Tuesday, June 10, 2014

COME AND DRINK By Pastor Malonga


Pastor Malonga
Opening Scripture John 7:37-39
37 On the last and greatest day of the festival, Jesus stood and said in a loud voice, “Let anyone who is thirsty come to me and drink. 38 Whoever believes in me, as Scripture has said, rivers of living water will flow from within them.”[a] 39 By this he meant the Spirit, whom those who believed in him were later to receive. Up to that time the Spirit had not been given, since Jesus had not yet been glorified.

 

Man composed of three parts;

1.      Body

Outer physical part

You can touch it

You can see with physical eyes

You can feel it

 

2.      Spirit and Soul

Invisible

They work together

You cannot separate them

 

Body will die and separated from Spirit and Soul, but Spirit and Soul cannot be separated they can go together in hell or heaven

 

Our Physical body need water to survive, without water it will dehydrate then die

God has placed in-built sensors in our body when body get dehydrated sensors will send information that there is no water

Just as body needs water for its sustenance similarly Spirit needs Spiritual water for its survival

The Spiritual water is the Holy Spirit

In Verse 37  it says On the last and greatest day of the festival, Jesus stood and said in a loud voice, “Let anyone who is thirsty come to me and drink

Jesus shouted meaning this was an important announcement

Most of us are concentrating on outer man and disregarding the inner man

Feeding and ensuring it looks nice

But I want to tell you today the outer man is temporary but inner man will live forever

Thursday, June 5, 2014

KIVULI cha NAKALA HALISI na Mwalimu Frank Philip

Karibu katika makala haya ya Mafundisho ya Neno la Mungu yanayoletwa kwenu na Mtumishi wa Mungu Frank Philip.


Mwalimu Frank Philip
Katika maisha ya kila siku, tumekuwa na utaratibu wa kutumia KIVULI (copy) cha nakala HALISI (original), kwa matumizi mbali mbali. Mara nyingi, kama sio zote, kivuli cha nakala halisi huweza kutumika kama nakala halisi, hadi kuwe na ulazima wa kuonesha nakala halisi. Kwa mahali pengine, kivuli cha nakala halisi hakiwezi kusaidia kitu, hadi nakala halisi iwepo. Kwa matumizi ya kuanzia (preliminary use), kivuli cha nakala, huwa ni kitu cha msaada; kwa matumizi mengine maalum, kivuli hakimfai mtu kitu. Kwa mfano, huwezi kusafiri na kuingia nchi nyingine kwa kutumia vivuli vya nyaraka za kusafiria. Ndiyo ilivyo hata kwa nchi tunayoiendea baada ya maisha haya, jina lake ni Yerusalem mpya, ushukao kutoka juu. Huwezi kuingia na kivuli cha wokovu, unahitaji vazi halisi. Wokovu ni vazi jeupe, limeoshwa kwa Damu ya Mwana-kondoo. Huwezi kuingia kwenye karamu ya Mwana-kondoo bila vazi halisi.

Sifa moja kubwa ya kivuli cha nakala halisi ni kufanana sana, hasa kwa kubeba taarifa muhimu. Mara nyingi, kama sio zote, kulingana na kinakilishi (photo copier), ni vigumu kubainisha kati ya kivuli na halisi, hadi kwa kutumia vifaa maalum (counterfeit detectors). Bwana Yesu akasema, “acheni msing’oe, msije mkang’oa na ngano pia”! Hii inaonesha mfanano wa hali ya juu kiasi kwamba unaweza kung’oa ngano ukidhani ni gugu. Hivi ndivyo ilivyo hata kwa watu wenye majina ya kuwa hai, kumbe! Wamekufa. Tunadhani tuko na wenzetu, kumbe ni kivuli tu! Dhambi huleta mauti. Atendaye dhambi ni wa Ibilisi, japo anaishi, amekufa. Kweli hatuokolewi kwa matendo ya sharia, ila matendo yako yatakufanya kuwa kivuli au halisi.

Kwa kuelezea jambo hili, Bwana Yesu alitumia mfano wa magugu na ngano (Mathayo 13:24-30). Kwa bahati mbaya, kila shamba la ngano huwa na magugu, tena mengi. Ndipo wanafunzi wake waliposhangaa, kwanini Bwana hakutoa kibali cha kung’oa magugu mara moja? Bwana Yesu alisema “acheni magugu na ngano vikue pamoja”. Angalia neno hili, wakati ngano inakua, na magugu yanakua pia. Laiti kimoja kingekua zaidi ya kingine, ndipo tofauti ingekuwa dhahiri. Lakini ona sasa, kila ngano ikuapo, magugu hukua pia!

Nikitizama mfano wa magugu na ngano najifunza mambo mengi. Kwanza, magugu na ngano yanaweza kuwa kiwakilishi cha jamii ambayo hapa naita “shambani mwa Bwana”, kwa lugha nyepesi, mkusanyiko wa waaminio. Sasa najua shambani mwa bwana ni zaidi ya mkusanyiko wa waaminio, lakini kwa sasa, nachukua kundi la wana wa Mungu kama ngano, na kundi la wana wa giza kama magugu. Ona jambo hili, wote wanakaa katika shamba moja; na Bwana anasema, usiwatenganishe, waache wakue pamoja! Pili, nikaona jambo hili kuwa la msingi sana, Je! Kama ngano ingetengwa kabisa na magugu, tungejuaje sifa za ngano fulani katika kupambana na mazingira yake? Nani angejua tofauti ya ngano bora na mbovu, dhaifu na njema? Kwa maana, kama ngano ikizidiwa na magugu, basi kila mmoja atajua udhaifu wake. Kumbuka imeandikwa “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo” (Ufunuo 21:17). Lakini kukiwepo na ngano ambayo itastahimili magugu, na kuzaa kati ya magugu hayo, na kuonekana kwa dhahiri tofauti yake baina ya magugu, hiyo itakuwa ngano njema na yakusifiwa. Naam, yafaa kutunzwa ghalani, kwa maana ni ngano njema. Kwa ngano dhaifu, mara ipandwapo, hukua ila ilitingwa sana na magugu, na yamkini kushindwa kuzaa, na hatimaye kufanana na magugu kabisa. Ngano dhaifu namna hii, isiyozaa, haina tofauti na gugu, kwa maana imefanana sana, japo kwa jina, inaitwa ngano, hiyo ni gugu tu.

Tuesday, June 3, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa


Karibu tena katika Makala haya yanayoletwa kwenu na Mshauri wako wa Ndoa na Mahusiano, Leo tunaendelea na Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue kuoa au kuolewa , tukimalizia sababu tano zilizobaki
 
Tuendelee

 

6.      Kuambatana na Urafiki kweli

Lengo kubwa la Ndoa ni wanandoa kuwa na mahusiano ya yaliyojengwa ndani ya urafiki na kuambatana

Rafiki ni mtu ambaye mnashirikiana katika mambo mengi, ni mtu unayependa kumuona na kuzungumza naye mambo yako, ni mtu ambaye ukiwa na huzuni utapenda awe wa kwanza kumwambia, ukiwa na furaha pia utamshirikisha furaha yako. Hata ikitokea mmetofautiana na kugombana na rafiki hutajisikia vizuri utatamani tu utafute njia ya kutatua mgogoro na urafiki uendelee.

Na marafiki wengi wa kweli ambao wamekuwa marafiki wa muda mrefu wamepita katika vipindi vingi, kuna kipindi wamegombana, wamekwazana na wamefurahi sana kwa pamoja lakini wameendelea kuchukuliana na dio maana urafiki wao unaendelea.

Hivyohivyo ndoa inapaswa kujegwa katika urafiki wa dhati na wa kweli, ili kuweza kuchukuliana pale mnapopishana

Kwahiyo ukitaka kuingia katika ndoa uwe Tayari kumfanya mwezi wako kuwa Rafiki hapo utafurahi sana katika ndoa, maana utakuwa huru kwa mwenzako, kumtania, kumweleza chochote, na hata kama hujafurahi utamwambia nay eye pia, na pale mnapokwazana kwasababu ni rafiki itakuwa rahisi sana kusulihisha mgogoro. Kwahiyo kijana na binti yangu ingia katika ndoa na mtazamo huu utakusaidia sana

Usije ukamfanya mwenzako baba au mama yako, mama na baba wana nafasi zao tunaziheshimu, mfanye mwezi wako kuwa rafiki, Haleluyaaaaaaaaaaaa

 

Hata Neno katika Mwanzo 2 : 21- 24 “Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,

na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.

Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

 

Mungu aliona ni vyema wana ndoa kuwa Mwili mmoja na kuambatana, hamwezi kuambatana pia kama sio marafiki ndio maana leo tumeona ndoa nyingi wameshindwa kuambata kwasababu mahusiano yao hayana urafiki, Mungu akusaidie wewe unayetegemea kuingia katika ndoa ujifunze hili na wewe uliyeko katika Ndoa basi anza leo kuwa na urafiki na mwezi wako ili muweze kuambatana, yaani mkifanya mambo yenu kwa pamoja

 

7.      Ushirika

Ndoa ni nafasi nzuri sana ya kuweka ushirika katika matendo,yamkini umelelewa katika mazingira ya ubinafsi mpendwa wangu ambapo chako ni chako, hakuna mtu anavaa hata ndala zako, au hata anayegusa kitu chako, sasa ukiingia katika ndoa ujue mambo yatakuwa tofauti, kama Neno la Mwanzo 2: 21-24 Ndoa ni kuambatana inabidi ufungue moyo wako kuwa Tayari kushirikiana na mwenzi wako katika mambo yote, katika huzuni, changamoto, hali ya kupungukiwa, furaha na raha, sio kwa vile leo umeolewa na mwenzako anavitu basi unashirikiana naye akiishiwa tu au wanavyosema wana dotcom akifulia unamkimbia si sawa, hiyo sio ndoa mpendwa. Jiweke Tayari kushirikiana na mwenzako hapo utaona maisha mazuri utakuwa unaimba haleluyaaaa

 

8.      Kusaidiana mahitaji ya kila mmoja

Monday, June 2, 2014

Kenyan Christian leaders oppose polygamy bill


Christian leaders are appealing to President Uhuru Kenyatta not to sign into law a proposed new marriage bill that legalizes polygamy.

 (Date unknown) A Christian wedding in the Wakamba native reserve near Nairobi, Kenya, which was held in a mission church in the reserve. Religion News Service file photo 

Legislators passed the law last week after an intense debate that saw women members of Parliament storm out in protest. The bill’s passage followed an amendment to the existing marriage legislation to allow men to marry as many women as they want. It awaits Kenyatta’s signature to become law.

But the National Council of Churches of Kenya, the Kenya Conference of Catholic Bishops and the Evangelical Alliance of Kenya, have rejected it, saying the law will undermine Christian principles of marriage and family.

The Rev. Peter Karanja, general secretary the Kenyan church council, said the bill demeans women and fails to respect the principle of spouses’ equality in marriage.

Wednesday, May 28, 2014

Mkesha Maalumu kwa Dreamers


DO YOU HAVE A DREAM or Not Clear with Your Dream….

This is for You…

Venue: Victoria Petrol Station (former VCC place of worship)

Time: 9pm to 6am (all night long)

Entry: FREE


Theme: Wake Up and Pursue your Dream

 

Speakers:

Timothy Kyara

Rose Mushi

Luphurise Lema-Mawere

Geofrey Thobias

Stella Mdawah
 

Worship:

The Doxas from Word Alive Centre

The Annointed Voices - tav

Yehovah Nissi Worship Team

 

Dancing Crew:

The Blessed Twin

God's Generation

Friday, May 23, 2014

Kutana na Samwel Mwangu mwandishi wa Habari anayemtumikia Mungu kwa njia ya Uimbaji



Samwel Mwangu mwimbaji wa nyimbo za Injili
 
Blogger: Naomba majina yako kamili,na je unatumia Jina tofauti la kisanii? Tungependa kulijua pia ili jamii iweze kukutambua kwa urahisi.

Mwambaji: Samuel Mwangu

Blogger:Umeokoka na unaabudu wapi


Mwimbaji: Nimeokoka na ninaabudu katika kanisa la TAG, CITY HARVEST, Dar es salaam.

Blogger Historia yako kwa Kifupi ya kuimba,yaani ulianzaje na wapi?

Mwimbaji: Nimezaliwa 1988, katika familia ya kikristo, huduma ya uimbaji nimeanza mwaka 2003 katika kwaya, kanisa la Mission to Unreached church (MUAC), mkoani pwani, mlandizi. Mwaka 2010 Mungu aliniwezesha kuanza kujitegemea katika uimbaji, mpka hivi sasa kwa neema ya Mungu naendelea kutumika.


Blogger:Katika kuimba kwako je umeshatoa Album au single yoyote? Itaje ina nyimbo ngapi?

Mwimbaji: Mpaka hivi sasa nina albam mbili, ya kwanza inaitwa NINAISHI SABABU YA MUNGU nay a pili inaitwa NJOO VILE ULIVYO ( UTAN’GAA KAMA JUA.)

 

Wednesday, May 21, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa


Mpendwa wangu Shalom,
 
Karibu tena katika Makala haya ya Uchumba hadi Ndoa, yanayoletwa kwenu na Washauri Wenu wa Ndoa na Mahusiano.

Wiki mbili zilizopita tuliangalia sababu 10 zisizofaa kuamua kuoa au kuolewa, ambapo tulipata nafasi ya kuchambua mambo mengi na ya muhimu.


Basi leo Karibu tena tuendelee na Somo lingine, Leo tutazungumzia Sababu Kumi(10) zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa;


1.      Ndoa ni Mpango wa Mungu

Mungu ndiye Mwanzilishi wa Ndoa, tunasoma katika Mwanzo 2: 18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Mungu aliona si vema mtu awe peke yake na ndipo akamfanyia msaidizi(MKE) wa kufanana naye. Kwahiyo unaona kabisa Ndoa ilikuwa ni mpango wa Mungu na sio kwamba baba yetu Adamu alijiamulia tu kwa msukumo wake mwenyewe. Na hii muhimu sana kwa Wakristo kujua kwamba Mungu anatuwazia mawazo mema, yeye bila kuombwa na Adamu anaona huyu ngoja nimpatie mwezi wake ambaye anafanana naye, Mungu alijua akimpa ambaye hawafanani itakuwa kasheshe. Mungu ni Mpangaji Mzuri sana kwakweli Uzuri wake haulezeki nikiangalia jinsi amefanya mambo yake huwa namshangaa na kumsifu tu.

Katika maisha yako ya kila siku najua umekuwa na mahitaji mbalimbali ambayo unayapeleka mbele za Mungu kwa njia ya maombi, kwa mfano Kufaulu mitihani, kupata kazi, kupona magonjwa , kupata kazi nakadhalika nakadhalika, Sasa kama umemuomba Mungu akakujibu juu ya hivyo vitu vingine kwanini kwenye swala la Ndoa usimwamini Mungu hivyohivyo.

Kabla ya kupata mwezi na baada ni vizuri kuwa katika hali ya maombi ili mapenzi ya Mungu yatimizwe, ili Mungu akupe mtu yule aliyemkusudia ambaye unafanana naye. Kwasababu ukipata unayefanana nae mtaishi kwa upendo na kuchukuliana.

Kwahiyo ni ombi langu kwako ndugu yangu mpendwa kwamba Mungu akupe neema ya kukaa katika maombi katika hatua yoyoye ambayo uko, iwe hujapata mwenza , au umeshampata au uko ndani ya Ndoa.

Hiyo itakusaidia sana kuwa na maisha ambayo Mungu amekukusudia kwasababu utakuwa unatembea katika mpango wa Mungu


2.      Kuonyesha Upendo wa Mungu kwa Mwenzi wako

Mungu wetu ni Upendo na upendo wake ni wa Agape, yeye alitupenda wakati sisi tuko katika dhambi na wala hatuna chochote ambacho tumempa.

Upendo wa Mungu sio kama ambao baadhi ya watu wanao, hauna masharti, watu wengi wana upendo wa masharti ule wa Nipe Nikupe, nakupenda kwasababu ya Pesa, au nakupenda kwasababu ya najua nitapata upendeleo fulani fulani, na siku hizi imekuwa hatari sana vijana wengi wanaoa au kuolewa na watu kwasababu hao watu wana vitu fulani kama magari, nyumba, hela, au vyeo

Lakini Upendo wa Kweli ni ule wa Mungu ambao hauna masharti, tunapaswa kuingia katika Ndoa ikiwa ni njia nzuri ya kuonyesha Upendo wa Mungu kwa wenzi wetu.

Ndoa ni sehemu sahihi kabisa ya wenzi kuonyesha upendo wa Agape kwa kila mmoja,kumpenda mwenzako akiwa mzima au mgonjwa, akiwa na fedha ua hana, akiwa na cheo au asipokuwa nacho, kumuonyesha mwenzako upendo bila kusubiri kupata chochote kama Mungu na Kristo walivyotupenda kwanza.

 

3.      Kuonyesha Upendo wa Kweli kwa Mwezi wako

Ndoa ni sehemu muhimu sana ya kuonyesha upendo kwa mwezi wako, kwahiyo ni vizuri kuoa  au kuolewa kwa makusudi ya kutaka kuonyesha upendo kwa mwenzi wako

Katika Ndoa kunatakiwa kuonyesha aina tatu za Upendo;

·         Phileo ambao ni ule upendo wa Kimahaba kwa mpenzi wako, kwahiyo unapooa au kuolewa ndugu mpendwa ujue una jukumu la kuonyesha upendo wa kimahaba kwa mwenzi wako

·         Eros ni vizuri kuingia kwenye ndoa kwa shauku ya kutaka kuonyesha upendo wa kimapenzi kwa mwenzako, kuwa Tayari na furaha kwa ajili ya ile zawadi kubwa ya Tendo la Ndoa Mungu aliyoiandaa

·         Agape wanandoa pia wana jukumu la kuonyesha upendo wa Mungu kwa kila mmoja kama nilivyokwisha kuelezea hapo juu

              Kwa hiyo Upendo kwa mwenzi wako ni jambo la msingi sana nan i msukumo unaoruhusiwa kufanya maamuzi ya kuingia katika Ndoa, kwahiyo mpendwa kama hujaingia hebu jichunguze je kuna upendo , ni nini  

             Msukumo wako?


4.      Shauku ya kuazisha familia pamoja