Thursday, January 19, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 19

SIKU YA 19 - 19/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

2017 KOMBOA WAKATI NA KUPINGA WANAOKULA MUDA WAKO

NZIGE, NA PARARE, NA MADUMADU, NA TUNUTU, JESHI KUBWA LILILOKULA MUDA WAKO… mwaka 2016 

LAKINI NAJUA UNAWEZA KUKOMBOA… Waefeso 5:16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

NA BWANA ANAWEZA KUKURUDISHIA Yoeli 2:25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.

HILI SIYO SUALA LA UMRI ULIOPOTEA BALI NI MATOKEO YA KAZI ILIYOFANYIKA AMBAYO HAIONEKANI….. Mithali 14:23 Katika kila kazi mna faida; I WAPI FAIDA YA KAZI ZAKO??...

Yoeli 1:2-4 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine. Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.

UKISOMA MISTARI YA CHINI UTAGUNDUA KUNA VITU VINGI VIMEHARIBIWA Yoeli 1:7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe. ANGALIA TENA Yoeli 1:17 Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka. ALIPOFIKA MLANGO WA PILI BAADA YA KUMLILIA BWANA Yoeli 1:19 Ee Bwana, nakulilia wewe; Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani, Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.

HAYA NDIYO MAJIBU YAKE…. Yoeli 2:25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.

JE, WATARUDISHIWA 2015 AU 2014? HAPANA… NI NGUVU KAZI ILIYOPOTEA
REDEMPTION/RECLAMATION/RESTORATION…

Kwa mfano: Kama ulitakiwa leo….uwe na nyumba na bado huna… na kujenga kikawaida hutumia miezi 6 REDEMPTION hukufanya urudishie kwa speed NYUMBA na vitu ambavyo unatakiwa kuwa nazo leo….ambavyo ADUI ALIZIHARIBU AU KUZIBANIA…

MFANO MWINGINE.. Kama leo ungezaa mtoto mmoja mmoja ulitakiwa kuwa na watoto watatu… REDEMPTION hukupatia MAPACHA WATATU (TRIPLETS) 

Hapa wale ulioanza nao halafu ulipopotea wakakuacha huwa wanajiuliza, kha mbona juzi tu ndo kaanza? 

HAPA SIO KURUDISHIWA SIKU BALI PRODUCTIVITY (MAZAO) YA SIKU ZAKO ZILIZOPOTEA.. 

UKIMUOMBA MUNGU AKOMBOE VITU VYAKO, HIVYO NDIVYO ZITAKAVYOFANYIKA IN JESUS NAME

*NAPINGANA NA KILA JAMBO LINALOWEZA KULA UWEZO WANGU WA KUZALISHA KATIKA JINA LA YESU, NAKOMBOA VYOTE NILIVYOPOTEZA KATIKA JINA LA YESU, NACHUKUA SPEED SAWA SAWA NA NILIVYOPOTEZA KATIKA JINA LA YESU… KILA ZAO LANGU LA HAKI LINANIRUDIA… SITAPOTEZA TENA KATIKA JINA LA YESU*

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

MWAKA 2017 KOMBOA WAKATI NA KUPINGA WANAOKULA MUDA WAKO


SASA OMBA KWA MANENO YAKO

KAMA UNA TATIZO KUMALIZA SIKU HALAFU UNASHANGAA HAKUNA IMPACT YOYOTE YAANI KAMA VILE ULIRUKA SIKU HIYO…OMBA, KEMEA, PANGA MUDA WAKO VIZURI, ANGALIA MUDA WAKO UNAVYOTUMIKA ILI USIPOTEZE TENA, ACHANA NA MAMBO YASIYO NA MBELE WALA NYUMA

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment