Wednesday, May 28, 2014

Mkesha Maalumu kwa Dreamers


DO YOU HAVE A DREAM or Not Clear with Your Dream….

This is for You…

Venue: Victoria Petrol Station (former VCC place of worship)

Time: 9pm to 6am (all night long)

Entry: FREE


Theme: Wake Up and Pursue your Dream

 

Speakers:

Timothy Kyara

Rose Mushi

Luphurise Lema-Mawere

Geofrey Thobias

Stella Mdawah
 

Worship:

The Doxas from Word Alive Centre

The Annointed Voices - tav

Yehovah Nissi Worship Team

 

Dancing Crew:

The Blessed Twin

God's Generation

Friday, May 23, 2014

Kutana na Samwel Mwangu mwandishi wa Habari anayemtumikia Mungu kwa njia ya Uimbaji



Samwel Mwangu mwimbaji wa nyimbo za Injili
 
Blogger: Naomba majina yako kamili,na je unatumia Jina tofauti la kisanii? Tungependa kulijua pia ili jamii iweze kukutambua kwa urahisi.

Mwambaji: Samuel Mwangu

Blogger:Umeokoka na unaabudu wapi


Mwimbaji: Nimeokoka na ninaabudu katika kanisa la TAG, CITY HARVEST, Dar es salaam.

Blogger Historia yako kwa Kifupi ya kuimba,yaani ulianzaje na wapi?

Mwimbaji: Nimezaliwa 1988, katika familia ya kikristo, huduma ya uimbaji nimeanza mwaka 2003 katika kwaya, kanisa la Mission to Unreached church (MUAC), mkoani pwani, mlandizi. Mwaka 2010 Mungu aliniwezesha kuanza kujitegemea katika uimbaji, mpka hivi sasa kwa neema ya Mungu naendelea kutumika.


Blogger:Katika kuimba kwako je umeshatoa Album au single yoyote? Itaje ina nyimbo ngapi?

Mwimbaji: Mpaka hivi sasa nina albam mbili, ya kwanza inaitwa NINAISHI SABABU YA MUNGU nay a pili inaitwa NJOO VILE ULIVYO ( UTAN’GAA KAMA JUA.)

 

Wednesday, May 21, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa


Mpendwa wangu Shalom,
 
Karibu tena katika Makala haya ya Uchumba hadi Ndoa, yanayoletwa kwenu na Washauri Wenu wa Ndoa na Mahusiano.

Wiki mbili zilizopita tuliangalia sababu 10 zisizofaa kuamua kuoa au kuolewa, ambapo tulipata nafasi ya kuchambua mambo mengi na ya muhimu.


Basi leo Karibu tena tuendelee na Somo lingine, Leo tutazungumzia Sababu Kumi(10) zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa;


1.      Ndoa ni Mpango wa Mungu

Mungu ndiye Mwanzilishi wa Ndoa, tunasoma katika Mwanzo 2: 18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Mungu aliona si vema mtu awe peke yake na ndipo akamfanyia msaidizi(MKE) wa kufanana naye. Kwahiyo unaona kabisa Ndoa ilikuwa ni mpango wa Mungu na sio kwamba baba yetu Adamu alijiamulia tu kwa msukumo wake mwenyewe. Na hii muhimu sana kwa Wakristo kujua kwamba Mungu anatuwazia mawazo mema, yeye bila kuombwa na Adamu anaona huyu ngoja nimpatie mwezi wake ambaye anafanana naye, Mungu alijua akimpa ambaye hawafanani itakuwa kasheshe. Mungu ni Mpangaji Mzuri sana kwakweli Uzuri wake haulezeki nikiangalia jinsi amefanya mambo yake huwa namshangaa na kumsifu tu.

Katika maisha yako ya kila siku najua umekuwa na mahitaji mbalimbali ambayo unayapeleka mbele za Mungu kwa njia ya maombi, kwa mfano Kufaulu mitihani, kupata kazi, kupona magonjwa , kupata kazi nakadhalika nakadhalika, Sasa kama umemuomba Mungu akakujibu juu ya hivyo vitu vingine kwanini kwenye swala la Ndoa usimwamini Mungu hivyohivyo.

Kabla ya kupata mwezi na baada ni vizuri kuwa katika hali ya maombi ili mapenzi ya Mungu yatimizwe, ili Mungu akupe mtu yule aliyemkusudia ambaye unafanana naye. Kwasababu ukipata unayefanana nae mtaishi kwa upendo na kuchukuliana.

Kwahiyo ni ombi langu kwako ndugu yangu mpendwa kwamba Mungu akupe neema ya kukaa katika maombi katika hatua yoyoye ambayo uko, iwe hujapata mwenza , au umeshampata au uko ndani ya Ndoa.

Hiyo itakusaidia sana kuwa na maisha ambayo Mungu amekukusudia kwasababu utakuwa unatembea katika mpango wa Mungu


2.      Kuonyesha Upendo wa Mungu kwa Mwenzi wako

Mungu wetu ni Upendo na upendo wake ni wa Agape, yeye alitupenda wakati sisi tuko katika dhambi na wala hatuna chochote ambacho tumempa.

Upendo wa Mungu sio kama ambao baadhi ya watu wanao, hauna masharti, watu wengi wana upendo wa masharti ule wa Nipe Nikupe, nakupenda kwasababu ya Pesa, au nakupenda kwasababu ya najua nitapata upendeleo fulani fulani, na siku hizi imekuwa hatari sana vijana wengi wanaoa au kuolewa na watu kwasababu hao watu wana vitu fulani kama magari, nyumba, hela, au vyeo

Lakini Upendo wa Kweli ni ule wa Mungu ambao hauna masharti, tunapaswa kuingia katika Ndoa ikiwa ni njia nzuri ya kuonyesha Upendo wa Mungu kwa wenzi wetu.

Ndoa ni sehemu sahihi kabisa ya wenzi kuonyesha upendo wa Agape kwa kila mmoja,kumpenda mwenzako akiwa mzima au mgonjwa, akiwa na fedha ua hana, akiwa na cheo au asipokuwa nacho, kumuonyesha mwenzako upendo bila kusubiri kupata chochote kama Mungu na Kristo walivyotupenda kwanza.

 

3.      Kuonyesha Upendo wa Kweli kwa Mwezi wako

Ndoa ni sehemu muhimu sana ya kuonyesha upendo kwa mwezi wako, kwahiyo ni vizuri kuoa  au kuolewa kwa makusudi ya kutaka kuonyesha upendo kwa mwenzi wako

Katika Ndoa kunatakiwa kuonyesha aina tatu za Upendo;

·         Phileo ambao ni ule upendo wa Kimahaba kwa mpenzi wako, kwahiyo unapooa au kuolewa ndugu mpendwa ujue una jukumu la kuonyesha upendo wa kimahaba kwa mwenzi wako

·         Eros ni vizuri kuingia kwenye ndoa kwa shauku ya kutaka kuonyesha upendo wa kimapenzi kwa mwenzako, kuwa Tayari na furaha kwa ajili ya ile zawadi kubwa ya Tendo la Ndoa Mungu aliyoiandaa

·         Agape wanandoa pia wana jukumu la kuonyesha upendo wa Mungu kwa kila mmoja kama nilivyokwisha kuelezea hapo juu

              Kwa hiyo Upendo kwa mwenzi wako ni jambo la msingi sana nan i msukumo unaoruhusiwa kufanya maamuzi ya kuingia katika Ndoa, kwahiyo mpendwa kama hujaingia hebu jichunguze je kuna upendo , ni nini  

             Msukumo wako?


4.      Shauku ya kuazisha familia pamoja

Monday, May 19, 2014

Kongomano la Mwanamke wa Thamani lawa Baraka kwa Wanawake wa Moshi


Kongomano la Mwanamke wa Thamani lililofanyika Moshi mjini, lilimalizika wiki iliyopita likiwaacha wanawake wengi wakiwa wamepata maarifa ya Neno la Mungu na kufunguliwa.


Pastor Neema Shoo mwandaaji wa Kongomano la Mwanamke wa Thamani akifungua rasmi Kongomano hilo
Upendo Kilahiro alikuwepo akimsifu na kumwabudu Bwana Yesu

Watu wakisifu na Kuabudu
 
 
Kongomano hilo liliandaliwa na Pastor Neema Shoo ambaye alifungua na utangulizi kutoka  Mithali 31:1 alisema mwanamke au mke mwema nani awezaye kumuona nikaonyesha kipo kitu ndani ya mwanamke ambacho ni cha thamani 

Mambo manne yaliyofichika ndani ya Mwanamke             

1. Hekima Ayubu 28:18b naam Kima cha Hekima chapita marijani, Kama hekima inapita marijani basi na Mithali 31:1 inasema mwanamke mwema uthamani wake unapita marijani basi hicho cha thamani ndani ya mwanamke ni Hekima       Mithali 14:1 inaonyesha ukiwa na hekima unajenga nyumba yako bali mpumbavu anaibomoa                                                                   

2. Ufahamu kilichofichika ndani ya mwanamke ni ufahamu Ufahamu ni uwezo wa kupambanua jema/baya.  Ufahamu ni Akili Mwanamke mpumbavu asiye na akili hubomoa nyumba kwa mikono yake ukiwa na Akili utajenga utajua nini nifanye wapi na saa ngapi kwalugha nyepesi Utajitambua.                                         



Pastor Neema akitambulisha Mchungaji wake na Baba na Mama wa kiroho Pastor Dickson Mtalitinya na Mke wake pia alifundish​a

Wednesday, May 14, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Usioe au Kuolewa kwa msukumo wa Sababu hizi kumi zisizofaa


 
Habari mpendwa wangu, Karibu tena wiki hii nyingine nzuri Mungu ametupa tuzungumze na kushauriana

Leo tunaendelea na somo letu zuri tuliloanza wiki iliyopita la Usioe au Usiolewe kwa Msukumo wa Sababu hizi Kumi zisizofaa

Halleluya nasikia furaha sana kupata kibali cha kuzungumza na wewe siku ya leo.

 

Haya tuendelee na zile sababu tano zingine;

 

6.      Hofu ya kujitegemea

Kuna watu wengine ni tegemezi sana kwa wazazi wao,utegemezi huu unaweza ukawa umesababishwa na malezi wazazi waliwalea au yeye mwenyewe tu ni mvivu.

Utakuta mzazi anamfanyia mtoto kila kitu, atamtafutia chuo, atampeleka chuo, atamtafutia kazi, atamtafutia kiwanja,kupikiwa, kufuliwa etc,yaani mtoto anafanyiwa kila kitu kiasi kwamba yeye mwenyewe hana nafasi ya kuwaza na kufanya vitu peke yake. Sasa hapo pia inategemea na mtoto mwenyewe kama anapenda hiyo hali ndio atabweteka hivyohivyo.

Sasa basi akiona amekaa kwao na umri unaenda sana na wazazi labda wanamshauri apange nyumba na kujitegemea yeye anapata woga kwasababu alizoea kufanyiwa kila kitu ili kukwepa hayo anaamua aolewe au aoe na yeyote anayejitokeza ili tu apate pa kutegemea.

Sasa ndugu yangu kama umemuoa mtu au umeolewa na mtu kwasababu ya huo woga unafikiri kweli utaiweza ndoa, na je huyo uliyemtegemea akashindwa kufikia hayo matarajio yako ya utegemezi si utakimbia, nakuomba leo badili mtazamo usichukua uamuzi wa kuingia kwenye ndoa kama sehemu ya kumtegemea mwenzio akufanyie fanyie, badilika leo ndugu yangu, kuolewa ni kuzuri pale tu panapofanyika vile Mungu anataka na kama nilivyosema mwanzo kuna sababu nzuri tu za kuoa au kuolewa lakini sio hofu ya kujitegemea.

 

7.      Hofu ya kumuumiza mwenzako

 

Inawezekana ulikuwa kwenye mahusiano ya uchumba, lakini muda ulivyoendelea ukaona kwamba huwezi tena kuendelea na huo uhusiano inawezekana kwa sababu nzuri tu

Sasa labda ukiangalia muda ambao mlikaa katika huo uhusiano, mambo mliyoahidiana na kufanya pamoja, labda jinsi jamii inavyowatambua, ukaingiwa na hofu kwamba kwakweli sitaweza kumwambia huyu kaka au dada kwamba siwezi kumuoa au kuolewa naye kwasababu nitamuumiza sana. Matokeo yake unamuoa au unaolewa na mtu ambaye kiukweli hukupenda ila ni kwasababu uliogopa kumuumiza.

Sasa vile vitu vilivyokusababisha utake kufanya uamuzi wa kuachana nae na wewe ukashindwa kwasababu uliogopa kumuumiza, ujue kwenye Ndoa ndio utaviona vizuri sana tena clear, sasa sijui utamlaumu nani unaanza kukosa raha na mwisho kama hutakuwa makini na Mungu kuingilia kati hiyo ndoa inaweza kuvunjika kabisaa.

Au mwingine anaamua kabisa kumwambia mwenzake kwamba kutokana na jinsi huu uhusiano unavyoenda naona tuvunje kabla hatujaenda kupata matatizo katika ndoa, sasa mwingine hasa wakina dada Analia hapo mawiki na mawiki, na mwingine anatishia kujiua, sasa mkaka akiona hivyo anaogopa kwamba mwenzake atapoteza maisha kwasababu yake kwahiyo analazimika kuendelea na mahusiano hadi ndoa.

Je unategemea akimuoa huyo aliyetishia kujiua na bado ulikuwa na sababu za msingi za kuvunja uhusiano unafikiri maisha ya ndoa yatakuwaje? Hebu tafakari

Nakumbuka kuna kijana aliniambiaga namuoa fulani kwasababu unajua nimekaa nae miaka mingi sasa nimempotezea muda japo simpendi lakini namuonea Huruma,hiyo si sawa bora uchumba uvunjike kwa machozi kuliko Ndoa jamani naomba kusisitiza, Haleluya bado unanipenda jamani maana kuna watu wanapenda kung`ang`ania wee kama kakukataa jamani sio mwisho wa Safari na wala hutakufa kwa kumkosa tena baadae ukijam kutafakari  kwanini nilikuwa napoteza muda kwa mtu kama huyu utajicheka sanaaaaa cause they don’t deserve you, Wewe ni mtoto wa Mfalme Bwana, Ambassador of Christ why worries enhee! Aminaaaa!

Tuesday, May 13, 2014

When the Little is Much by Pastor Yared Dondo


Pastor Yared Dondo
Lead Pastor,City Harvest Church
Opening Scripture 1 King 17 : 8-16

 “And the word of the Lord came unto him, saying,

 

9 Arise, get thee to Zarephath, which belongeth to Zidon, and dwell there: behold, I have commanded a widow woman there to sustain thee.

 

10 So he arose and went to Zarephath. And when he came to the gate of the city, behold, the widow woman was there gathering of sticks: and he called to her, and said, Fetch me, I pray thee, a little water in a vessel, that I may drink.

 

11 And as she was going to fetch it, he called to her, and said, Bring me, I pray thee, a morsel of bread in thine hand.

 

12 And she said, As the Lord thy God liveth, I have not a cake, but an handful of meal in a barrel, and a little oil in a cruse: and, behold, I am gathering two sticks, that I may go in and dress it for me and my son, that we may eat it, and die.

 

13 And Elijah said unto her, Fear not; go and do as thou hast said: but make me thereof a little cake first, and bring it unto me, and after make for thee and for thy son.

 

14 For thus saith the Lord God of Israel, The barrel of meal shall not waste, neither shall the cruse of oil fail, until the day that the Lord sendeth rain upon the earth.

 

15 And she went and did according to the saying of Elijah: and she, and he, and her house, did eat many days.

 

16 And the barrel of meal wasted not, neither did the cruse of oil fail, according to the word of the Lord, which he spake by Elijah.”

 

When Elijah request a help from a widow she replied that have nothing but a handful meal in a barrel and little oil in a cruse.

May be there is someone here who think he has little but I want to assure you God has different plan, the little you have can be much in the Kingdom of God

If God want to do something is doesn’t matter what you have, whether it is much or little, educated or not,rich or poor, ministry accepted or rejected, he will fulfill his word regardless of who is standing.

In the above story the country was devastated , there are several things that we can learn from this story;

1.      Poverty

The country was in Poverty.

Sometimes we complained that we are poor but we are not fair because our condition is better compared to others.

Some they don’t have place to live, the whole family( father, mother, grandmother, grandfather and kids) are working as servants to rich people

Elijah was poor even the brook that he depended for water dried. He has nothing.

As he was speaking to God, God told him to go to Zeraphat to meet a widow who will feed him.

In Verse  9 Arise, get thee to Zarephath, which belongeth to Zidon, and dwell there: behold, I have commanded a widow woman there to sustain thee.

In those days widows where poor than other people but still God commanded him to go widow.

The widow has nothing and she has given up with her life, she was waiting to die

She believes in God but has no hope to live again.

To believe in God is not sufficient we have to put into action what we Believe

 

2.      Promise

Thursday, May 8, 2014

Kongomano Kubwa la Mwanamke wa Thamani kufanyika mjini Moshi

 

 
Wote Mnakaribishwa Katika Kongomano Kubwa La Mwanamke wa Thamani litakalofanyika Moshi mjini.
 
Mada:  Uthamani wa Mwanamke
            Uhusiano wa Mungu na Mwanamke
 
Wahubiri: Pastor Neema Shoo -Host
                 Pastor Lilian Ndegi
                 Pastor Dickson Mtalitinya- MTBC Moshi
 
Lini: Tarehe 10/ 05/2014 siku ya Jumamosi kuanzia saa 4 Asubuhi hadi saa 9 Mchana
 
Wapi: Ukumbi wa Lutheran Bookshop Stand ya Moshi Mjini
 
Waimbaji: Upendo Kilahiro
                MTBC Praise Team
 
Nikiongea na mwandaaji wa Kongomano hilo Pastor Neema Shoo, amesema kwamba wanawake watakaohudhuria Kongomano hilo wategee Kufunguliwa na Kupata Maarifa ya Neno la Mungu, hawataondoka kama walivyokuja, Amen!
 
Kwakweli mwanamke mwenzangu usikose maana vitu Mungu ameweka ndani ya hawa watumishi vitakupeleka kiwango kingine kabisa.
Kwa ninavyomjua Pastor Lilian Ndegi lazima wanawake wa Moshi wapate urejesho.... Haleluyaaaaaa