Tuesday, January 17, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 17

SIKU YA 17 - 17/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

KWA NINI HOFU SIYO KIKWAZO KWAKO

Warumi 8:15 Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
2 Timotheo 1:7 Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

UKIONA UNA ROHO YA HOFU UJUE IMETOKA KWA ADUI KWANI MUNGU HAJAKUPA HIYO ROHO KWA HIYO LAZIMA UPINGANE NAYO

MUNGU HUTUPA roho ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi WALA HATUNA roho wa utumwa iletayo hofu; bali tulipokea (kwa Mungu) roho ya kufanywa wana….. WANA WAKO HURU… 

SABABU KWA NINI HUPASWI KUOGOPA

KUNA SABABU NYINGI ZA WATU KUTAKIWA KUOGOPA...

1 Samweli 22:23 Kaa wewe pamoja nami, usiogope; kwa maana yeye atafutaye roho yangu, ndiye atafutaye na roho yako; nawe utakaa kwangu salama.

2 Wafalme 6:16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.

1. BWANA NDIYE AKUFANIKISHAYE…

Zaburi 49:16 Usiogope mtu atakapopata utajiri, Na fahari ya nyumba yake itakapozidi.

HAUKO PEKE YAKO BWANA YUKO KAZINI NA WEWE…

Isaya 41:10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

1 Petro 5:7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

YESU ALISEMA Mathayo 28:20 …… na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. YAANI JANA, LEO NA KUENDELEA

Zaburi 4:8 Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.

2. MUNGU ANAWEZA KUKUEPUSHA NA AIBU

Isaya 54:4 Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena

3. KUMTUMAINI BWANA HUONDOSHA MBALI HABARI MBAYA…..NA HATA IKIJA HAUTATIKISIKA WALA KUOGOPA

Zaburi 112:7 Hataogopa habari mbaya; Moyo wake u imara ukimtumaini Bwana.

Zaburi 23:4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

4. MALAIKA WAKO KAZINI KUHAKIKISHA USALAMA WAKO WALA HATUJILINDI...

Zaburi 34:7 Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Zaburi 91:5 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,

5. BWANA NDIYE TEGEMEO LETU SIYO WATU…..HATA KAMA WANAWEZA KUTUSAIDIA BWANA ANAWEZA KUMTUMIA MTU/KITU CHOCHOTE

Waebrania 13:6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

Yeremia 17:7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.

Mithali 29:25 Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama. 

Zaburi 125:1-2 Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele. Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele. 

Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa……….MUNGU YUKO PAMOJA NAMI SIKO PEKE YANGU…. Sitaogopa habari mbaya; Moyo wangu u imara namtumaini Bwana……. walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao… Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami.. Sitaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

MWAKA 2017 NATEMBEA NA KUFANYA MAMBO YANGU KWA UJASIRI..…. MWENYE HAKI NI JASIRI KAMA SIMBA

SASA OMBA KWA MANENO YAKO* KAMA UNA TATIZO LA HOFU AU WOGA WA AINA YOYOTE, OMBA

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment