Friday, May 24, 2013

Usikate Tamaa Songa Mbele


Usikate Tamaa
Nawasalimia katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo,

Leo nina ujumbe mfupi kwako wewe ambaye una mzigo mzitoo  sana,umelia sana ,umekata tamaa,labda huna school fees ya watoto,au hujabahatika kupata mtoto,au hujapata kazi,au watu hawakupendi wamekuzushia mambo mabaya,au unaumwa ugonjwa ambao Daktari amesema kwamba hakuna tiba,au unatamani kuwa na mwezi wako wa maisha na unaona kama  muda umeenda,au una msukosuko katika ndoa mambo sio shwari,au umeachwa mpendwa wangu,au kila uanchofanya hufanikiwi umejaribu kila biashara na kila fursa haufanikiwi kila unachoshika na mkono wako kimezaa mapooza matokeo yake vimekuacha katika madeni, mpendwa natanguliza Pole lakini siku ya leo napenda kukuambia hivi Bwana Yesu alisema katika 1Peter 5: 7 Neno  katika tafsiri ya NIV "Mwekeeni matatizo yenu yote, maana yeye anawatunzeni",hilo jambo ambalo unaliona Zito sana kwako mtwike Yesu na yeye atakutunza na kukupumzisha na masumbuko ya dunia hii.

Yawezekana umelia sana sana umepita vituo mbalimbali vya maombi,nakushauri leo mpendwa tulia kwa Bwana na kama neno linavyosema katika Yohana 14:1 "Yesu aliwaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia". Yawezekana hata umesafiri nchi mbalimbali kwa watumishi wakubwa ukitafuta suluhu ya kilio chako,lakini umejikuta uko palepale..

Usifadhaike mpendwa liko tumaini,mwamini Mungu kwamba atafanya katika wakati ambao hukujua utamshangaa Bwana. Mungu anakwenda kukushangaza (Surprise) nao waliokucheka,waliokata tamaa wakaona kwamba wewe ndio basi au kukukebehi watajua kwamba unamtumikia Bwana Mwenye uwezo kuliko kitu chochote duniani na Mbinguni. Mungu anakwenda kukufunika na utukufu wake. Amen

Tena anasema katika Wafilipi 4:6-7 "Msifadhaike juu ya jambo lo lote; lakini katika kila jambo mjulisheni Mungu haja zenu, kwa kusali na kuomba pamoja na kushu kuru 7. Na amani ya Mungu, ambayo inapita ufahamu wote, italinda mioyo yenu na nia zenu kwa Kristo Yesu"

Unapokuwa katika majaribu usimtafute mwanadamu wa kukusaidia,wengine wanakimbilia wazazi wao na kuamini ndio watakao wasaidia ni kweli nafasi ya mzazi ni kubwa lakini atakupa tumaini la muda ,Mungu ndie mwenye tumaini la kweli na yeye ndio anayekujua kwasababu alikuumba kwahiyo anayo majibu juu ya maisha yako,anayo majibu juu ya afya yako,anayo majibu juu mapito yote unayopitia,Songa mbele mpendwa utayapita tuu,nakuambia utacheka tena mpendwa,utainuliwa,kila kilichokuwa kimeibiwa na Ibilisi katika maisha yako kitarudishwa kwako,Halleluya

Napenda sana haya maneno katika Yakobo 1:2-4 ” Ndugu wapendwa, mnapopatwa na majaribu mbalimbali, yahesabuni kuwa ni furaha tupu. 3 Kwa maana mnafahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu hujenga ustahimilivu. 4 Na ustahimilivu ukimaliza kazi yake mtakuwa wakamilifu pasipo kupungukiwa na cho chote.”

Kwahiyo mpendwa ujue kabisa kwa kila jaribu unalipitia hebu hesabu kwamba ni furaha maana unajengwa,unakwenda kubadilishiwa jina,Mungu anakwenda kukurejeshea heshima yako,inawezekana umekosa kibali ofisini kwako,au umeshushiwa heshima na jamii,lakini hebu leo chukua hatua ya Imani na mimi kwamba ni furaha tu maana Mungu anakwenda kukuvalisha vazi la Sifa,Halleluya,Jina la Bwana Libarikiwe

Naongea na mtu wakati huu,Usikate tamaa,narudia usikate tamaa,maana ukishapita kipindi hiki kama neno linavyosema hutapungukiwa na CHOCHOTE, Amen

 

Kwahiyo sasa nakusihi wewe ambaye unapita katika majaribu futa machozi,simama,tembea songa mbele endelea na safari maana kuanguka sio mwisho wa safari mpendwa wangu.

 

Kwakweli leo nimekuja kukutia moyo tu na kukupa Ujumbe Mzuri kwamba Mwokozi wetu Yesu anaweza na atakuwezesha tena,USIKATE TAMAA,Tumaini lipo

 

Hebu sikiliza wimbo huu wa Martha Mwaipaja

3 comments:

  1. umenigusa mpendwa. ubarikiwe sana kwa ujumbe huu wakuturudishia tumaini kwamba Mungu bado yuko katika kiti chake cha enzi. Najua Mungu hajatuacha japo mwanadamu wakati mwingine huangalia mazingira yake na kutoa hitimisho lakukatisha tamaa lakini najua bado Mungu yu pamoja nasi. isaya 43:1-2, 8-9,

    ReplyDelete
  2. Tumaini bado lipo,Tumaini bado liipo tumaini tumaini bado liipo tumaini bado liipo,huu wimbo kwakweli unanitiaga nguvu sana yakuendelea mbele,Ujumbe unatia nguvu tunamshukuru Roho Mtakatifu kwa kutumia watumishi wake

    ReplyDelete
  3. BARIKIWA,UJUMBE MZURI SANAA

    ReplyDelete