Wednesday, January 11, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 11

SIKU YA 11 - 11/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA


Isaya 54:2 Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako.

Isaya 26:15 Umeliongeza hilo taifa, Bwana, umeliongeza taifa; wewe umetukuzwa, umeipanua mipaka yote ya nchi hii.

YABESI ALIJUA ANAYEPANUA HOZI (TERRITORY) YA MTU NI BWANA

Habari za Yabesi hazikuandikwa sana lakini maandiko yanaonyesha kuwa Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze; na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa huzuni. 1 Mambo ya Nyakati 4:9

1 Mambo ya Nyakati 4:10 [Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishiahozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.]

Mungu atanue nafasi yako katika sekta au nafasi uliyoitiwa, katika territoty uliyopo katika jina la Yesu…


Haijalishi umenenewa nini, umeitwa jina gani, umeaminishwa nini juu yako… Kama Yabesi aliyeitwa na kuungamanishwa na huzuni alichomoka kwa kumuomba Mungu Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishiahozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! IWE KWAKO KWA JINA LA YESU…BWANA ABADILI MAJIRA YAKO.. UPANUKE NA KUIMARIKA PANDE ZOTE..

SASA OMBA KWA MANENO YAKO

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment