Monday, January 23, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 21

SIKU YA 21 - 21/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

2017 NAKIRI NA KUMTAMBUA MUNGU KWENYE MAFANIKIO YANGU

RECOGNITION OF GOD’S PURELY SUPPORT IN OUR SUCCESS

Kati ya jambo gumu litakaloipata kizazi chetu katika nyakati hizi ni watu kuhisi wamejiwezesha kufanikiwa kwa sababu ya kufundishwa sana juu ya SELF-HELP STRATEGIES pamoja na kujaa kwa SELF-HELP BOOKS ambazo zimejikita kuonyesha kwamba MUNGU SIYO MUHIMU kwenye njia ya mafanikio… Lakini KATIKA KWELI YOTE Mungu ndiye anayefanikisha na Mungu ndiye anaye-reward kazi zetu zote…

Kinachotufanikisha siyo akili zetu siyo uwezo wetu, siyo connections zetu nk. Bali ni Bwana.. Mithali 3:5-6 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.

Pamoja na kwamba Daudi alirusha jiwe kwa kombeo lake hakusema yeye ndiye aliyemuua Goliathi ijapokuwa wanawake mjini walisema 1 Samweli 18:7 Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake.

Katika njia zake, Daudi alimkiri Bwana… ANGALIA ALIVYOFANYA 1 Samweli 17:45-47 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana. Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli. Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.

UNACHOTAKIWA KUJUA NI KWAMBA 1 Samweli 2:7-8 Bwana hufukarisha mtu, naye hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu. Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Humpandisha mhitaji kutoka jaani, Ili awaketishe pamoja na wakuu, Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu; Kwa maana nguzo za dunia zina Bwana, Naye ameuweka ulimwengu juu yake.

Hata maandiko mengine yanasema Kumbukumbu la Torati 8:12-13 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake; na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

USIJE UKAWAHI KUJIONA KWAMBA I MADE IT … MY SELF-EFFORTS…. 

Kumbukumbu la Torati 8:17-18 Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo. Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

WANA WA ISRAEL PAMOJA NA KWAMBA WALIPIGANA KUELEKEA NCHI YA AHADI LAKINI WALIKUWA MAKINI KUWAELEKEZA WATOTO WAO KWAMBA Zekaria 4:6 Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. 

BALI HII NDIYO HADITHI WALIZOWAAMBIA WATOTO WAO… Zaburi 44:1-3 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu Baba zetu wametuambia, Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale. Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa, Ukawakalisha wao. Wewe uliwatesa watu wa nchi, Ukawaeneza wao. Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi, Wala si mkono wao uliowaokoa; Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako, Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.

ANAYETOA MAFANIKIO NI MUNGU SIYO SHETANI? YA AINA YOYOTE? 

KWA NINI BASI WATU WAKIENDA KWA WAGANGA WANAFANIKIWA?

Adui (shetani) huwa anasimama kupinga watu wa Mungu wasipokee kutoka kwa Mungu wala Yeye hatoi chochote.. (soma Yakobo 1:17, 1 Wakorintho 16:9) Kumbuka Daniel na majibu mazuri ya maombi yake.. Danieli 10:13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi 

KWA HIYO ILI SHETANI AACHIE ANAHITAJI MAMBO MAWILI

1.KUPIGWA ASOGEE NJIANI (Angalia Daniel aliendelea kupigana na malaika nao wakawa kazini) 
2.KUABUDIWA/KUSUJUDIWA- Ndiyo maana alimwambia Yesu.. amsujudu ili apewe vyote bila fight yoyote.. Luka 4:7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.

OPTION YA PILI NI RAHISI LAKINI INA MADHARA MAKUBWA HUWA ZINAWATOKEA PUANI.. 

Ya kwanza ni option sahihi sana…. Yakobo 4:7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

MUNGU NDIYE KILA KITU… SIYO SHETANI, SIYO NGUVU ZETU, SIYO AKILI ZETU….
NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

MWAKA 2017 SITAISHI KWA KUTEGEMEA AKILI ZANGU, WALA NGUVU ZANGU, NITAMTUMAINI BWANA NAYE ATANITENGENEZEA NJIA, NA KATIKA NJIA ZANGU ZOTE NITAMKIRI YEYE… TUTAWAAMBIA WATOTO WETU, WEWE NDIYE ULIYETUTAJIRISHA, WEWE NDIYE ULIYETUPA VYOTE KATIKA JINA LA YESU

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment