevyo viko vizuri.


John Lisu aliyasema maneno hayo alipokuwa katika mahojiano na Watangazaji na Ma-blogger wa Kikikristo,mahojiano yaliyofanyika katika kanisa la DPC mwisho wa wiki iliyopita.
John Lisu

John Lisu aliendelea kusema kwamba ana uhakika kwamba uzinduzi huo utakuwa mzuri maana pia hajafanya kama mazoea bali wameomba kumsihi Bwana Yesu ashuke na kuonekana siku hiyo.

Albam hiyo itakuwa na nyimbo kumi na moja (11), anmeiita  “Uko Hapa” kwasababu yeye hajawahi kukaa na kuandika nyimbo hata siku moja bali anazipata akiwa amejitenga akiwa anamuomba Mungu.Kwahiyo Wakristo tuna cha kujifunza hapa kama unataka kumsikia Mungu basi utafute muda ujitenge utamsikia,Halleleya!

Katika Albam hii mpya John Lisu anaupenda sana wimbo wa Fungua Macho,kwasababu ni wimbo wa maombi kwa Mungu.

Kwa kifupi John Lisu alianza kuimba akiwa na miaka 6 na ni mtoto wa Mchungaji,kwahiyo amekulia katika wokovu. Na alikuwa akiimba sana katika mikutano ya baba yake Mchungaji Lisu,tena alikuwa pia akipiga na gitaa. Mungu amempa huduma ya kuwaingiza watu katika uwepo wa Mungu kwa njia ya nyimbo.

John Lisu ana mke aitwaye Nelly Lisu na mbali na kuimba ni Mjasiriamali.
John Lisu na mke wake

Mpaka sasa ana Albam moja ya Jehova Yu Hai ila kuna nyingine ambayo ndio ilikuwa iwe ya kwanza lakini haikutoka na haijulikani sana inaitwa“Tutakaribishwa Kwake aliitoa mwaka 2003.

Uzinduzi wa Albam ya Uko Hapa utafanyika pale CCC –Upanga mkabala na Mzumbe University,Waimbaji wengine watakaohudumu siku hiyo ni Pastor Paul Safari,Glorious Celebrations,The Voice,Bomb Johnson,Next Level Team na wengine. Muda ni kuanzia saa 9 hadi baadaye na Kiingili ni shilingi elfu tano (5000).

WOTE MNAKARIBISHWA

 

 

No comments:

Post a Comment