Tuesday, January 31, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 31

SIKU YA 31 - 31/01/2017
NINAMSHUKURU BWANA, KWA KUSIKIA NA KUJIBU MAOMBI YANGU
MUNGU HUWA ANAJIBU MAOMBI, HAKUNA OMBI LOLOTE AMBALO MUNGU HAKUWAHI KUJIBU

MAANDIKO YAWEKA WAZI…

Mathayo 7:8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
*Marko 11:24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.
MUNGU HASIKII TU LAKINI HUSABABISHA NAFASI YA TUKIO ULILOOMBA LIWE HALISI

Zaburi 118:5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
MUNGU ANA NJIA YAKE YA KUHAKIKISHA ANATUPA MAHITAJI YETU HATA KAMA TUMEISHIWA MBINU KABISA…

Warumi 11:33 Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!
EE MUNGU AHSANTE KWA MAOMBI HAYA (TAJA MAMBO ULIYOYAOMBEA)………….. NA KWA KUWA WEWE UNAJIBU NA HATA SASA UMEJIBU… NIMEYAPOKEA YOTE NILIYOOMBA.. NAISHI KATIKA AHADI ZANGU AMBAZO NI ZA KWELI DAIMA… KATIKA JINA LA YESU
Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu 

TUONANE JUMAMOSI HII MLIMANI DULUTI, WALETE WENYE MAHITAJI AU UKIWA NA HITAJI LAKO TUPATIE TUKUOMBEE

AMEN

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment