Wednesday, November 16, 2016

KUJAMIIANA, UASHERATI NA USAFI - MCHUNGAJI YARED DONDO, TAG CITY HARVEST CHURCH


Pastor Architect Yared Dondo - TAG City Harvest Church
 Upendo wa Kweli Hungoja – Waebrania. 13:4

Mpango wa Mungu kuhusu kujamiiana unahusisha mwanaume mmoja na mwanamke mmoja walio ndani ya uhusiano wa ndoa. Serikali na dunia kwa ujumla hutumia mamilioni ya fedha kwa kinaitwa “ngono salama”. Hakuna ngono salama zaidi ya iliyo ndani ya mpango wa Mungu!
Tafsiri ya kidunia kuhusu ngono salama haijaegemea kwenye maadili hata kidogo. Mawazo yao ni kuwa: “ikiwa hauwezi kuenenda vyema, basi kuwa mwangalifu”.
Tafsiri ya Mungu wa ngono salama ni kungoja mpaka ndoa.
1 Petro 2:11 “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”

Maadili ya Kibiblia huchekwa, hudharauliwa husemwa ni ya kale na yamepitwa na wakati.
Ninashukuru kwa ajili ya viajana matineja wachache ambao leo wanasema, kuanzia leo na kuendelea, nitangojea mpaka wakati wa ndoa….. nitaishi sawa na mpango wa Mungu….. na watu wazima wanaojitoa tena kuwa wasafi na waaminifu. Tumeliruhusu neno ngono/kujamiiana kuwa neno chafu. Kilichopaswa kuwa taswira njema ya upendo, ndoa na maskani, kwa sasa kinahusishwa na upotovu/ukimwi/ukahaba/usagaji/ngono ya jinsia moja.
Jamii inajifunza kwamba kuna adhabu ya uasherati na uzinzi. Lakini badala ya kurejea kwenye viwango vya Mungu na kutii sheria za Mungu, jamii husema “wacha tuone tunachoweza kufanya kukwepa matokeo ya matendo yetu”
Hapa ndipo hatari iko: ikiwa utaingia kwenye uhusiano wa kimwili kabla ya ndoa:

Hatari 5 za ngono kabla ya ndoa:

1.             Pendo bandia
Mahusiano yaliyojengwa juu ya ngono hayadumu! Mkianza na mambo ya kimwili mtajikuta hata hamvutiani. Hamtakua pamoja kiakili, kihisia au kiroho!
Upo hapo ukiwa hauna kitu isipokuwa malai/krimu iliyochapika na inazeekana ambayo utaitupa pia! Lakini…ikiwa kujamiiana kutaanza baada ya ndoa, sehemu nyingine tatu zitaendelea kukua pia! Hivyo unakuwa na siyo tu mshirika wa kujamiiana, bali pia rafiki bora zaidi anayekupenda.
Upendo wa kweli huvumilia, ni halisi na hauna ubinafsi.
Wasichana, pale mwanaume anaposema “Siwezi kusubiri”, utajua kwamba hakupendi. Pale anaposema “Ikiwa wanipenda kweli, nithibitishie”, chukulia hilo kuwa tusi na umchape kibao cha nguvu kiasi cha ubongo wake kupiga kelele kama kengele za kanisa wakati wa asubuhi yenye baridi!

Hatari za upendo wa bandia..

2.             Madhara kihisia

Mabinti wadogo:
Tafiti zinaonyesha uhusiano wa moja kwa moja baina ya ngono kabla ya ndoa na matatizo binafsi ya kihisia… Kujihisi mkosaji/wasiwasi/kupoteza kujiheshimu
Kujihisi una hatia ndiyo hisia inayoweza kutuharibu zaidi.
Hukukosesha usingizi, amani, furaha, kujithamini na uhusiano wako na Mungu.
Hukuacha umevunjika vunjika, ukiwa hauna uhakika na kutoweza kuzalisha matunda.
Na kisha hupoteza ule “mng’ao” unaoambatana na usafi.
Sikieni haya mabinti, na nitawaambia namna wanaume hufikiri…
…..kuna fumbo fulani kuhusu yasiyojulikana. Kuna kitu fulani cha kuvutia sana kuhusu yasiyojulikana.
Mara tisa kati ya kumi, pale unapojifunua kwa mwanaume, baada ya fumbo kuondoka, naye pia huondoka….atakudondosha kama jiwe la moto! Na haitakuwa kama kuachana kwingine kokote, itakuwa kama kupewa talaka.

3.             Madhara ya Kimwili

Bado mshahara wa dhambi ni mauti!
Kuwa mchafu – uko katika hatari ya magonjwa yasiyo na tiba. Kuna magonjwa saba, nje na ukimwi ambayo hayana tiba na yote yamebeba madhara ya muda mrefu, na yote huenea na huhusiana na kundi la watu walio tayari kufanya ngono nje ya usalama wa ndoa!
Utasema yuko tayari kuwa nami pekee. Usijihakikishie hivyo! Ikiwa wako tayari kufanya ngono nawe, basi wako tayari pia kufanya na wengine, na huenda wamekwisha kufanya hivyo tayari.
Unapolala na mtu, unalala na historia nzima ya ngono ya mtu huyo na KILA MTU ambaye amepata kuwa naye.
Mshahara wa dhambi bado ni mauti.

Hatari ya upendo bandia, madhara ya kimwili na kihisia…

4.             Madhara katika ndoa

Nimewashauri watu ambao wamekuwa wakisema “ni swa kwetu kufanya ngono kwani tunajua tutaoana”. Hapana, si sawa…. Kwa nini?
Kwa kuwa Mungu amesema si sawa…. Nani atakaye kubadili sheria yake? Inawezekana usionane naye!
Kwa wastani, kijana tineja hupenda takribani mara 10 kabla ya kuingia katika ndoa
Hivyo, hata ikiwa umeonana naye, umepunguza nafasi za kuwa na ndoa yenye furaha kwa kuwa umemegua msingi wa uaminifu. Kwenye akili yako, siku zote kutakuwa na lile wazo kuwa mtu uliyeoana naye anauwezo wa kuwa mdanganyifu. Waliweza kufanya dhambi nawe kabla ya ndoa, wanaweza kufanya dhambi dhidi yako sasa baada ya kuoana.

Kisha kuna…

5.             Madhara ya kiroho

Lakini Mchungaji, hauamini kuwa Mungu husamehe? NDIYO, NINAAMINI!
Lakini msamaha na madhara ni mambo mawili tofauti. Huwa tunadhani mambo yote mawili yanaishi kwenye mstari mmoja, kuwa tunapousogolea zaidi msamaha ndivyo tunakuwa mbali na madhara… siyo hivyo!
Daudi alifanya dhambi na Bathsheba na kisha akafanya amauaji…na katika vifungu viwili vya ajabu vya Biblia tunaona msamaha wa hali ya juu ambao Daudi aliomba na kupokea – lakini ngoja niulize, madhara hayakuendelea kuwepo?
Ndiyo. Mungu akasema, “Daudi, utaishi katika bonde la machozi maisha yako yote. Upanga hautaondoka nyumbani mwako”
Alimzika mwanae aliyefariki. Kisha mwanaye mmoja akambaka bintiye. Na Mungu akasema ni matokeo ya moja kwa moja ya dhambi zake.

Namna gani ubakie safi?
1.             Linda ufahamu wako
Mlango wa macho na mlango wa masikio ni muhimu sana…. Ni barabara kuu ya ufahamu.
2 Petro 2:14 “macho yaliyojaa uzinzi”
Wanaume, lindeni macho yenu. Biblia inasema (Zaburi 101:3) “Sitaweka mbele ya macho yangu neno la uovu”. Dai mstari huo
Ayubu alisema “Nilifanya agano na macho yangu, basi nawezaje kumwangalia msichana kwa kumtamani?” jiweke mbali na muziki ambao maudhui yake ni tamaa ya kingono.

2.             Usiatamie dhambi

Ikiwa huwezi kuingia duka la videa na kusalia msafi, usiingie kabisa!
Ikiwa huwezi kuperezi kwenye vituo vya televisheni pasipo kutazama kitu kichafu, basi zima kabisa. Ikiwa hamwezi kuwa peke yenu kwenye gari, basi msikae peke yenu.
“Usiupe mwili nafasi”

3.             Azimia kabla

Fanya maamuzi ya awali kubakia msafi, na kuwa hutaingia kamwe kwenye uhusiano na mtu ambaye hajafanya maazimio kama hayo.
Maneno ya mpumbavu: “Atabadilika mara tutakapooana”
Wewe unasema: “Nimechelewa mno mchungaji” (Tayari nimeshatoa)
Habari njema! Siku moja mwanamke aliletwa kwa Yesu, akiwa ameshikwa akifanya uzinzi. Alitarajia kuhukumiwa, lakini Yesu akamwambia, Sikuhukumu, enenda zako na usifanye dhambi tena!


Huwezi kubadili yaliyopita, lakini mustakabali wako waweza kuwa bila madoa!

No comments:

Post a Comment