Saturday, January 14, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 14

SIKU YA 14 - 14/01/2017
Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

NAJITENGA NA UFUKARA NAJIUNGAMANISHA NA UTELE

Kuna watu wanajisikia raha kuwa masikini, lakini pia wanaumia wanaposhindwa kuwasaidia watu wenye uhitaji…. Ni hivi wanafanya kama Yakobo 2:15-16

Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini?

Lakini Mhubiri anaongezea pia Mhubiri 9:16 Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi

Kumbukumbu la Torati 8:18 Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

2 Wakorintho 8:9 Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

NI MPANGO WA MUNGU KUTAJIRISHWA KATIKA VITU VYOTE…. Kwa sababu ina kazi kwa Mungu 2 Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.

ADUI ANAPENDA UOKOKE LAKINI USIWE NA CHOCHOTE, MUNGU AKAMWAMBIA MUSA Kutoka 3:21 Nami nitawapa watu hao kufadhiliwa mbele ya Wamisri; hata itakuwa, hapo mtakapokwenda zenu hamtakwenda kitupu;

LAKINI FARAO AKA REACT MUSA AKASEMA Kutoka 10:9 Musa akamjibu, Tutakwenda na vijana wetu na wazee wetu, na wana wetu, na binti zetu, tutakwenda na kondoo zetu na ng'ombe zetu; kwa kuwa inatupasa kumfanyia Bwana sikukuu.

BAADA YA PIGO ………… Kutoka 10:24 Farao akamwita Musa, na kumwambia, Haya, nendeni, mkamtumikie Bwana; kondoo zenu na ng'ombe zenu tu na waachwe; watoto wenu nao na waende pamoja nanyi.

KIRI NA UOMBE….. USIMPE ADUI AKUZUIE USIINGIE KATIKA UTELE…
Zaburi 23:1 Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. KUBALI KUONGOZWA NA BWANA KWANI Zaburi 23:2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

MUNGU amenipa nguvu za kupata utajiri; Nimetajirishwa katika vitu vyote ili niwe na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yangu

Kama Yohana alivyoomba 3 Yohana 1:2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo. Zaburi 34:9-10

Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema. WATAKUWA NAVYO TELE

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

MWAKA 2017 UIMARISHWE KWENYE KIPATO CHAKO….


SASA OMBA KWA MANENO YAKO

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment