Wednesday, February 20, 2013

MJUE EDSON MWASABWITE MUIMBAJI MAHIRI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA




Edson Mwasabwite


Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kufanya Interview na Muimbaji wa nyimbo za Injili hapa Tanzania,aliyeimba nyimbo zinazobariki wengi twende tuone anasemaje;
 
Blogger: Naomba majina yako kamili,na je unatumia Jina tofauti la kisanii? Tungependa kulijua pia ili jamii iweze kukutambua kwa urahisi.
Jina langu ni Edson Mwasabwite
 
Blogger:Umeokoka na unaabudu wapi
Ndio,KKKT Kijitonyama
 
Blogger Historia yako kwa Kifupi ya kuimba,yaani ulianzaje na wapi?
Tangia utoto,sana Sunday School Mbeya-Rungwe,UWAKI-Umoja wa Watoto wa Kikristo,alivyoanza kujitambua akagundua ana kipaji cha uimbaji.
 
Blogger:Katika kuimba kwako je umeshatoa Album au single yoyote? Itaje ina nyimbo ngapi?
Ninayo moja iko katika Audio Cassete,CD,VCD & DVD,Inaitwa ni kwa Neema na Rehema,ina nyimbo nane ,ila ninaandaa Albam ya pili ndio anaiandaa


Blogger: Wimbo unaoupenda katika nyimbo zako
NI KWA NEEMA NA REHEMA
 
 
 
 
 



Blogger:Ni kwanini unaupenda huo wimbo/nyimbo
Kwasababu hakutegemea kama atafika alipo ni kwa neema tu na rehema,na pia ameishi maisha magumu maana aliachwa Yatima. Hii ni historia ya maisha yangu. Wokovu wenyewe ni kwa neema akiangalia vijana wengine yeye yuko salama zaidi. Amen
 
Blogger:Nani anasambaza kazi zako? Je anakusaidia vizuri?
UMOJA AUDIO VISUAL
 
Blogger:Kuna mafanikio gani umeyapata katika kuimba kwako nyimbo za Injili
Mafanikio yapo,japo kwa mtu mwingine yanaweza kuonekana kama sifuri ila mafanikio inategemea na huyo mtu yuko katika nafasi au ngazi gani. Ingawa ndio nimeanza naona mafanikio,namshukuru Mungu.
 
Blogger:Umekutana na changamoto gani katika safari yako ya kuimba
Ndio,hasa mtu anapoanza kuimba maana kuna mtu anataka kufanya ila unakuta fedha mara nyingine inakuwa ni kikwazo ili kuweza kuiweka uimbaji wako katika viwango vya juu.pili, watu wengine wanakushauri vibaya kwa makusudi ili uanguke
tatu,hakuna ushirikiano kwa wale walio wazoefu katika muziki wa Injili,hii imesababisha hata hasara maana huna mwongozo kutoka wazoefu
 
Blogger:Unaonaje Music wa Injili hapa Tanzania?
Wanafanya vizuri ila kuna changamoto ya utaalamu,wasikilizaji na jamii kwa ujumla hawajaupa nafasi sana. Watu wengi wanauchukulia kama burudani tu swala la kuelimisha na kusisimua. Ila tunashuru Mungu kwamba watu wanatuunga mkono. Na ndio maana utakuta nyimbo zinazohit ni zile za kuburudisha zaidi. Kwa Tanzania Mungu ameupa musiki wa Injili Neema.
 
Blogger:Na Unatoa Ujumbe gani kwa waimbaji wa Nyimbo za Injili ambao kwa njia moja au nyingine wanajisahau na kujichanganya na mambo ya dunia hii
Ujumbe wangu kwa waimbaji wenzangu wa nyimbo za Injili,ujue kama unahubiri kwahiyo uwe mfano na wakili,tusiwe kama vibao lakini tusiende huko. Yesu alisema itamfaa nini mtu apate vya dunia na kuikosa mbingu.
 
Blogger:Zaidi ya kuimba ni kitu gani kingine unachofanya
Mfanyabiashara,Mungu amenipa karama hii,kwasasa niko kiutumishi zaidi.
 
Blogger:Je kimaisha je uko wapi? Umeoa au Hujaoa bado? Watoto wangapi?
Niko Dar,sijaoa,namuomba Mungu anipe yule aliyekusudia maana ukosee kujenga nyumba au kurekodi nyimbo utarejea lakini si kuoa naomba Mungu anipe aliyenikusudia. Sina mtoto
 
Blogger:Una Ujumbe gani kwa Waimbaji wa Nyimbo za Injili hapa Tanzania
Tuwe barua mtu akituona ajue kweli huyu anamwimbia Mungu aliye hai. Tujiandae kuimba mbinguni sio kupata sifa hapa duniani

Blogger: Una Ujumbe gani kwa Jamii inayoburidishwa na nyimbo za Injili
Wawe tayari kuelimishwa pia na nyimbo za Injili na si kuburudika tu,wajue tunaishi kwa neema tu wajue Mungu ndio ametupa vyote tulivyo navyo,ambao hawajaokoka wampokee Yesu Kiristo.Vyote tulivyo navyo bila Kiristo ni bure wajiulize wataishi wapi baada ya maisha haya.
 
Edson Rejoice and Rejoice inakutakia Baraka unapoendelea kumtumikia Mungu kwa uaminifu,Mungu akakuinue zaidi na zaidi,Amen

2 comments:

  1. Hongera sana kaka..Nyimbo zako ni nzuri sana na zinagusa maisha yangu kwakweli..katika mkesha wakuingia mwaka huu wa 2013 pale Mikochen B Ilipofika saa 6 tu ulipigwa kwa neema tu na rehema..yani I was so bleced that day..keep it up and remember Jesus is Lord..

    ReplyDelete
  2. Jesus is Lord! Bwana Asifiwe sana.
    Alelujah! Ni ukweli usiofichika kwamba, haijalishi kama ni tajiri au masikini njia ni moja; ukiangalia waliotutangulia utajua kabisa kweli sisi binadamu humu duniani tunaishi kwa neema tu.

    ReplyDelete