Friday, January 13, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 12

SIKU YA 12 - 12/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

KUSHINDA KUDUMAA/OVERCOMING STAGNATION


Kuna watu wanapita sehemu moja kwa muda mrefu bila kujua kwanini wanashindwa kutoka, au kwa kukosa njia ya kutokea… changamoto kubwa ni pale ambapo wao wenyewe wameanza kuchukia hiyo hali. Hiyo ni dalili nzuri kwamba unatakiwa kwenda mahali pa juu Zaidi… MUNGU ANAWEZA KUKUPA PASSWORDS ZA KUKUTOA HAPO…

Yakobo alikaa kwa Labani akaona amekwama kwa muda mrefu MALAIKA AKAMLETEA FURSA ILIYOMTOA Mwanzo 31:11-12

Na malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, Yakobo! Nikasema, Mimi hapa.

Akasema, Inua, basi, macho yako, ukaone; mabeberu wote wanaopanda wanyama wana milia, na madoadoa, na marakaraka; maana nimeona yote aliyokutendea Labani.

LABAN ALIBADILI MSHAHARA WA YAKOBO MARA KUMI Mwanzo 31:41 Miaka hii ishirini nimekaa nyumbani mwako; nilikutumikia miaka kumi na minne kwa binti zako wawili, na miaka sita kwa wanyama wako, nawe umebadili mshahara wangu mara kumi.

Mwanzo 30:43 Kwa hiyo mtu huyo akazidi mno, akawa na wanyama wengi, na vijakazi, na watumwa, na ngamia, na punda.

RIPOTI KWA ESAU INASEMA Mwanzo 32:5 nami nina ng'ombe, na punda, na kondoo, na watumwa, na vijakazi; nami nimepeleka watu nimpashe bwana wangu habari, nipate neema machoni pako.

BAADA YA KUKWAMA SIKU NYINGI Kumbukumbu la Torati 2:1-2

Ndipo tukageuka, tukashika safari yetu kwenda jangwani kwa njia ya Bahari ya Shamu, kama alivyoniambia Bwana; tukawa kuizunguka milima ya Seiri siku nyingi.

Bwana akanena, akaniambia,

MUNGU ANAWAPA PASSWORD

Kumbukumbu la Torati 2:3 *Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini.*

YUSUFU ALIKAA GEREZANI MPAKA MUNGU ALIPOMPA PASSWORD YA KUTAFSIRI NDOTO (KUMBUKA HATA ILE YA KWAKE ALIYOIOTA HAKUWEZA KUITAFSIRI BADALA YAKE ALIIPELEKA KWA BABA YAKE) 


MUNGU AKUONGEZE UWEZO 2017 AMBAO HUKUWAHI KUWA NAO…

Mwanzo 41:38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?

Mwanzo 41:42 Farao akavua pete yake ya muhuri mkononi mwake, akaitia mkononi mwa Yusufu; akamvika mavazi ya kitani nzuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake.

Mwanzo 41:41 Farao akamwambia Yusufu, Tazama, nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri.

MUNGU ANAWEZA AKAKUWEKA PANAPO NAFASI…*

Zaburi 31:8 Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha panapo nafasi.

MUNGU AKUONYESHE FURSA ITAKAYOKUTOA… AKUPE NAFASI ILI UONE NJIA SAHIHI YA KUPITA… KAMA UMEKWAMA SEHEMU MUNGU Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni. Zaburi 20:2
MWAKA 2017 HAUTAKWAMA KATIKA JINA LA YESU….

SASA OMBA KWA MANENO YAKO


Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment