Monday, October 22, 2012

Kutana na Queen Mchomvu mwimbaji wa nyimbo za Injili


QUEEN MCHOMVU ....Gospel Singer

Queen Mchomvu
 

Wiki hii nimepata nafasi ya kuonana na mwimbaji wa Injili aitwaye Queen Mchomvu

Kwakweli jinsi tulivyokutana namshukuru Mungu tu aliniwezesha tunavyoendelea na mazungumzo utajua ni kwanini nasema hivyo.

Mazungumzo yetu yalikuwa face to face au uso kwa uso na yalikuwa hivi;

Blogger: Bwana Yesu asifiwe dada

Queen: Amen

Blogger: Wewe ndio ulikuwa unaimba pale mbele enhee

Queen; Ndio

Blogger: Unaabudu wapi?

Queen: EAGT City Center na nimeokoka

Blogger: Amen

Blogger:Una album ngapi:Album 4 ,2 zimetoka sokoni na video zake,2 ziko njiani,album zenyewe hizo hapo?

1.      Jehovah Masiah

2.      Maiti yaweza kuokoka

3.      Nashangaa

4.      Kibao kitegeuka

Blogger: Kwanini umeimba Maiti yaweza kuokoka?

Queen:Kutokana na experince niliyoipata tunavyokwenda kushuhudia watu wengine wanakataa wanasema hakuna kuokoka duniani tutaokoka tukishakufa,ndio nikatoa huu wimbo kwamba kuokoka ni hapa hapa duniani maana maiti haiwezi kamwe kuokoka tukisha kufa ni hukumu hakuna wokovu.

Blogger: Historia yako kwa Kifupi ya kuimba

Queen:Tangia mtoto mdogo sana,maana kwanza nimezaliwa katika familia ya waimbaji baba na mama pia ni waimbaji,hata kukutana kwao walikutana katika kwaya wakachumbiana na kuaoana kwahiyo unaweza kuona wameniambukiza Roho ya uimbaji?

Blogger: Weee wewe ndio Queen wa Sunday School ya Temeke? Mamaa Jamani kweli Mungu wa ajabu maana nilikuwa najiuliza uko wapi nakumbuka sana ulivyokuwa mtoto mdogo sana ukiimba kwa ujasiri mkumbwa sana mbele za watu ,sauti nzuri ,ulikuwa saa ingine unawekwa hata juu ya kiti ili watu wakuone yaani Mungu wa ajabu ametukutanisha tena.

Blogger: Wimbo unaoupenda

Queen:  “Njooni Tumwabudu” Kwasababu huu wimbo niliupata siku niliyokuwa nakwenda kurekodi niliupata pale kwasababu huko nyuma mtu aliyekuwa anitolee album yangu akanitapeli wala hakunifanyia kazi tena,ndio nikakutana na mtu akajitolea kurekodi kwa gharama sawa na bure,kwakweli nilijua ni Mungu na ndio nikaimba wimbo huu.

Blogger:Unaonaje Music wa Injili hapa Tanzania?

Queen: Kwakweli umepiga hatua sana na kwasasa una funs (washabiki) wengi sana tena wengine hata sio wa Imani yetu,kwahiyo tunamshukuru Mungu

Blogger:Unatoa Ujumbe gani kwa waimbaji wa Nyimbo za Injili ambao kwa njia moja au nyingine wanajisahau na kujichanganya na mambo ya dunia hii

Queen: Kwakweli inasikitisha maana wanatukanisha Jina la Mungu maana wao sio waimbaji tu ni watumishi wa Mungu,sasa wanavyojichanganya wanafanya waimbaji wainjili waonekane kwamba ni wasanii tu wakati ni watumishi wa Mungu

Queen akiwa amepozi

Blogger:Zaidi ya kuimba ni kitu gani kingine unafanya

Queen: Mimi ni Professional Hair Dresser nimesomea kabisa na nina Saloon,pia ni mpambaji wa shughuli mbalimbali

Blogger:Ok Maisha Mengine Je ninayopenda kusikia?

Queen: Ha ha Haa Nina niko single na nina mtoto wa kiume anaitwa Prince ana miaka 11

Blogger: Hongera kwa Kukuza mpendwa

Blogger:Ujumbe kwa Waimbaji wa Nyimbo za Injili

Queen:Tuwe na Umoja na kama tumeamua kumuimbia Mungu basi tufanye kwa kumaanisha bila usanii wowote,maana Neno la Mungu linasema

Blogger:Ujumbe kwa Jamii

Queen:Naomba Jamii ituombee sana maana kwakweli kazi ni ngumu sana

Blogger: Amina,Asante sana Queen ,Mungu Akubariki nakutakia siku njema na utumishi mwema!
 
Ukihitaji Kazi zake zinasambazwa na GMC
 

 

 

 

2 comments: