Tuesday, November 29, 2016

MSANII WA WIKI - LEMBO JR

LEO KATIKA MSANII WA WIKI - EMMANUEL LEMBO JR

Rejoice Blog: Labda tuanze kwa kujua majina yako kamili na ikiwa unatumia jina tofauti kwenye kazi zako za muziki?

Lembo Jr: Jina langu ni Emmanuel Stephen Lembo, ila katika huduma nafahamika kama Lembo Junior
Lembo Jr

Rejoice Blog: Je, umeokoka? Unaabudu katika kanisa gani?

Lembo Jr: Nimeokoka nampenda Yesu, kwa sasa naabudu NAIYOTH CHURCH - GEITA

Rejoice Blog: Historia yako kwa kifupi ya kuimba, yaani ulianzaje na wapi ulianzia?

Lembo Jr: Naweza sema,nilianzia utotoni sundayschool kids choir...ila kuingia rasmi kwenye tasnia hii mpaka kuanza kusikika kwa medias ni 2007-2008 nikiwa UDOM

Rejoice Blog: Katika kuimba kwako, je, umeshatoa album yoyote? Majina ya albamu?

Lembo Jr: Mpaka sasa niko na 4 albums ila tatu ndizo zajulikana 1.TUTEMBELEE. 2 USIFIE JANGWANI. 3.UWE KILA KITU. 4.WINGU LIMESIMAMA WAPI

Rejoice Blog: Wimbo unaoupenda zaidi kati ya nyimbo zako ni upi?

Lembo Jr: mmmmmmh ni almost nyimbo zote nazipenda maana kila wimbo najua Mungu alinipaje ILA UWE KILA KITU, TUTEMBELEE NA USIFIE JANGWANI ni zaidi

Lembo Jr
Rejoice Blog: Ni kwa sababu gani unaupenda wimbo huo zaidi?

Lembo Jr: Nyimbo zina ushuhuda mkubwa sana sikuzipewa hivi hivi, nilipitishwa sana sanaaaaa

Rejoice Blog: Nani anasambaza na kusimamia kazi zako? Na je, anakusaidia vizuri?

Lembo Jr: Kwa sasa niko na Madam Gisela Malisa, yuko vyema

Rejoice Blog: Ni msanii gani wa muziki wa Injili anayekuvutia na unapenda kufuatilia kazi zake?

Lembo Jr: Sipho Makhabane, Emmanuel Mgogo

Rejoice Blog: Kuna mafanikio gani umeyapata katika kuimba nyimbo za Injili?

Lembo Jr: Yako mengi sana kiroho na kimwili. Kiroho; nimekua nikipokea shuhuda nyingi sana namna nyimbo zangu zimeokoa, zimeponya na kuganga NAFSI zilizokia zimejeruhiwa.  Kimwili kuna kupata kipato ingawa si kikubwa, ila MUNGU ni mwema. Na pia nimepata EXPOSURE kubwa sana ndani na nje ya mipaka ya Afrika
Lembo Jr

Rejoice Blog: Umekutana na changamoto gani katika huduma yako ya uimbaji?

Lembo Jr: Changamoto ni nyingi sanaaaa kiroho na kimwili pia kimwili zaidi ni PESA, nitatizo kikubwa, kiroho vita ni KUBWA sana

Rejoice Blog: Unaonaje muziki wa Injili hapa Tanzania? Na hasa wa aina unayoimba wewe?

Lembo Jr: Muziki huu naona kwa upande wangu uko vyema maana haujaniangusha

Rejoice Blog: Unatoa ujumbe gani kwa waimbaji wa nyimbo za Injili ambao kwa njia moja ama nyingine wanajisahau na kujichanganya na mambo ya dunia hii?

Lembo Jr: Kikubwa ni kurudi kwenye kusudi la MUNGU na kulitumikia Shauri la Bwana

Rejoice Blog: Zaidi ya kuimba ni kitu gani kingine unakifanya?

Lembo Jr: Kitaaluma nina Bachelor Degree ya Public Administration (Shahada ya Sanaa katika Utawala wa Umma), ingawa sijaajiriwa, ninafanya biashara zangu ndogo ndogo

Rejoice Blog: Je, kimaisha uko wapi? Ndoa na watoto vipi?

Lembo Jr: Naishi na familia yangu Geita, niko na mtoto mmoja tu

Rejoice Blog: Una ujumbe gani kwa Waimbaji wa Nyimbo za Injili hapa Tanzania?

Lembo Jr: Ujumbe TUIFANYE KAZI YA MUNGU KWA UNYENYEKEVU MKUU SANA

Rejoice Blog: Na kwa jamii inayoguswa na kuburudishwa na nyimbo za Injili una ujumbe gani kwao?

Lembo Jr: Waendelee kutusapoti kwa hali, mali na maombi.

Rejoice Blog: Ahsante sana Lembo Jr kwa muda wako, Mungu akubariki na kukuinua unavyoendelea kumtumikia kwa uaminifu

Lembo Jr: Nami NIWASHUKURU SANA SANA KWA MUDA WENU NA KUJALI KWENU MUNGU AWABARIKI SANAAAA

Huyo ndiye Emmanuel Stephen Lembo a.k.a Lembo Junior ambaye umepata kumfahamu zaidi kupitia Msanii wetu wa Wiki. Ukitaka kuendelea kufuatilia habari zake na kazi yake ya huduma, mpate kwa njia zifuatazo:

Emmanuel Lembo Jr:
Instagram: @lembojr
Facebook: Lembo Jr Emmanuel

~~~ UMEBARIKIWA! ~~~


No comments:

Post a Comment