Tuesday, December 6, 2016

S'fiso Ncwane Hatunaye Tena


Tasnia ya Muziki wa Injili imempoteza mwimbaji wa nyimbo za
Injili kutoka Afrika ya Kusini, S'fiso Ncwane. Taarifa kutoka Afrika ya Kusini zinasema S'fiso alifariki jana siku ya jumatatu asubuhi
kutokana na matatizo ya figo, ikiwa ni muda mfupi baada ya
kukimbizwa hospitali kutokana na kulalamika kujisikia kuumwa.

Ncwane ambaye alikuwa akihudumu kwenye tamasha Limpopo
wikiendi iliyopita alianza kulalamika kujisikia kuumwa na kisha
akakimbizwa hospitali mpaka pale umauti ulipomfika, ikiwa ni
taarifa kutoka kwa msemaji wa familia Sipho Makhabane.

Pamoja na kushiriki katika tamasha hilo huko Limpopo, S'fiso
hakuweza kumaliza kuhudumu baada ya kujisikia kuumwa na
kupelekwa hospitali ya Life Fourways



No comments:

Post a Comment